CHADEMA si kimbilio la wasomi!

CHADEMA si kimbilio la wasomi!

Teh...teh...ama kweli ccm imefika pabaya.Siku hizi mnaona fahari kujenga tabaka kati ya wasomi na wasiosoma?...mmesahau misingi ya kuthamini utu na usawa vitu ambavyo alivipiganie mwl.Nyerere.
 
mosi-mtoa hoja nivema ukaweka cv yakokwanza,pili-usiongee bila evidence,tembelea vyuo vikuu ujionee ukweli.udom,udsm,sauti etc.cdm inafnika.binafsi taasisi niliyopo hakuna mfuasi wa ccm anaejulikana ispokuwa cdm,wasomi wengi tz wako mijin matokeo yakoje?jiji la mwanza,mbeya,arusha ,dar, makabila yenye wasomi wengi na wachaga,wahaya,wanyaki,wasukuma +kerewe,wajita.khali ikoje maeneo yanapo patikana makabla hayo.istoshe hata unaodharau hawaja soma wameshindwa kupewa elimu na selikal ya ccm.hvyo sikosa lao ndomaana wako against ccm.istoshe jforum members walio weng ni cdm members kwa kukonsider ideoloji zao na hawa ndo wasomi.jiulize wangap wamekusapot ktk uz wako?
 
Tumewachoka chadema wanaoshabikia hawakijui undani wake ila ukiwa mchunguzi utagundua kile ni chama cha ukoo wa kaskazini mwa Tanzania.

Wakati mwingine muwe mnapumzisha utumbo wenu na kuzuia marudio, kwani pale alipo Kikwete?, Makamba, Nnauye, Malecela, Nyerere, Malima, Kagasheki, huo si ukoo?

Ulishajaribu kujiunga ukaambiwa hiki ni chama cha ukoo mmoja?

Kule America Bush Sr alikuwa rais, Bush Jr alikuwa Gavana Texas kabla ya kuwa rais, Bush mwingine alikuwa Gavana kule Florida.
 
Eti unaitwa Zawadi!kama hii ndo zawadi aliyoamua kutuletea watanzania heli angeichomoa tu hiyo mimba,,na hiyo mbegu iliyosabisha ukazaliwa bora baba yako angezipigia punyeto(kujichua)kuliko kukuzaa wewe,kwa taarifa yako me ni mmoja wa wasomi wa chuo kikuu,zaidi hapa chuoni Gwanda za kikamanda ni kama sale za chuo,kila darasa tumejaa makamanda,wanachadema na wengi wanakadi za CDM mpaka za kupigia kula,wewe kma ni msomi bt bado hayupo CDM,ujue ukoo wao magamba,nenda pale UDOM kisha umalizie SAUT utanenepa kwa hasira,japo usalama dhaifu wa ccm wapo na wanatupiga mikwala daily,hebu cheki kalenda,mwisho wa mwezi huu,isije CDM wakakusababishia round kuwa ndeeeeefuuuuuu. Nani aliikagua hiyo reseach?

Ungekuwa Smart, angalau kwa kujificha rangi yako USINGEANDIKA HAYA, maana hapa ndio umetoa lugha kamili ya KIJIWENI.

Si kosa lako na wala sina la kukushauri zaidi, ila moja ni la ukweli kuwa kama nyie mpo wengi katiika chama hiki. Pengine la kuwasaidia ni kuongeza bajeti ya ELIMU YA URAI ili mpate hata hicho kidoga ikiwa kama mtahudhuria.
 
Nisingetaka kujibizana na wanaJF kuhusu allegations kwamba CDM ni chama cha kikanda au kwamba mikakati yetu inaleta fujo au uvunjifu wa amani.

Ukweli unajionyesha katika matokeo ya chaguzi ambazo zimetupa Wabunge tangu Tanzania iingie katika mfumo wa vyama vingi vya siasa: Kigoma Mjini, Kigoma Kaskazini, Tarime, Mwanza, Ukerewe, Mbeya, Iringa, Singida na Dar es Salaam. Hizi ni sehemu ambazo tumeweza kuwa na majimbo yaliyowachagua wana-CDM tangia 1995. Sitaji Kilimanjaro na Arusha ambako ni chimbuko langu, na ilitegemewa ituelewe kwa urahisi zaidi.

Kuhusu fujo na tishio la uvunjifu wa amani, naweza kusema sio dhamira ya CDM kuleta fujo. Sera zetu zinaelezwa kwa mantiki na ufasaha. Viongozi wetu ni jasiri na wana uzalendo wa hali ya juu. Tuna huruma kwa wanyonge wanaotaabika kutokana na tunawapa ujumbe wa matumaini.

Inaonekana kwamba Serikali na CCM wameishiwa mbinu na mikakati ya kuleta maendeleo. Wamechoka.

Baya zaidi ni kwamba, jinsi inavyodhihirika wengi wao wamebakia kukwapua tu mali ya umma, wanalazimisha taasisi kama Polisi kutumia risasi za moto kutishia uhai wa wananchi wanaotuunga mkono. Chini ya Katiba ya sasa vyama vya siasa vina uhuru wa kuandamana kwa amani. Polisi jukumu lao ni kusindikiza maandamano hayo kuhakikisha amani na katika mikutano kuona kwamba watu wenye nia mbaya hawaleti fujo.

Ukweli kwamba wengi wa Wabunge wa CDM hawatoki vijijini, unatokana na historia na uchanga wetu. Nchi yetu ni kubwa na chama kichanga hakina uwezo wa kuwafikia wananchi wote wa vijijini. Katika kipindi hiki cha miaka 3 kufikia Uchaguzi Mkuu wa 2015 ni lazima mbinu zibuniwe kuwafikia Watanzania huko vijijini. Na helikopta nyingi zitahitajika.

Huyu nae ni mmoja wao.....wakule kule ukandani...."MTEI".

Subirini hukumu yenu kwa mungu kama mahakama zitaficha haki basi kule haki haifichwi.

Mmesababisha mauaji kwa kukusudia halafu mnajiona mna mikono misafi?
 
Mkuu Zawadi Ngoda, naomba kutofautiana na wewe kiasi fulani katika haya;

1. Kama msomi uliyefanya utafiti na kutumia pesa, nguvu, akili na muda wako/wenu..ni ajabu kusema UTATUCHOSHA na taarifa ya utafiti ulioufanya, then if ni hivyo why bringing up the topic at all?

-Uliposema "ulitegemea vijana wa vijiweni wasome"..ulimaanisha nini mkuu? kuwa wengine haiwafai? then itakuwa ulisahau kuandika title "kwa vijana wa vijiweni wa CHADEMA"..then kama ni vijana wa "vijiweni" wanapatikana huku jamvini mkuu?



2. Katika aya ya pili umesema utafiti ni mrefu na ungekosa mvuto?..Mkuu, naomba nikuulize swali ulishawahi kusoma hotuba ya Mh. Rais ya mwisho wa mwezi? vipi kuhusu taarifa za wizara za Bunge n.k ...nakuhakikishia ni NDEFU unaweza kutengeneza jarida!!

Ukaongelea suala "MVUTO" , ni mvuto upi unaousema? mvuto kwa nani? ni kipi bora kati ya mvuto au umakini wa taarifa?


3. Mkuu katika aya ya tatu umesema mimi ni "msomi pekee wa CDM" ..ningependa kukukumbusha kuwa siko CDM, lakini hadi sasa sijaona ubaya wa mimi kufikiria kuwa huko!


Kwa ushauri tu mkuu, ni ngumu..narudia tena ni ngumu sana, kushawishi watu kwa "ubaya" wa watu wengine kuliko kushawishi watu kwa mema uliyofanya/mliyofanya.

  1. Hakukuwa na haja ya kuandika "kwa vijana wa kijiweni" kwa vile walengwa ni CHADEMA, na asilimia zaidi yan 80 ya wanachama wake ni wa vijiweni. Hivyo nilijua watasoma tu. Na wamefanya hivyo, si unaona aslimia kubwa ya majibu yalivyojaa lugha za vijiweni, sina hata haja ya kuwataja kwa majina. Wanaoandika kwa kina kama wewe ni wachache sana tena ni chini ya 5%.
  2. Hilo la pili ni zuri sana, Amini usiamini, taarifa HIZO NDEFU ZA BUNGE ambazo unaweza kuandika jarida, HAKUNA KIJANA WA KIJIWENI ANAZISOMA. Kama walengwa ni watu wa kijiweni basi hutafanikisha kuufikisha ujumbe. Na hilo si lengo kabisa. Ni ngumu, na pengine haiwezekani kutoa taarifa ya kina (Umakini) kwa msomi ikawa na mvuto (kumvutia msomaji) kwa vijana wa vijiweni.- Hapa napo tumeshafanya utafiti wa kutosha. Hata taarifa ikawa na ukmakini sana kama msomaji hata haikaribii, hutafanikiwa hata dogo
  3. Hujachelewa, nenda kawaokoe. Maana hata Rais katika uzinduzi wake wa ujenzi wa Daraja la kigamboni alisema haya. (tafakari mwenyewe alikilenga chama gani?)
    "Rais Kikwete pia amewaonya watu ambao wamelifanya suala la kutunga na kusema uongokama sehemu ya utamaduni wao. “Watu wana viwanda vya kuzalisha uongo. Wanashinda wanasambaza uongo kwenye mitandao, kila mahali. Wamepata hata kusema kuwa mimi nimemuuzia George Bush eneo la Kigamboni. Bush aje kufanya nini Kigamboni

    Rais pia amesema kuwa wapo watu ambao hawapendi maendeleo ya nchi. “Wanatamanikila siku tushindwe kuwaletea wananchi maendeleo. Lakini watakufa kwa kihoro kwa sababu hatutashindwa. Kila tulilosema tutalifanya, litafanyika”.

    Amesema kuwa thamani kubwa ya vyama vya siasa ni maendeleo ya wananchi. “Lakini wapo wenzetu ambao wanaudhika wakiona maendeleo. Wanapenda hata daraja hili lisijengwe. Leo hawatalala usingizi. Kazi ya vyama vya siasa ni kuweka maslahi yetu sote mbele.”
 
Mkuu Zawadi Ngoda, nadhani kuna kati ya mambo mawili either hukunielewa au ulinielewa lakini unaepuka kujibu maswali yale niliyokuuliza kwa umakini hasa katika post#230.(Apologies sikuweza kui-quote)


1. Sasa kama unasema "uliwaandikia vijana wa vijiweni", katika maelezo ya kina baada ya kukuuliza na ulikuwa tayari
kusema kuna ugumu gani katika kuliweka hilo katika thread title, au hata aya ya kwanza ya ujumbe wako?

2. Bado nitaendelea kuwa na wasiwasi haya katika MTAZAMO, ...Unaposema sema "vijana wa vijiweni" ndio wanaoiunda
CHADEMA, Je wamevunja sheria gani ya Nchi katika hilo?
Wamekiuka haki zipi za kibinadamu kuwa huko?..lakini pia huoni kuwa unatengeneza tabaka fulani kwa vijana na
mtazamo wako?..wao wakueleweje?

3. Natofautiana na wewe katika TAKWIMU, unaposema kuwa ni takribani asilimia themanini(80%) ya vijana vijiweni
wanaiunda CHADEMA..unamaana gani? takribani asilimia tano(5%) ndio wanaandika kwa kina ..Takwimu hizi umezitoa
wapi? ni za lini? ulizifanyia wapi?

4. Bado naendelea kusema kwamba hata kama ilidhamiria thread hii iwe kwa hao "vijana wa vijiweni", as a great thinker
do you really think this is the BEST place where you could get them??

5. Katika aya ya tatu ya post yako(#230),umejaribu kuleta mada nyingine ndani ya hii...so, nisingependa kuijbu unless
uifungulie thread yake then tuendelee Mkuu wangu.

USHAURI:
Nadhani unakosea sana(na makosa haya yapo pia kwa viongozi na wafuasi wa CCM) kuwa endapo watakosolewa kwa NIA NZURI wao wana-conclude kuwa mtu aliyewakosoa ni MPINZANI, na hulka hii ndiyo inayofanya kuharibika kwa CCM.
Mfano mzuri ni wewe kunijumuisha na kuniita ni kati ya asilimia tano(%) ya Takwimu ZAKO, kuwa ni watu wachache wanaondika kwa umakini wa huko CHADEMA katika post #230...again, please read between the lines mkuu Zawadi Ngoda.
 
kwani darasa la saba sio watanzania?wewe ni mnafiki sijapata ona...sidhani kama ni owner wa firm za kupika uongo tu..nahisi una industry kabisa na kazi yako ndo hii...jomba mwenyewe kaisha kukana jana....

PATA HII:KWA UTAFITI WANGU NILIOUFANYA KWA MUDA WA MIEZI MIWILI..IMEBAINIKA 80%YA DEGREE HOLDER NI WAPENZI AU WANACHAMA HAI WA CHADEMA.

ANGALIZO:WATANZANIA WENYE DEGREE HAWAFIKI HATA 10% YA WATANZANIA WOTE..KWA HIYO 90% YA WAPIGA KURA INAWEZEKANA NI NON-DEGREE HOLDER
 
tatizo sa hiv vijana tunajidanganya kwamba ni wasom na hiz degree zetu tulizofundishwa asilimia kubwa na matutorial assistants na kuamua kuwatenga vijana wenzetu tunaowaita wa vijiwen, kumbuka mapinduz meng dunian yameletwa na watu wa tabaka la kati na tabaka la chini, kuhusu elimu mbona mbunge wa makambako na mwenyekit wa CCM mkoa wa iringa bwana deo sanga maaruf kwa jina la jah people ni mhitimu wa darasa la 4, weng mna elim ya kwenye vyet ila kurise issues mnakimbizwa hata na hao vijana wa darasa la 7.
 
Nimekuwa nikifuatilia kwanini upande wa kaskazini mwa nchi kuna wabunge wengi wa upinzani then hata kimaendeleo wapo mbele ukilinganisha na kusini,nikagundua kuwa wenzetu walitangulia kwenda shule pia walishajua kuwa adui yao mkubwa ni magamba
 
Sina budi kumtaja/kumuandika mtu huyu anajiita Zawadi Ngoda ila sifahamu kama ni mume/mke.Huyu mtu aliacha uzi wake humu akisema/kaandika kwenye kichwa cha ule uzi wake kuwa CHADEMA si kimbilio la wasomi!!!!so nikatafakari sana na mwisho nikasema itafahamika kama alivyoimba Ney wa Mitego.

Huyu mtu alimaanisha kimbilio la wasomi ni kule kwa wale jamaa wanaovaa nguo za kijana,hawa ni CCm Magamba na kasema CHADEMA hakuna wasomi sema kuna watu wa vijiweni au (jobbles corner) Sasa hapa/leo/juzi nikapata jibu kama mwanzoni nilivyotumia ujumbe wa bwana Ney wa Mitego kwamba Itafahamika so leo hii/juzi/jana tulimuona/kumsikiza msomi aliyekimbilia Ccm na si mwingine ni Mh Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Philip Mulugo huyu jamaa anayeitwa msomi na Zawadi Ngoda alikuwa anasoma the so called hotuba kule S/Africa katika hotuba ile kwa wale ambao hawakubahatika kuisikiza alisema Tanzania ilipata uhuru wake mwaka 11964 na imeunganishwa na visiwa vya Pemba na Zimbabwe huyu ndio msomi aliyekimbilia Ccm.

Na wakati ule alikuwa akinukuu/kusoma kupitia mijifaili yake mingi tu ambayo sifahamu aliandika mwenyewe au kaandikiwa na kama kaandikiwa hivi hajapata hata muda msomi huyu kusoma kilichoandikwa na kama hajapata muda kwa nini asisahihishe pale Zimbwabwe na kusema or sory sio Zimbwabwe ni Zanzibar huyo ndio msomi tena Naibu Waziri wa Elimu na Ufundi kama wanavyoita.
So swali langu ni kwamba hawa ndio miongoni mwa wasomi waliokimbilia Ccm???

Wako wapi kina
Ritz
zomba
Pasco
Kwa kuhitimisha mie nasema CHADEMA ni chama makini sana cha watu wote Wasomi,Wafanyakazi,Wafanyabiashara,Wasio na kazi,Wasiosoma,Wenye dini,Wasio na dini hata Matajili ,Rangi zote bila kujali huyu ni wa Yellow,Blue,Black,White nk.
 
Last edited by a moderator:
Mimi nafikiri aliyetoa mada hiii ni Nape kama si yeye basi ni Juha fulani anayefanana na yeye! Utafiti umefanya wapi? Unafikiri wanachama wa CDM ni kama wanachama wa magamba wanaojitapa kila kona? moja ya kielelezo cha uungwaji mkono wa CDM ni majimbo amboyo vyuo hivyo vipo mfano Ubungo ndipo kilipo chuo kikuu cha Dar es Salaam mbunge wake anatoka CDM, hali kadhalika Arusha mjini kuna vyuo Kibao ndipo mbunge kamanda Lema anakotoka. Mimi nafikiri wa2 wafike mahali wawe wazalendo waache kutumikishwa na mafisadi kwa sabu tu utashiba bilakujali utaacha heshima gani kwa kizazi chako. Huyu jamaa kwa utafiti wake nafanisha na tume au kamati zinazoundwa na serikali ya magamba kuchunguza ukweli ambao uko wazi. Hapo huo sio chunguzi bali ni kutafuta mazingira ya kupotosha ukweli, tufike mahala tuwe na uchungu na pesa zinazotumika pasipo sababu za msingi.

Namaliza kwa kukataa huyu jamaa hakufanya utafiti bali aliamua kutafuta hoja ya kupotosha ukweli!!!!!!!!!

Hahunaga kama CDM!!! sisiem walie tu maana wamebanwa kila idara na wataondoka kwa aibu!
 
Kelele nyingi zimepigwa eti CHADEMA inatamba vyuo vikuu na kuzoa wanachama wengi wasomi.

Tafiti tulizozifanya kwa wanachama hai wa CHADEMA zinaonyesha takwimu tofauti kabisa. Wanachama wengi wa CHADEMA ni vijana wa vijiweni wasiopenda kazi na waqkati wao mwingi huupoteza kwa kutia gumzo na kuleta hadithi za alinacha.

Kiwango cha elimu cha wanachama wengi wa CHADEMA ni kuanzia darasa la saba mpaka kidato cha nne na baadhi ya form six failure kama inavyojieleza kwa Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe. Na ndio maana CV zao zinapoanikwa hadharani kama Mh Sitta ALIVYOFANYA KWA Mh Mbowe, Mh Slaa akaanza kusema kuwa Sitta Kamdharau Mbowe. Jamani, Kukutangazia CV yako ndio dhambi.

Na kutokana na CV nyembamba za wanachama wa CHAMA hicho, ndio sababu kubwa ya chama hicho kuwa CHAMA CHA VURUGU NCHINI. Na hii inasababishwa na ueleo mdogo wa wanachama wake kutokana na elimu ndogo.

Fanya utafiti mdogo katika mji uliopo na utahakiki maneno yangu. Ukipata jibu ndio utaelewa kwanini CHADEMA HAIWEZI KUCHUKUA NCHI YETU.
kweli nimeamini CHADEMA inawapa kiwewe ccm wote watoto na wakubwa. hivi wewe kwa akili zako ule umati wa morogoro wale wote ni wazururaji? kule ARUMERU MASHARIKI ule umati wote ni watu wa kijiweni!! nimeamini akina MLUGO mko wengi.
 
Hapa nafikiri mtoa mada umekurupuka na unaonyesha kuwa na hasira kama vile umeambiwa C.C.M iondoke madarakani leo.Ukweli katika ufahamu wa kawaida tu CHADEMA inakubalika sana maeneo ya vyuoni,pia nina uhakika unaelewa kuwa inakubalika zaidi maeneo ya majiji km MWANZA,ARUSHA,MBEYA,DSM na pia miji mikuu mingi hapa Tanzania.swali langu kwako,je vyuo, majiji na miji mikuu ni sehemu ambayo wanaishi wenye elimu ndogo na wasionauelewa kama unavyojaribu kuwalaghai watu?.
Ubarikiwe na kutokuwa mkweli.
 
Hakuna msomi anaweza kuwa na muda na chama cha vihiyo. Mnyika ni form six alipata division three halafu wakati wa uchaguzi akadanganya eti ana division 1 ya point 3. Jamani, kuna mbunge wa mpanda wa chadema yeye ni darasa la saba. Jiulize hawa chadema nani amewahi kuwa angalau mkuu wa wilaya. Maprofessor woote ni ccm angalia wakina mwandosa, wangwe, mhongo, tibaijuka. Sasa chade ma ni
professor baregu peke yake. Lweitama ni chakubanga hana sifa za kitaaluma. Kitila mkumbo ni pandikizi amesomea education
Unavyosema sio fair umezungumza kama mgomvi. kama ugomvi wa mume na mke vile au sizitaki mbichi hizi! ...
 
Kelele nyingi zimepigwa eti CHADEMA inatamba vyuo vikuu na kuzoa wanachama wengi wasomi.

Tafiti tulizozifanya kwa wanachama hai wa CHADEMA zinaonyesha takwimu tofauti kabisa. Wanachama wengi wa CHADEMA ni vijana wa vijiweni wasiopenda kazi na waqkati wao mwingi huupoteza kwa kutia gumzo na kuleta hadithi za alinacha.

Kiwango cha elimu cha wanachama wengi wa CHADEMA ni kuanzia darasa la saba mpaka kidato cha nne na baadhi ya form six failure kama inavyojieleza kwa Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe. Na ndio maana CV zao zinapoanikwa hadharani kama Mh Sitta ALIVYOFANYA KWA Mh Mbowe, Mh Slaa akaanza kusema kuwa Sitta Kamdharau Mbowe. Jamani, Kukutangazia CV yako ndio dhambi.

Na kutokana na CV nyembamba za wanachama wa CHAMA hicho, ndio sababu kubwa ya chama hicho kuwa CHAMA CHA VURUGU NCHINI. Na hii inasababishwa na ueleo mdogo wa wanachama wake kutokana na elimu ndogo.

Fanya utafiti mdogo katika mji uliopo na utahakiki maneno yangu. Ukipata jibu ndio utaelewa kwanini CHADEMA HAIWEZI KUCHUKUA NCHI YETU.
Sio lazima wote tutupie thread jamvini, tuwaambie mpaka lini
 
kuna wananchi wengi wanakisapoti Chadema kwa kuwa wanaona kinafaa. hao si wa kudharau. kuna wengine wanapenda mabadiliko na wanaona Cdm kinaongoza vyama vingine, ndo maana unaona vyama vingi havina mvuto hivo havishine. Ukweli Cdm kinashine yaani kimelamba madume. sasa mtu akisema ni chama cha wahuni ana maana wtz wana kawaida ya kuwapenda wahuni? mimi naona ni aina ya wivu usio na tija
 
Back
Top Bottom