CHADEMA tujipange kwa ajili ya 2025, hatujachelewa

Countrywide

JF-Expert Member
Mar 2, 2015
18,173
27,223
Habari wana JF,

Poleni kwa wote ambao matokeo yamewaumiza.

Ipo hivi, kwenye mambo kama haya kuna kushinda na kushindwa hivyo ni vyema tukapunguza hasira na kuangalia tunafanyaje kwenye chaguzi zijazo.

Ila natoa rai kwa wana Chadema wenzangu, tupunguze ujuaji, matusi, kebehi na dhihaka za kila namna.

Kabla ya matokeo wengi tuliona humu jinsi maneno yetu yalivyo makali, tujirekebishe hapo.

Ninatoa rai kwa chama kujipanga kwa ajili ya 2025, kuchanika kwa jamvi sio mwisho wa maongezi.

Mipango isukwe vizuri na pia kweli tuwe na nia ya kushika dola. Mara kadhaa humu nilikuwa nikishangaa tunawezaje kushinda uchaguzi kama huu ikiwa ni kama tumekurupushwa tu? Nikaishia kutukanwa kila aina ya tusi. Yote kwa yote tujipange, kwenye kushika dola hakuna shortcut.

Mwisho, ninamuomba Mh. Rais Magufuli akiona inafaa ampe ubunge wa viti maalum(vile 10) Mh Mbowe. Mbowe anaweza kuchaguliwa hata kama yupo Chadema, ishawahi kutokea kwa Mbatia.

Hivyo kwa unyengekevu ninamuomba Mh. Rais amteue Mbowe kuwa mbunge wa viti maalum.

Nawasilisha
 
Ateuliwe Mbowe ili aweze kusimangwa live na Speaker? Na abebeshwe lawama mambo yakienda sivyo? Na mbaya zaidi, aonekane kuwa kweli alikuwa ni mchumia tumbo tu!

Nadhani kuna watu wengi wa vyama vya upinzani ambao nafasi hiyo itawafaa sana. Wakina Lipumba, Mrema, Cheyo, Mbatia n.k.

Amandla...
 
Utakuwa ni mpumbavu wa kiwango cha juu sana kama utakubaliana na hiki alichofanya Magufuli. Mtu anaifanya nchi yenu kuonekana kituko mbele ya nchi zingine na nyie mnaona sawa! Sioni faida ya Tanzania kuitwa nchi yenye uhuru.
 
Viti maalum vya Rais baadhi ya wapinzani watapewa ila sio Mbowe na wenzie wenyekashfa na kebehi kwa Rais na serikali yake.
 
Utakuwa ni mpumbavu wa kiwango cha juu sana kama utakubaliana na hiki alichofanya Magufuli. Mtu anaifanya nchi yenu kuonekana kituko mbele ya nchi zingine na nyie mnaona sawa! Sioni faida ya Tanzania kuitwa nchi yenye uhuru.
Hii nchi inaheshimika sana ndugu hizo ni hisia zako tu. Nchi hii inajulikana kimataifa sasa sababu ya Magufuli, tena inajulikana kwa maendeleo yake ya kasi sana. Hata hivyo una uhuru, unaweza kuhamia kwa marafiki waliokuambia nchi haiheshimiki maana huenda mnafanana na mnaweza kuwaza kwa hisia wote.
 
Habari wana JF,

Poleni kwa wote ambao matokeo yamewaumiza.

Ipo hivi, kwenye mambo kama haya kuna kushinda na kushindwa hivyo ni vyema tukapunguza hasira na kuangalia tunafanyaje kwenye chaguzi zijazo.

Ila natoa rai kwa wana Chadema wenzangu, tupunguze ujuaji, matusi, kebehi na dhihaka za kila namna.

Kabla ya matokeo wengi tuliona humu jinsi maneno yetu yalivyo makali, tujirekebishe hapo.

Ninatoa rai kwa chama kujipanga kwa ajili ya 2025, kuchanika kwa jamvi sio mwisho wa maongezi.

Mipango isukwe vizuri na pia kweli tuwe na nia ya kushika dola. Mara kadhaa humu nilikuwa nikishangaa tunawezaje kushinda uchaguzi kama huu ikiwa ni kama tumekurupushwa tu? Nikaishia kutukanwa kila aina ya tusi. Yote kwa yote tujipange, kwenye kushika dola hakuna shortcut.

Mwisho, ninamuomba Mh. Rais Magufuli akiona inafaa ampe ubunge wa viti maalum(vile 10) Mh Mbowe. Mbowe anaweza kuchaguliwa hata kama yupo Chadema, ishawahi kutokea kwa Mbatia.

Hivyo kwa unyengekevu ninamuomba Mh. Rais amteue Mbowe kuwa mbunge wa viti maalum.

Nawasilisha
Kwa katiba hii ambayo Rais ni mteule wa kila mtu usitegemee jipya, Chadema kama chama kimetutoa matongotongo kuhusu namna serikali inavyotufisadi, nachokiona baada ya miaka 2 itakuwa ni kubadili katiba
 
Kamanda unaandamana saa ngapi?
Ateuliwe Mbowe ili aweze kusimangwa live na Speaker? Na abebeshwe lawama mambo yakienda sivyo? Na mbaya zaidi, aonekane kuwa kweli alikuwa ni mchumia tumbo tu!

Nadhani kuna watu wengi wa vyama vya upinzani ambao nafasi hiyo itawafaa sana. Wakina Lipumba, Mrema, Cheyo, Mbatia n.k.

Amandla...
 
Back
Top Bottom