CHADEMA si kimbilio la wasomi!

CHADEMA si kimbilio la wasomi!

Akili za wanachama wa CCM zinafanana, ati kafanya utafiti wake...ha ha ha ha ha ha. inaonekana wewe hata darasa la saba ujafika.
 
Mkuu Zawadi Ngoda,

1. Hoja huioni ina mantiki machoni "mwako"..wewe ndio mleta mada(it's so obvious utaona ina umuhimu) ila sisi wachangiaji ndio inabidi utushawishi, lakini si kama kwa njia hiyo hapo juu.

2. Nilikukumbusha kama MSOMI, inabidi ulete DATA za utafiti kama ambavyo nilisema mwanzo(nani aliufanya, wapi, lini, result...THEN ndiyo comparison ya cyama vingine vile vile pamoja na utafiti wao ulinganishwe) na si kwa kusema "wewe angalia mwenyewe tu", kirahisi namna hiyo.

3. Unapoita vijana wamitaani wamebweteka nadhani unakosea TENA, as wasomi we dont generalize mkuu, "to generalise is to be an idiot" mkuu...take that from me.

4. "Hujawahi kukutana na watu fulani wanaojiira wasomi lakini mamvo ambayo anayoyafanya ukiyaona unakataa hata kama ukiona cheti chake?!".. what difference is it thete then kwa "viongozi wasomi" uliowataja?

5. A leader is not born, is made! Kuna viongozi walikuwa hawana elimu kubwa lakini waliongoza katika mageuzi, nchi mbalimbali...wasomi hawakuwepo? walifanya nini?
Kwa mfano hapa TZ, Hayati Baba wa Taifa Mwl JK Nyerere, alikuwa ni mwalimu PROFFESIONALY, je hakukuwa na wasomi zaidi yake? lakini je hakuwa kiongozi bora? wale waliokuwa "wasomi" wako wapi?.. What legacy have they left for the country? will you compare with Mwalimu's?!
Dah mkuu...... kuna chief wangu mmoja(A specialist doctor) aliwahi kuniambia hii statement nikiwa medical school baada ya kutoa jibu la "ku-generalise"(jibu la ki-jumla jumla)........ Aisee, isije ikawa ndo wewe......... niliona kama amenitusi, ila its a very valid statement
 
Na mimi utafiti nilioufanyanya wa kina kabisa kwa utaratibu wa maswali yaliyofungwa mtizamo na maswali ya wazi nimebaini kwamba wewe Zawadi Ngoda ni mwanachama hai wa CCM ambaye kwa leo ulikosa la kufanya ukaamua kuja humu JF kupoteza wakati. Utafiti wako unafanana sana na ule wa Synovet. Umejaribu kazi pale umekosa?

Kelele nyingi zimepigwa eti CHADEMA inatamba vyuo vikuu na kuzoa wanachama wengi wasomi.

Tafiti tulizozifanya kwa wanachama hai wa CHADEMA zinaonyesha takwimu tofauti kabisa. Wanachama wengi wa CHADEMA ni vijana wa vijiweni wasiopenda kazi na waqkati wao mwingi huupoteza kwa kutia gumzo na kuleta hadithi za alinacha.

Kiwango cha elimu cha wanachama wengi wa CHADEMA ni kuanzia darasa la saba mpaka kidato cha nne na baadhi ya form six failure kama inavyojieleza kwa Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe. Na ndio maana CV zao zinapoanikwa hadharani kama Mh Sitta ALIVYOFANYA KWA Mh Mbowe, Mh Slaa akaanza kusema kuwa Sitta Kamdharau Mbowe. Jamani, Kukutangazia CV yako ndio dhambi.

Na kutokana na CV nyembamba za wanachama wa CHAMA hicho, ndio sababu kubwa ya chama hicho kuwa CHAMA CHA VURUGU NCHINI. Na hii inasababishwa na ueleo mdogo wa wanachama wake kutokana na elimu ndogo.

Fanya utafiti mdogo katika mji uliopo na utahakiki maneno yangu. Ukipata jibu ndio utaelewa kwanini CHADEMA HAIWEZI KUCHUKUA NCHI YETU.
 
Nimesoma michango ya wanaJF kuhusu uanachama wa CHADEMA, na kama Muasisi wa chama na Mwenyekiti Taifa mstaafu, nataka kusema kwamba nafurahia sana jinsi chama kinavyowavutia Watanzania wote kwa ujumla wao, bila kubagua wasomi, vijana wa kijiweni, wakulima wadogo na wakubwa, wafanya biashara na wawekezaji viwandani wadogo na wakubwa etc.

Ujumbe ni kwamba kila Mtanzania mzalendo, mwenye wazo zuri la kuboresha sera ili tutatue matatizo lukuki yanayoikabili nchi yetu, anakaribishwa kuwa mwanaCDM. Naridhika binafsi kwamba kwa sasa tumeweza kujumuisha Watanzania, hasa vijana ambao kwa uongozi wao wameonyesha performance nzuri.

Ukimsikiliza Mbunge yeyote wa CDM akifafanua msimamo ama Bungeni au katika mkutano wa hadhara utaona kwamba tuko sawa: Mnyika, Tindu Lissu, Halima Mdee, Wenje, "Sugu", Msigwa, wakiongozwa na vinara vyao Zitto Kabwe, Mbowe na Slaa utakuwa na matumaini kwamba "saa ya ukombozi inakaribia". Nje ya Bunge tuna brilliant people kama Prof. Baregu, Kitila Mkumbo wanaosaidia "kupika" sera za mabadiliko ya manufaa.

Mimi ni mzee mwenye raha sana kutokana na calibre ya WaTz ambao wamejiunga na chama nilichobahatika kuasisi kuleta demokrasia na mabadiliko ya kweli.

Ubunifu wa hali ya juu unahitajika kuweza kueleza misimamo na sera zetu nchini kote. Tunavyosema "Hakuna Kulala, Mpaka Kieleweke"
 
Mmefanya utafiti..............!!!!!!!
CHADEMA HAIWEZI KUCHUKUA NCHI YENU!!!!!!!!!

Tatizo kubwa la CCM mnaamini nchi ni yenu!! Nawakumbusha, nchi hii ni yetu sote bila kujali itikadi zetu za vyama.
Otherwise, hii ni story ya kutunga iliyotungwa na mtu wa kijiweni anayeota ndoto za alinacha!!.
 
Kelele nyingi zimepigwa eti CHADEMA inatamba vyuo vikuu na kuzoa wanachama wengi wasomi.

Tafiti tulizozifanya kwa wanachama hai wa CHADEMA zinaonyesha takwimu tofauti kabisa. Wanachama wengi wa CHADEMA ni vijana wa vijiweni wasiopenda kazi na waqkati wao mwingi huupoteza kwa kutia gumzo na kuleta hadithi za alinacha.

Kiwango cha elimu cha wanachama wengi wa CHADEMA ni kuanzia darasa la saba mpaka kidato cha nne na baadhi ya form six failure kama inavyojieleza kwa Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe. Na ndio maana CV zao zinapoanikwa hadharani kama Mh Sitta ALIVYOFANYA KWA Mh Mbowe, Mh Slaa akaanza kusema kuwa Sitta Kamdharau Mbowe. Jamani, Kukutangazia CV yako ndio dhambi.

Na kutokana na CV nyembamba za wanachama wa CHAMA hicho, ndio sababu kubwa ya chama hicho kuwa CHAMA CHA VURUGU NCHINI. Na hii inasababishwa na ueleo mdogo wa wanachama wake kutokana na elimu ndogo.

Fanya utafiti mdogo katika mji uliopo na utahakiki maneno yangu. Ukipata jibu ndio utaelewa kwanini CHADEMA HAIWEZI KUCHUKUA NCHI YETU.
CUF style. Oh Tanzania!
 
Wakati mwingine si vema kuchangia kila andiko naamini andika lisilo na tija ni vema kutoa changia chochote.Tukijenga tabia ya kutochangia mada zisizo na mashiko tutawasaidia wenzetu kufikiri vizuri zaidi wakati mwingine. MI NAAMINI UKIWA BAFUNI UNAOGA KWA ZILE BAFU ZETU ZA USWAHILINI AKAPITA MWENDA WAZIMU AKACHUKUA NGUO ZAKO NA KUVAA KISHA WE UKATOKA UCHI NA KUMKIMBIZA WATAkaoSHUHUDIA TUKIO HILO WATAJUA WEWE NDO mwendawazimu.Ningeshuri tussiendelee na hii mada kozi kwani hata hao tunaowaita si wasomi bado ni Watanzania.Tunataka taifa la wasomi na waeledi na si CHAMA CHENYE WASOMI
 
Mwandika mada hii uko nyuma saana kifikra.....zaidi wewe una dharau kubwa na kuwadhalilisha maskini wasio na uwezo. Wewe kwa akili yako hao ambao hawakusoma ni kwa matakwa yao??? au ni kwa ajili ya mfumo mbovu na usio lingana wa serikali yako??? Again hao wa darasa la saba siyo watanzania?? hawana haki ya kuamini chama chochote?? Waliosoma tu ndio wana haki..una uwezo mdogo saana wa kufikiri....pole..
 
Nimesoma michango ya wanaJF kuhusu uanachama wa CHADEMA, na kama Muasisi wa chama na Mwenyekiti Taifa mstaafu, nataka kusema kwamba nafurahia sana jinsi chama kinavyowavutia Watanzania wote kwa ujumla wao, bila kubagua wasomi, vijana wa kijiweni, wakulima wadogo na wakubwa, wafanya biashara na wawekezaji viwandani wadogo na wakubwa etc.

Ujumbe ni kwamba kila Mtanzania mzalendo, mwenye wazo zuri la kuboresha sera ili tutatue matatizo lukuki yanayoikabili nchi yetu, anakaribishwa kuwa mwanaCDM. Naridhika binafsi kwamba kwa sasa tumeweza kujumuisha Watanzania, hasa vijana ambao kwa uongozi wao wameonyesha performance nzuri.

Ukimsikiliza Mbunge yeyote wa CDM akifafanua msimamo ama Bungeni au katika mkutano wa hadhara utaona kwamba tuko sawa: Mnyika, Tindu Lissu, Halima Mdee, Wenje, "Sugu", Msigwa, wakiongozwa na vinara vyao Zitto Kabwe, Mbowe na Slaa utakuwa na matumaini kwamba "saa ya ukombozi inakaribia". Nje ya Bunge tuna brilliant people kama Prof. Baregu, Kitila Mkumbo wanaosaidia "kupika" sera za mabadiliko ya manufaa.

Mimi ni mzee mwenye raha sana kutokana na calibre ya WaTz ambao wamejiunga na chama nilichobahatika kuasisi kuleta demokrasia na mabadiliko ya kweli.

Ubunifu wa hali ya juu unahitajika kuweza kueleza misimamo na sera zetu nchini kote. Tunavyosema "Hakuna Kulala, Mpaka Kieleweke"

Pengine unajiliwaza kwa kudhani kuwa CHADEMA imekumbatia wanachama wa madaraja yote TZ. Ikiwa viongozi wa juu wa CDM wamekubali kuwa Chama hiki hakifahamiki Vijijini, ni vipi unadiriki kuwakumbatia wakulima wakati huko hamfahamiki. Au ulimaana wakulima wadogpowadogo wa mijini. Any way swala hilo nawaachia wenzangu watafakari.

Wabunge wa CHADEMA hawana moja. Kumbuka mlipoamua kuondoka Bungeni, Zitto Kabwe alikuwa na lake jingine. Wabunge wengi wa CDM wanaburuzwa na majuaji 5 tu. Hawa wataloamua hakuna kupinga, ukipinga unafukuzwa na kuitwa msaliti. Kuwa na mawazo tofauti ndani ya CHADEMA ina maana kuwa wewe ni CCM. UDIKITETA ULIOJE!!

Nakuelewa kuwa mzee mwenye raha, si unakumbuka sababu kubwa iliyomfanya Mh Sitta akatae ombi lenu la kuhamia chama chenu na kupewa offa ya kugombea Urais. Mh Sitta alisema, Uongozi ndani ya CDM unatolewa kikanda. Na kanda utokayo Mheshimiwa ndio kanda yenye neema CDM..

"Hakuna kulala, mpaka kieleweke" Sentensi hii ina maana, maandamano, Fitina, Uhasama, Danganya, Susia bunge kama mlivyotikisha kiberiti bungeni baada ya uchaguzi na tukio la Arusha. Kifupi maana yake ni vita.
 
Mmefanya utafiti..............!!!!!!!
CHADEMA HAIWEZI KUCHUKUA NCHI YENU!!!!!!!!!

Tatizo kubwa la CCM mnaamini nchi ni yenu!! Nawakumbusha, nchi hii ni yetu sote bila kujali itikadi zetu za vyama.
Otherwise, hii ni story ya kutunga iliyotungwa na mtu wa kijiweni anayeota ndoto za alinacha!!.

Imetungwa kijiweni!!! Na wanachama wa CHADEMA? Kifupi nchi hii ni Yetu na wataoilinda ni wapenda amani na maendeleo.

Cha ajabu ni kuwa chama chenu mnakiita cha Maendeleo wakati hampendi maendeleo, Ajabu!!
 
Chadema haiwezi kuwa kimbilio la wasomi. Chadema ni kimbilio la criminals. Edwin mtei alifukuzwa kazi na rais wa kwanza wa jamuhuri ya muungano hayati baba wa taifa kwa kulisaliti baraza la mawaziri. Yeye alikuwa waziri wa fedha halafu akawa kigeugeu na kuanza kuwaungema huwa inawalaghai watana mkono wa zungu waliokuwa wanataka tanzania iachane na azimio la arusha. Chakushanaza leo hii chadema huwa inawalaghai wa tanzania eti kinaimba ujamaa. Lakini chadema is a conservative party kama ilivyo renamo ya mozambique, unita ya angola na vingine. Ndo siri ya urembo wa kupewa helikopta kutoka huko conservative union.

Sasa viongozi wengine wa chadema waliasi aukutofuata maadili fulani huko walikokuwa na ama kufukuzwa kazi au kuombwa kujiuzulu. Wengine hawajawahi kushika wadhifa wowote tangu wazaliwe zaidi ya kuwa wabunge.
Chadema inahatarisha uhuru na uwepo wa tanzania yetu. Bado tuna uchungu tunasali kila siku mungu atueposhe na janga la hiki chama. Kimewasaliti watanzania na kujirafikisha na vyama viwili vilivyokuwa vinaitawala tanzania. Kile cha kikristo cha ujerumani na kile cha conservative party cha uingereza. Kupitia fedha za hivi vyama chadema bila kufahamu madhara ya haya mambo imekuwa ikipeleka vijana nje ya nchi eti kufundishwa siasa. Huko wanajifunza kuchukia uhuru ewa nchi za na kuendekeza ukoloni. Nasari yule mbunge pumba wa arumeru alikwenda kwenye hayo mafunzo amerudi akihamasisha kuitenga tanzania katika majimbo, kukataa mwenge wa uhuru. Sasa sisi watanzania tutegemee kuinanganywa tanzania yetu na kugeuzwa nchi iliyokwenye makwapa ya hao wanaotumia pesa zao kuhakikisha wanaturidisha kwenye mfumo wa kikoloni
 
Sasa hao wasomi wa kiccm ccm wameifanyia nini nchi hii zaidi nya kujilimbikizia mali?
Je walioichagua ccm miaka yote ni wasomi?
Acha upambafu pambafu!!!!!!!!!!!!!!!

Nilipovaa ujasiri na kuandika Thread hii, nilifahamu wazi kuwa nitaokabiliana nao ni vijana wa vijiweni hivyo nilijiandaa kisaikolojia kuwa stable.

Tegemeo la kwanza, ilikuwa ni matusi mbalimbali kati ya 400 hadi 500. Japo sijayahesabu lakini ninahakika kuwa jumla ya matusi ni mpaka hivi sasa ni 200-250. Bado ninauwezo wa kuyakabili na kulala usingizi salama.

Endeleeni kutukana, ili tuwajue sura zenu.
 
No educated person can talo of CHADEMA UNLESS IS promised something like a trip to Germany. This is happening. Ohh njjoo tutawapeleka Ujerumani. Mie nilipokuwa chuo kikiuu walinitokea nikawakatalia. wenzetu walikwenda na wengine wameachwa solemba
 
CHADEMA imezidi. Kila siku kukimbilia Uingereza kupewa helikopta nani aliwaambia wa Tanzania ni washamba wa helikopta?? tunataka sera siyo kuungurumisha helikopta mkishashinda mnaanza kutoa pumba kama za nasari
 
ccm ndo imetufanya tuishie darasa la saba na tukae vijiweni ccm na wasomi fake na wezi na mafisadi
 
Imetungwa kijiweni!!! Na wanachama wa CHADEMA? Kifupi nchi hii ni Yetu na wataoilinda ni wapenda amani na maendeleo.

Cha ajabu ni kuwa chama chenu mnakiita cha Maendeleo wakati hampendi maendeleo, Ajabu!!

Wapenda maendeleo wote wanaiunga mkono CHADEMA. CCM haiwezi ikaleta maendeleo; ingekuwa na uwezo huo Tanzania ingekuwa na maendeleo. Kuendelea kuiunga mkono CCM ni kuimarisha umaskini unaotengenezwa na chama kilichochoka kuwatumikia wananchi CCM.
Kuhusu hoja ya CHADEMA na vijana wa vijiweni, hustahili kujibiwa; jibu unalo.
 
Dah mkuu...... kuna chief wangu mmoja(A specialist doctor) aliwahi kuniambia hii statement nikiwa medical school baada ya kutoa jibu la "ku-generalise"(jibu la ki-jumla jumla)........ Aisee, isije ikawa ndo wewe......... niliona kama amenitusi, ila its a very valid statement

Mkuu Dr. Wansegamila, am sorry to say he was right kusema vile, but am not the one though!! msamehe chief wangu, ila tuwakumbushe vijana, wasilete "cheap ideas" and above ku_generalize.
 
CHADEMA imezidi. Kila siku kukimbilia Uingereza kupewa helikopta nani aliwaambia wa Tanzania ni washamba wa helikopta?? tunataka sera siyo kuungurumisha helikopta mkishashinda mnaanza kutoa pumba kama za nasari

Mkuu Almasiomary, what is the point again here?
 
Hakuna msomi anaweza kuwa na muda na chama cha vihiyo. Mnyika ni form six alipata division three halafu wakati wa uchaguzi akadanganya eti ana division 1 ya point 3. Jamani, kuna mbunge wa mpanda wa chadema yeye ni darasa la saba. Jiulize hawa chadema nani amewahi kuwa angalau mkuu wa wilaya. Maprofessor woote ni ccm angalia wakina mwandosa, wangwe, mhongo, tibaijuka. Sasa chade ma ni
professor baregu peke yake. Lweitama ni chakubanga hana sifa za kitaaluma. Kitila mkumbo ni pandikizi amesomea education

Michango mingine munaitoa kwa lengo gani? unafahamu ni kwa nini hao unaowaita maprofesa wako ccm? unafahamu kwa nini maprofesa au tuseme watumishi wa serikali wanashindwa kuonyesha uanachama wao wa Chadema, CUF n.k.? Unafahamu kwa nini utumishi ssa wanataka kila anayeajiliwa serikalini aombe kwao?

Hebu ktk hao maprofesa niambie ni yupi huko CCM ametoa mchango wa "kiprofesa" yaani akatoa hoja ukasema kweli huyo ni profesa. Anzia hapo kwa Mwandoysa uendelee. Hawa ndo tunawasikia wakitoa shukrani kwa mabinti na vimada wao ktk bajeti ya serikali!

Kwa mtoa mada: Siyo kila mtu ana sifa ya kufanya utafiti. Ulichoandika hapa ni umbea. Umbea siyo utafiti.
 
Kelele nyingi zimepigwa eti CHADEMA inatamba vyuo vikuu na kuzoa wanachama wengi wasomi.

Tafiti tulizozifanya kwa wanachama hai wa CHADEMA zinaonyesha takwimu tofauti kabisa. Wanachama wengi wa CHADEMA ni vijana wa vijiweni wasiopenda kazi na waqkati wao mwingi huupoteza kwa kutia gumzo na kuleta hadithi za alinacha.

Kiwango cha elimu cha wanachama wengi wa CHADEMA ni kuanzia darasa la saba mpaka kidato cha nne na baadhi ya form six failure kama inavyojieleza kwa Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe. Na ndio maana CV zao zinapoanikwa hadharani kama Mh Sitta ALIVYOFANYA KWA Mh Mbowe, Mh Slaa akaanza kusema kuwa Sitta Kamdharau Mbowe. Jamani, Kukutangazia CV yako ndio dhambi.

Na kutokana na CV nyembamba za wanachama wa CHAMA hicho, ndio sababu kubwa ya chama hicho kuwa CHAMA CHA VURUGU NCHINI. Na hii inasababishwa na ueleo mdogo wa wanachama wake kutokana na elimu ndogo.

Fanya utafiti mdogo katika mji uliopo na utahakiki maneno yangu. Ukipata jibu ndio utaelewa kwanini CHADEMA HAIWEZI KUCHUKUA NCHI YETU.
Mod. Tafadhari tena. Niliwahi kutoa maoni kwamba ktk majukwaa ongeza na "JF Toto" Ni aibu kuona ktk jukwaa la siasa kuna thread kama hii. Nahisi huyu amesoma lakini ana tatizo la kutoweza kupanga hoja. Kwa ujumla ukimpa maksi zinakuwa za kuokota okota baadaye anapita.

Angalia pia michango iliyofuata kuunga mkono ni ya aina gani. Nilitaka kuunga mkono lakini nashindwa kabisa kutokana na ubora hafifu wa wale wanaounga mkono.

Mtu anaaandika haya na kuyaita ni matokeo ya utafiti! Hivi kweli hata umbea ni utafiti?

Zawadi Ngoda, elimu na ufahamu wa viongozi wa CCM ukoje? Wako kama wewe au ni zaidi?
 
Back
Top Bottom