Uchaguzi 2020 CHADEMA: Tutaishinda CCM jinsi ilivyo. Ng'ombe huyu mara hii hageuziwi Kibla, anachinjwa alivyolala

CHADEMA

JF-Expert Member
Apr 13, 2013
488
2,468


"Serikali inayoogopa watu, serikali inayoishi kwa uongo haiwezi kushinda kura. Na mimi niwaambie na hiyo meseji iwafikie, uchaguzi huu tunaenda hakuna wa kujitoa. Uchaguzi huu tunaenda, tunajua hakuna Tume Huru (ya Uchaguzi).

Tunajua wanatunga sheria zozote wanazotunga. Tumeamua tuache watunge sheria yoyote, kusiwe na Katiba, kusiwe na Tume Huru, uchaguzi tunakwenda kushindia kituoni. Wanataka hawataki, watatutangaza.

Nani anawadanganya kwamba hamtatangazwa? Toka lini CCM na serikali yake, toka lini walikuwa na mpango wa kuwatangaza wapinzani? Haijawahi kuwa nao, hawana, hawatakuwa nao. Tutawashida hivyo hivyo.

Ng'ombe huyu mara hii anachinjwa alivyolala, akilala kifudifudi, tunachinja kuanzia mgongoni. Akilala kiubavu, tunachinja kiubavu. Huyu tunachinja alivyolala. Tutawashinda wanapenda hawapendi."

Mhe. Benson Kigaila, Naibu Katibu Mkuu Chadema, Bara.
 
"Serikali inayoogopa watu, Serikali inayoishi kwa uongo haiwezi kushinda kura. Na mimi niwaambie na hiyo meseji iwafikie. Uchaguzi huu tunaenda hakuna wa kujitoa. Tunaenda tunajua hakuna Tume Huru ya Uchaguzi. Tunajua wanatunga sheria zozote wanazotunga," Mhe. Kigaila, NKMB

Tumeamua tuwaache watunge sheria yoyote. Kusiwe na Katiba au Tume Huru, uchaguzi tunakwenda kushindia kituoni. Wanataka hawataki, watatutangaza. Nani anawadanganya kwamba hamtatangazwa? Toka lini CCM na serikali yake walipanga kuwatangaza wapinzani?," Mhe. Kigaila Benson, NKMB.

"Haijawahi kuwa nao, hawana, hawatakuwa nao. Tutawashida hivyohivyo. Ng'ombe huyu mara hii anachinjwa alivyolala. Akilala kifudifudi tunachinja kuanzia mgongoni, akilala kiubavu tunachinja kiubavu. Huyu tunachinja alivyolala. Tutawashinda wanapenda hawapendi," Mhe. Kigaila, NKMB.
 
Quinine,
Mh, nachelea kusema kuwa akiamua kutangaza anayempenda unafanyaje? Tulifikirie kwa mapana na marefu! Watafanya hivyo kama serikali za mitaa. Quinine unalionaje hili?
 
Mh, nachelea kusema kuwa akiamua kutangaza anayempenda unafanyaje? Tulifikirie kwa mapana na marefu! Watafanya hivyo kama serikali za mitaa. Quinine unalionaje hili?
Uko sahihi mheshimiwa. Naona mazingira yaliyotawala uchaguzi wa serikali za mitaa yatajirudia. Wagombea wa vyama vya upinzani makini hawatapitishwa na Tume ya Uchaguzi kwa visingizio mbalimbali.

La sivyo wakishinda kwenye sanduku la kura hawatatangazwa washindi. Hii tayari imesukwa ndani ya taratibu mpya ya maadili ya uchaguzi ambayo wapinzani walishurutishwa kutia saini (wawakilishi wa vyama kwenye kituo cha kupigia kura kutopewa nakala ya matokeo).
 
Wanasema, ukikubaliana na boss Kufanya kazi yake maana yake umeishajiridhisha, ugumu wa kazi na kila Aina ya usumbufu wake

Sasa Manung'uniko na kelele zikizidi unaitwa wewe ni muoga na Ile kazi utaonekana tayari ilishakushinda kabla ya kuianza

Punguzeni kulalamika ijulikane moja kuwa ninyi ni wanaume
 
Nimemuelewa.

Kusubiri fadhila kutoka CCM ni kupoteza muda, na kususia uchaguzi hakusaidii kama ilivyoonekana kwenye serikali za mitaa.

Dawa ni kwenda kushindana nao huko huko kwenye vyumba vya majumuisho ya kura na kumtangaza mshindi, mbivu na mbichi zijulikane hukohuko, atakaekubali haki yake kunyan'ganywa afanye hivyo, but atleast not without a fight.

Sometimes haki inatafutwa, huletewi kwenye sahani.
 
tindo , Salary Slip , Retired , Erythrocyte kama mna kumbukumbu nzuri huu ndiyo ulikuwa ushauri na msimamo wangu kamwe CHADEMA wasisusie uchaguzi na kuwapa washindani wao ushindi kwenye sahani ya fedha (not to give or serve CCM everything on a silver platter).

Kususia uchaguzi Tanzania ni sawa na kujimaliza kisiasa, matokeo tumesha yaona kule Zanzibar na huku Tanganyika kwenye chaguzi za kujaza nafasi kwenye majimbo na udiwani na kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa.

Kususia uchaguzi kunafanya kazi kwenye nchi ambazo maslahi ya mabeberu yameguswa hivyo beberu anataka kulinda maslahi yake au kulipa kisasi kwa gharama yeyote ile.

Kwa Tanzania beberu kashikwa pabaya na ndiyo maana bado hawajafanya udhalimu wao kwa kiwango kikubwa. Ukiigusa na kuivuruga Tanzania unaenda kuvuruga na kutibua 'equilibrium' inayowezesha mabeberu wafanye shughuli zao kwenye nchi za ukanda huu, zile nchi ambazo zinaizunguka Tanzania (hasa Tanganyika).

Ukiivuruga Tanzania basi ujue unaenda kutengeneza ukanda mwingine hatari sana kwa usalama wa dunia, maana eneo hili ndiyo linaenda kuzalisha maghaidi wengi sana na hata wasiokuwa maghaidi lakini wenye kuvuruga maeno ya uwekezaji wa mabeberu wataongezeka.

Kwa maana hiyo kususia uchaguzi na kutegemea CHADEMA itapata msaada toka nje wa kuivamia Tanzaina na kuitoa madarakani serikali iliyopo haitawezekana kamwe, njia pekee ni kushiriki chaguzi na hakika lazima baadhi yamaeneo CHADEMA au upinzani kwa ujumla utashinda na kupata wawakilishi wa kuendeleza kupigia kelele muhimu bungeni, zile kelele za kuleta mabadiliko.
 
fanyeni yote na piganeni weeee ila Mwananchi anahtaji maji, umeme hospitali na huduma nyingne muhimu za jamii..chaguzi uwe huru usiwe huru mtajuana wenywe tu
 
Nimemuelewa.

Kusubiri fadhila kutoka CCM ni kupoteza muda, na kususia uchaguzi hakusaidii kama ilivyoonekana kwenye serikali za mitaa.

Dawa ni kwenda kushindana nao huko huko kwenye vyumba vya majumuisho ya kura na kumtangaza mshindi, mbivu na mbichi zijulikane hukohuko, atakaekubali haki yake kunyan'ganywa afanye hivyo, but atleast not without a fight.

Sometimes haki inatafutwa, huletewi kwenye sahani.
Haswaaaaa..wanatutisha tu hao pimbi..watatutangaza tu
 
tindo , Salary Slip , Retired , Erythrocyte kama mna kumbukumbu nzuri huu ndiyo ulikuwa ushauri na msimamo wangu kamwe CHADEMA wasisusie uchaguzi na kuwapa washindani wao ushindi kwenye sahani ya fedha (not to give or serve CCM everything on a silver platter).

Kususia uchaguzi Tanzania ni sawa na kujimaliza kisiasa, matokeo tumesha yaona kule Zanzibar na huku Tanganyika kwenye chaguzi za kujaza nafasi kwenye majimbo na udiwani na kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa.

Kususia uchaguzi kunafanya kazi kwenye nchi ambazo maslahi ya mabeberu yameguswa hivyo beberu anataka kulinda maslahi yake au kulipa kisasi kwa gharama yeyote ile.
Kwa Tanzania beberu kashikwa pabaya na ndiyo maana bado hawajafanya udhalimu wao kwa kiwango kikubwa.
Ukiigusa na kuivuruga Tanzania unaenda kuvuruga na kutibua 'equilibrium' inayowezesha mabeberu wafanye shughuli zao kwenye nchi za ukanda huu, zile nchi ambazo zinaizunguka Tanzania (hasa Tanganyika).

Ukiivuruga Tanzania basi ujue unaenda kutengeneza ukanda mwingine hatari sana kwa usalama wa dunia, maana eneo hili ndiyo linaenda kuzalisha maghaidi wengi sana na hata wasiokuwa maghaidi lakini wenye kuvuruga maeno ya uwekezaji wa mabeberu wataongezeka.
Kwa maana hiyo kususia uchaguzi na kutegemea CDM itapata msaada toka nje wa kuivamia Tanzaina na kuitoa madarakani serikali iliyopo haitawezekana kamwe, njia pekee ni kushiriki chaguzi na hakika lazima baadhi yamaeneo CDM au upinzani kwa ujumla utashinda na kupata wawakilishi wa kuendeleza kupigia kelele muhimu bungeni, zile kelele za kuleta mabadiliko.
Nitarudi
 
Chadema wanawaanda tu wafuasi wao ili wakishindwa wapate sababu
Kama unaona mazingira sio mazuri,usiingize timu,lakini ukiweka wagombea maana yake unaamini utashinda kwa tume hiyo.hiyo,tusidanganyane
 
Back
Top Bottom