CHADEMA si kimbilio la wasomi!

CHADEMA si kimbilio la wasomi!

Tafadhali moderators ondoeni hii thread kwakuwa utimamu wa mtoa mada una walakini.
 
Kelele nyingi zimepigwa eti CHADEMA inatamba vyuo vikuu na kuzoa wanachama wengi wasomi.

Tafiti tulizozifanya kwa wanachama hai wa CHADEMA zinaonyesha takwimu tofauti kabisa. Wanachama wengi wa CHADEMA ni vijana wa vijiweni wasiopenda kazi na waqkati wao mwingi huupoteza kwa kutia gumzo na kuleta hadithi za alinacha.

Kiwango cha elimu cha wanachama wengi wa CHADEMA ni kuanzia darasa la saba mpaka kidato cha nne na baadhi ya form six failure kama inavyojieleza kwa Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe. Na ndio maana CV zao zinapoanikwa hadharani kama Mh Sitta ALIVYOFANYA KWA Mh Mbowe, Mh Slaa akaanza kusema kuwa Sitta Kamdharau Mbowe. Jamani, Kukutangazia CV yako ndio dhambi.

Na kutokana na CV nyembamba za wanachama wa CHAMA hicho, ndio sababu kubwa ya chama hicho kuwa CHAMA CHA VURUGU NCHINI. Na hii inasababishwa na ueleo mdogo wa wanachama wake kutokana na elimu ndogo.

Fanya utafiti mdogo katika mji uliopo na utahakiki maneno yangu. Ukipata jibu ndio utaelewa kwanini CHADEMA HAIWEZI KUCHUKUA NCHI YETU.

CCM kimbilio la wasomi wapumbavu
 
kelele nyingi zimepigwa eti chadema inatamba vyuo vikuu na kuzoa wanachama wengi wasomi.

Tafiti tulizozifanya kwa wanachama hai wa chadema zinaonyesha takwimu tofauti kabisa. Wanachama wengi wa chadema ni vijana wa vijiweni wasiopenda kazi na waqkati wao mwingi huupoteza kwa kutia gumzo na kuleta hadithi za alinacha.

Kiwango cha elimu cha wanachama wengi wa chadema ni kuanzia darasa la saba mpaka kidato cha nne na baadhi ya form six failure kama inavyojieleza kwa mwenyekiti wa chadema, freeman mbowe. Na ndio maana cv zao zinapoanikwa hadharani kama mh sitta alivyofanya kwa mh mbowe, mh slaa akaanza kusema kuwa sitta kamdharau mbowe. Jamani, kukutangazia cv yako ndio dhambi.

Na kutokana na cv nyembamba za wanachama wa chama hicho, ndio sababu kubwa ya chama hicho kuwa chama cha vurugu nchini. Na hii inasababishwa na ueleo mdogo wa wanachama wake kutokana na elimu ndogo.

Fanya utafiti mdogo katika mji uliopo na utahakiki maneno yangu. Ukipata jibu ndio utaelewa kwanini chadema haiwezi kuchukua nchi yetu.

shhhhh zawadi usiseme kwa sauti kumbuka hawa unaowaita si wasomi ndo walimwingiza jk, utaharibu chama chetu cha kifisadi, na kumbuka ni asilimia zaidi ya 90% ya watanzania hawajafika chuo tafadhali tuishie huku kwenye udini na ukabila, sema sana chadema ni wachaga wa mbeya na wakristu wa lindi!
 
Sasa hao wasomi wa kiccm ccm wameifanyia nini nchi hii zaidi nya kujilimbikizia mali?
Je walioichagua ccm miaka yote ni wasomi?
Acha upambafu pambafu!!!!!!!!!!!!!!!
 
gamba at work, take an example of leaders of the party. Are they form six failure or not? By the way, kama uelewa ungekuwa mdogo wa wana chadema basi hoja zao zisingesikika kwa haraka kiasi hicho nchi nzima. Hata hivyo unataka kutuambia kwamba maeneo yote waliyochukua chadema nchini ni la saba hadi form six peke yake? Mbona unataka kudanganya umma? Kumbuka pia kwamba ccm ina wanachama wengi zaidi vijijini ambako hawana uelewa. Unasemaje kuhusu hilo?

mkuu kwenye blue hapo mambo yamebadilika hata vijijini hawaitaki ccm sijui wewe unasema kijiji kipi!?
 
Anaonekana ana muda wa kufanya utafiti lakini nina wasiwasi na ujuzi wa utafiti alio nao, na nini cha kutafiti. Kama anaona CDM ni ya Wahuni aiache, aende kutafiti vitu vingine.
 
naona ccm yenu ndo imejaa wasomi watupu mkiongozwa na msomi mkuu kuliko wote Livingstone Lusinde mkitoa speech majukwaani mnawakuna kina dada.
 
hakuna msomi anaweza kuwa na muda na chama cha vihiyo. Mnyika ni form six alipata division three halafu wakati wa uchaguzi akadanganya eti ana division 1 ya point 3. Jamani, kuna mbunge wa mpanda wa chadema yeye ni darasa la saba. Jiulize hawa chadema nani amewahi kuwa angalau mkuu wa wilaya. Maprofessor woote ni ccm angalia wakina mwandosa, wangwe, mhongo, tibaijuka. Sasa chade ma ni
professor baregu peke yake. Lweitama ni chakubanga hana sifa za kitaaluma. Kitila mkumbo ni pandikizi amesomea

education

acha ufenenge,profesa ,kahig,dr slaa,mnyika kasoma maua alipata one ya 3,na alifika chuo kikuu,halafu wasira anayelala usingizi bungeni,dhaifu mwenye phd ya kupew zawadi.mikataba feki ya madini na nishati nani aliingia kama sio wasomi wa mabwepande? Usom wao unawsaidia ni katika maisha na katika taifa? Shame on you gamba! Policcm,dhaifu,liwalo na liwe bila kumsahau nepi na magamba wote ,2015 mtaisoma kaniki hata kama haina maandishi.
 
Eti umefanya utafiti, wapi? na lini? We mwenyewe ni msomi? Mbona hata kijana bright wa darasa la saba anakuzidi. Halafu kwa taarifa yako kwenda shule sio lazima uwe umeelimika, ndio maana kuna watu wanaaitwe learned foools. Be careful my friend, utafiti wako ni feki. Kwanza msomi akiwepo CCM ujue ana lake jambo.
 
Majobless siku zote ndio wafata mkumbo, wao wala hawapimi maneno,ni kushabikia tu.
 
2015 ndio mtajua majobless wanafuata mkumbo au vipi,kwenye sanduku la kura hatuangalii kura ya professa au ya jobless.
Kwa thread kama hizi magamba mnajipalia mkaa.Asilimia kubwa ya watu wenye shida wamesababishiwa na magamba.
 
I feel like bursting!!!!!!
Hujawahi kujiuliza kwa nini wakati wa chaguzi kuu vyuo vya elimu ya juu havifunguliwi hadi uchaguzi upite???!!!!
Wanajua wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu ni mwiba mkali kwa ccm so hawapendi wapige kabisa kwa kuwa wanakuwa wamejiandikisha vyuoni so wakiwa wajumbani mwao hawawezi kupiga kura maana ni nje ya vituo vyao!!!!!
UTAFITI WAKO NI RABBISH!!!!!!!!!!!!
 
hata OBAMA alitokea kundi la walalahoi na yupo kwaajili ya kutetea walalahoi wenzake, ndivyo walalahoi wa CHADEMA ndivyo wanavyopigana kuwakomboa walalahoi wenzao ambao ni wengi, na hakika watashinda.
 
Waliomkaribisha Julius Nyerere na kumuonesha njia za kudai uhuru wa nchi hii hakuna hata mmoja aliyekuwa na elimu ya chuo kikuu, hawa ni aina ya watu kama akina Mzee Tambaza, Dossa Aziz, Sykes na wengine! watu wa aina hii ndio wenye uchungu na nchi yao maana imesemwa " aliyevaa viatu ndie ajuae wapi kinabana". hao unaowaita wasomi wengi kama sio wote ni wachumia tumbo tu, na ndio maana wanakimbilia CCM maana huko ndio kwenye watu wa aina yao, ni lini ulisikia msomi wa nchi hii anatetea au kukemea kwa dhati kabisa maovu ya nchi hii, hao wapiga kelele kama kina Benson Bana, Kapuya Mwandosya na wengine walivyopewa ulaji tu wakafunga midomo! Ukombozi siku zote huletwa na wanyonge, soma kitabu cha KULI (Shafi Adam Shafi), au very recently rejea vuguvugu la Occupy Wall Street (USA), Tahlil Square (MIsri) na Benghazi (Libya)! sasa hivi ni mapambano kati ya walionacho na tusiokuwanacho! Hatuhitaji kuwa na mashahada ya vyuo vikuu kujua ni kiasi gani tunanyonywa na kuibiwa!
 
Hao majobless wamezalishwa chini ya serikali ya chama cha mapinduzi toka tupate uhuru.

Serikali yenu imefanya nini kutatua hili tatizo.

Majobless wana ikimbilia cdm kwani wana imani nayo kuwa itawezesha kuwaondolea matatizo yao!
Majobless siku zote ndio wafata mkumbo, wao wala hawapimi maneno,ni kushabikia tu.
 
Mleta mada anasema asichokijua,

Toka mfumo wa vyama vingi umeingia nchini hakuna hata siku moja CCM iliongoza kwa kura kwenye kituo chochote cha uchaguzi kilichopo kwenye maeneo ya Vyuo vikuu.

Hivi hajui ni kwanini serikali iliamua kutunga sheria kuzuia siasa vyuoni?

Kama anabisha ajaribu kwenda chuo chochote halafu apime reaction ya wasomi kwa kusema kwa nguvu(shout) CCM oyeee.... VS Peopleeee's....
 
Back
Top Bottom