Chadema ndani ya Bukoba

Ni kweli..ndio maana serikali makini ingekabiliana na CHADEMA kwa kuthibiti mfumuko wa bei za bidhaa, kuongeza mishahara ya wafanyakazi, kubana matumizi ya serikali ili kujenga uwezo wa serikali kuwapunguzia wananchi ugumu wa maisha n.k.Tatizo raisi huyu hana strategists; na aliowaweka wengi rafiki zake hawana uwezo na wanatumbua raha huku yeye akitetemeka kuwajibu CHADEMA.
 
attachment.php
majibu ndiyo hayo jk sikia, tafuta utatuzi wa shida za watu sio kulalama haisaidii!!!!!!!!! Watu wamepigika wamechoka wanataka majibu sahihi!!!!
 
eti wanajiamini kuwa wananchi hawawezi kuchukua hatua yoyote zaidi ya kulalamika JK sikiliza kero za wananchi na uzitafuatie ufumbuzi vingenevyo itafikia kipindi wananchi uzalendo utatushinda na kitakachofuata.........................................................
 
Dada Regia,

Hongera sana, nilikwambia wazi tulipokuwa Sengerema baada ya Sugu kumaliza kutoa hotuba huku umati ukitaka jua lisizame taarifa unazotupatia tunafurahi sana.
Tutumie picha, mimi kwa leo niko Arusha lakini kwa kweli tunafarijika sana.

Kila la Kheri kwa busara iliyotumika kutokuwaambia wananchi wasiingie barabarani kudai kura zao, naamini wamejifunza huu umati hata baada ya kutupora kwa nguvu.

Ninaye Rais wangu Moyoni ananiongoza na ninamuheshimu, Huyo mtalii(Mkwere) wenu ananitawala tu ila sina mpango naye na sikuumpa kura yangu:rain:
 
Kikwete ujue kwamba kuongea kauli tupu za mdomoni, huku wananchi wanasota waya ni sawa na kumpigia mbuzi gitari...
Hukuwa na haja ya kubwabwaja maneno ya aibu kuhusu chadema, ulitakiwa kuwa kivitendo zaidi...kusemea sukari peke yake ni kituko, maana watu wengi sasa wana'avoid sukari maana inaleta ugonjwa mbaya sana mwilini.
Usituuwe bana...tuna majukumu kulea watoto!
 
Kikosi kazi cha CDM kilichokuwa kinatalajiwa kutua Bukoba mjini leo hii majira ya saa 7 kimewasili hapa bukoba mjini majira ya saa kumi hivi. Hivi sasa kinahutubia mkutano wa hadhara katika uwanjawa kaitaba. Mahudhurio ni makubwa sana haijapata kutokea. Maandamano yalikwenda vizuri. Polisi hawakuwabugudhi hata kidogo waandamanaji.
ni kweli kabisa mkuu.hivi sasa Dr Slaa ndo anazungumza na ameelezea jinsi alivyochukuliwa kuhojiwa na polisi Kahama.Ameijibu hotuba ya Rais kwenye kipengele kilichomuhusu baba wa taifa.wwww
 
Wakuu.Habari!!!

Yale Maandamano ya CHADEMA katika Kanda ya Ziwa yanatarajiwa kuhitimishwa leo kwa maandamano makubwa na ya aina yake Bukoba Mjini. Maandamano hayo yanatarajiwa kuanza saa 7 mchana.Maandalizi yameshakamilika na msafara wa Vikosi Kazi ndio unajiandaa kutoka Kahama vilipotia nanga kuelekea Bukoba. Kazi kamili itahitimishwa kesho kwa kufanya mikutano ya hadhara kwenye Wilaya za Mkoa wa Kagera. Baada ya hapo Vikosi vitarudi Dar es salam kwa maandalizi ya Kanda nyingine baada ya Bunge la Aprili. Habari ya matukio baadaye kazi ikianza.

Kutoka Kahama
Reagia E Mtema
Waziri Kivuli- Kazi na Ajira.

Aluta continua Mheshimiwa Regia, unafaa kabisa kuwa communication expert, you update us regulary, yan ni kama tuko kwenye msafara ingawa physically tuko mbali. Msichoke dada yangu. Msisikilze la mtu chapeni kazi watz tunawategemea.
 
Aluta continua Mheshimiwa Regia, unafaa kabisa kuwa communication expert, you update us regulary, yan ni kama tuko kwenye msafara ingawa physically tuko mbali. Msichoke dada yangu. Msisikilze la mtu chapeni kazi watz tunawategemea.

sio siri huyu Mh.Regia anafaa sana kuweka katika hiyo wizara ya mambo ya mawasiliano
Regia you are rocking.
 
kaa la moto ongeza zingine Tafadhali........napenda kuangalia picha sana
 
This is a new African Democracy, whereby we are voting by FOOT!

Ballot boxes no longer effective for change
 
Je inawezekana kumtoa mtu aliyewekwa madarakani kwa wingi wa kura za wananchi na kuapishwa kisheria. Chadema lazima mtumie japo akili kidogo kujua kuwa hamtaweza kumng'oa JK mpaka miaka mitano yake imalizike. sasa msituletee balaa kwa maneno yenu ya uchochezi na kufarakanisha watu ili damu imwagike.

Sisi tunazidi kuomba amani itawale na wenye nia tofauti na hiyo Mola awaadhibu sana.

Kwani mubarak hakuapishwa we vipi wewe?
 
Je inawezekana kumtoa mtu aliyewekwa madarakani kwa wingi wa kura za wananchi na kuapishwa kisheria. Chadema lazima mtumie japo akili kidogo kujua kuwa hamtaweza kumng'oa JK mpaka miaka mitano yake imalizike. sasa msituletee balaa kwa maneno yenu ya uchochezi na kufarakanisha watu ili damu imwagike.

Sisi tunazidi kuomba amani itawale na wenye nia tofauti na hiyo Mola awaadhibu sana.

Wale wote wanaojidanganya kuwa Tanzania ni nchi ya amani poleni sana.

Angalia jinsi nyumba zinavyojengwa na kuta na mageti kama jela, pamoja na joto lote hili watu hawathubutu kuacha hata mageti wazi ili wapate upepo mzuri unaotoka nje.

Kupokea simu sehemu zingine ni balaa, kuna watu hata vibrations wanaziondoa maana vibaka wanazistukia mpaka vibrations.

Kina mama kunyang'anywa mikoba yao na hata kina baba ukiweka pesa kwenye pochi kaa chonjo.

Usiku unalala huku sikio liko nje, kusikikilia kelele za mwizi.

Gari ukiliegesha usishangae kurudi hakuna side mirrors, alama za gari kama TOYOTA, MITSUBISHI n.k. Hata gari lenyewe ukizubaa linaenda. Magari mengi yamewekewa alarm ukipita karibu tu unasikia king'ora.

Na wale majambazi waliouawa jana Morogoro wakiiba duka la sonara, kweli inaashiria amani.

Orodha ni ndefu sana wengine wanaweza kuongeza.

Naomba ninukuu usemi kwa lugha ya kiingereza,

Peace does not mean the absence of war!

Amani ni kuwa na utulivu mpaka wa kisaikolojia, kuwa na uhuru wa kutembea, kulala bila hofu, kuwaacha watoto wako waende matembezini ama ufukweni kuogelea wewe mwenyewe ukiwa umepumzika nyumbani kwako bila hofu yoyote. Kuwa na uhuru wa kuacha mlango wazi wakati wa joto na kuanika nguo zako kwenye kamba nje mwenyewe ukaingia ndani. Amani ikuwezeshe kuacha gari lako mahali ukaenda kwenye shughuli zingine ukarudi baada ya masaa matatu ukalikuta liko salama. Amani ni kumpa mtoto wako simu ya Nokia akienda shule ukamwambia ukiona nimechelewa kuja kukufuata, mpigie simu mama yako mdogo halafu umsubiri kituoni aje kukuchukua. Nawe uwe na amani kabisa kuwa itakuwa hivyo. Kama hayo hayawezekani, basi Tanzania hakuna amani. Huhitaji Chadema kuvunja amani maana haipo.
 
hili bangp linalosema kikwete we vipi?!!

yaani najaribu kujenga picha jk yuko mbele yangiu then namsukuma kidogo halafu natoa kauli hii

we vipi wewe ? we lofa nini? tatizo ni wewe na serikali na sio chadema ...we mwehu nini?!!

hahahahh....kaa la moto ongeze zingine please
 
I love to hear the word CHADEMA!

Tumaini jipya kwa watz hebu mfanye mpango wa dharura kufungua kituo chenu cha tv ili tuwe tunapata uhondo huu live, maana tv nyingi za kibongo zinaogopa kupingana na majambazi wa nchi.

Dar tunawasubiri kwa hamu maana ni wakati wa kutoa shule ili 2015 hawa majambazi wakimbie nchi wenyewe kwa vile wananchi watakavyokuwa wameelimika. Big up wnacdm wote na watz wote kwa kuiunga mkono chadema.

Aluta continua!!!!!!!!!!!!!!!11
 
sio siri huyu Mh.Regia anafaa sana kuweka katika hiyo wizara ya mambo ya mawasiliano
Regia you are rocking.

Apewe nyenzo na wataalamu awe mkuu wa kitengo cha mawasiliano cha Chadema, ametusaidia sana kupata habari za haya maandamano.
 
Je inawezekana kumtoa mtu aliyewekwa madarakani kwa wingi wa kura za wananchi na kuapishwa kisheria. Chadema lazima mtumie japo akili kidogo kujua kuwa hamtaweza kumng'oa JK mpaka miaka mitano yake imalizike. sasa msituletee balaa kwa maneno yenu ya uchochezi na kufarakanisha watu ili damu imwagike.

Sisi tunazidi kuomba amani itawale na wenye nia tofauti na hiyo Mola awaadhibu sana.

hata Mungu hapendi uonevu unaofanywa na CCM
 
Back
Top Bottom