CHADEMA msijidanganye, Dr. Slaa hayuko peke yake

CHADEMA msijidanganye, Dr. Slaa hayuko peke yake

Bahati mbaya na wewe unasema kwa niaba ya watu wengine ambao unadai wako wengi, umejuaje nafsi za watu wengine.
 
Wafuasi wake sisi wanatuhusu nini? wafuasi wake si ni Dr. Mwakyembe ndani ya serena hotel? Lipumba yupo wapi? Risasi yenu ya mwisho kuitumia ndo hiyo...bye bye bye...Lowasa kumbe ni tishio kuuu...
 
Maneno mazito haya; sasa tunajua na tumeona tofauti ya watu wanaotaka mabadiliko ya kweli na wanaotaka mabadiliko tu. Wanaotaka mabadiliko tu hawana cha kusimamia isipokuwa kitu kibadilike tu. Hawajali ni mabadiliko gani, ya nini, kwanini na kwa vipi tu. Ni kama watu wanaopigishana stori kijiweni; mtu anaweletea stori za mpirani jinsi magoli yalivyofungwa na watu wanashangilia na kurudia jinsi kona ilivyopigwa n.k kumbe aliyewasimulia alisikia redioni tu. Wanataka tuamini kuwa Lowassa anawakilisha kweli mabadiliko! Hata kusema "CHADEMA" Lowassa maskini wa Mungu anapata tabu, halafu juu yake anatakiwa awakilishe UPAWA vile vile! Ili watu wapewe!

Ndio maana toka mwanzo nilishapuuzia huu UPAWA niliamini wakati ule kuwa ni dubwasha baya zaidi lililovuruga harakati za mabadiliko na litatusumbua baadaye. Lakini sikudhania lingetokea na la Lowassa vile vile. Sasa hivi CCM wala hawana haja ya kupiga kelele tena, wanasubiri vichinjio vyao wafutilie mbali upinzani tarehe 25 liwe onyo na somo kwa wengine!

Umefika golini kabisa na umebaki wewe na kipa mtu anakuonesha kisura halafu unabutua juu; hata wakionesha replay zile unashindwa kuangalia kwani ni aibu.


Nina heshima kubwa sana juu yako Mwanakijiji kwa sababu kupitia wewe nimejifunza mengi mno. Kwa ufupi wewe ni shujaa wanhu japo hatufahamiani personally. Hata hivyo, katika siku za karibuni umekuwa na mabadiliko makubwa katika arguments zako kiasi nimepata mashaka makubwa unachohitaji hasa ni nini.

1. Umekuwa ukihubiri sana nadharia za mabadiliko kama zile za 'utopia' huku kwa ujanja mkubwa ukionekana
kudiscourage au kufifisha kila hatua ya utendaji wowote kuelekea mabadiliko hayo. Na sijajua kama unaangukia
ktk tatizo la kawaida la wasomi kuwa wamejaa nadharia tu kuliko vitendo au ni hulka yako binafsi au kuna kusudi
unalitumikia.

2. MM umekuwa mtu wa mashaka sana, too pessimistic na ni kama vile huamini au huna imani kuwa kwamba
ukombozi waweza kuwa umekaribia au umefika kabisa. Huoneshi kukubali au hata kutamani kuwa saa ya matumaini
iwe ni sasa. Unahubiri ngoja ngoja, subiri kidogo, mchakato na upembuzi uendelee. Hujali hisia za wanamadiliko wenzako wanaoona kuwa saa ya ukombozi ni sasa

3. Shujaa wangu huhamasishi tena, huwapi watu matumaini, unaonyesha wafuasi wako njia ndeeefu lkn wewe
mwenyewe huitembei hiyo njia.

Nini kimekupata shujaa?
 
Maneno mazito haya; sasa tunajua na tumeona tofauti ya watu wanaotaka mabadiliko ya kweli na wanaotaka mabadiliko tu...
Mzee, nikisoma maoni ya wengi humu. Ni dalili tosha kuwa hata zile operesheni Sangara na M4C hawakuwa wanaelewa dhima yake hasa.

upepo wa mabadiliko unavuma, na watu hawataki kujua madhara ya upepo ukibadilika
 
Tunahitaji haya ilituendelee according to Hayati Mwl. Nyerere
- Watu
- Ardhi
- Uongozi bora
- Siasa safi
 
Baada ya Dr. Slaa kung'atuka siasa za kitapeli za CHADEMA na washirika wake, tumeshuhudia manguli na viwanda vya propaganda wa CHADEMA wakitumia kila mbinu kutuaminisha kuwa kila kitu ni shwari ndani ya Chama hicho na kikundi cha UKAWA. Hoja nyingi zinazokosoa kitendo cha CHADEMA hususani UKAWA kuonyesha taswira ya kununuliwa na mgombea wake wa urais ambaye walipita nchi nzima na kutumia rasilimali nyingi ikiwemo damu na wengine kupata ulemavu kwa kumnadi ni FISADI papa pamoja na wenzake alioambatana nao. Hoja hizi hazijibiwi badala yake viwanda vya propaganda vimekuwa vikifanya CYBER BULLYING kwa yeyote anayehoji ama kukosoa.

Vinara wa uhuni huo wamekuwa wakiongea kwa kusema Dr. Slaa amechelewa na hakuna kinachobadilika na kinachoshangaza zaidi, yule waliyekuwa wanamnadi ni Rais wa mioyo ya Watanzania amepewa majina mapya ya Babu, Mzee, Kizee n.k. Pia wazungumzaji wanaotulazimisha tuwasikilize wao pekee wanajinasibu kuzungumza kwa niaba ya Watanzania wote. Hili ni kosa ambalo si muda mrefu watakuja kujutia na anguko lake si dogo.

Najua, nafahamu, natambua kuwa yeyote asomaye huu uzi anaelewa namaanisha nini lakini kwa kuwa tayari wengi wameshakula kiapo cha giza, wataporomosha matusi, kebehi na kubeza.

CHADEMA mnaodhani mmeshika mpini, tambueni kwamba Dr. Slaa hayupo peke yake. Kuna kundi kubwa la wanamageuzi wa kweli ambao wanamuunga mkono na wanajua cha kufanya ili kuondokana na upuuzi wa viongozi waroho kutaka kutumia njia za mkato kufanikisha malengo yao huku wakisigina misingi iliyofanikisha Chama kukubalika na wengi. Misingi ya kupambana na Ufisadi, ukiukwaji maadili ya uongozi na wizi wa amali za umma.

Dr. Slaa ni kioo, msimamo wake usiyoyumbishwa ni tunu pia ana mapenzi ya dhati kwa Taifa na watu wake.

Angetwambia mafisadi wangapi aliwataja pale mwembeyanga na kwa nini leo anamshikilia mmoja tu ningemwelewa.
Na kama hili la maaskofu kuhongwa alikuwa wapi kutwambia watanzania hadi ajekuliibua leo?

Yeye mwenyewe kwenye press conference amesema ukweli haugawanyiki, kwa nini kwenye upande wa mafisadi aliohubiri katika kipindi chote alichokuwa chadema leo anakuja kumkalia koooni mmoja tu?

Namheshimu Slaa ila kwa alichokisema hakiendani na ukweli anaousimamia.
 
Babu Slaa yuko na CCM waliomtuma na kumuhonga ,, Slaa amekodishiwa private jet kumpeleka Afrika Kusini akale ela alizohongwa na CCM

Asante sana laki si pesa. Umemjibu vema msaanii. Msanii umeeelewa. Dr Slaa anawaaminisha watanzania kuwa ana simamia misingi huku mkutano wake na waandishi wa habari na matangazo ya TV na redio yamegharimiwa na ccm. Anafikiri sisi watanzania wajinga. Dr. potelee mbali sana. Hatukuhitaji msaliti mkubwa wewe.
 
mkifika kwenye safari yenu ya mabadiliko.. tutakuja kujadiliana tena ..humu ndani.. kwasasa msafara unatoka serengeti kwenda mara... kama ilivyo ada...
 
dr. Slaa hajabomoa bali amejenga. Ukitaka kujua kama amejenga angalia muda aliotumia kujenga hiyo nyumba. Kwa miaka zaidi ya kumi dr slaa amekua akiijenga cdma. Kwa hiyo hawezi kuibomoa kwa dakika 10 hata kama ingekuwa ya nyasi.
 
Baada ya Dr. Slaa kung'atuka siasa za kitapeli za CHADEMA na washirika wake, tumeshuhudia manguli na viwanda vya propaganda wa CHADEMA wakitumia kila mbinu kutuaminisha kuwa kila kitu ni shwari ndani ya Chama hicho na kikundi cha UKAWA. Hoja nyingi zinazokosoa kitendo cha CHADEMA hususani UKAWA kuonyesha taswira ya kununuliwa na mgombea wake wa urais ambaye walipita nchi nzima na kutumia rasilimali nyingi ikiwemo damu na wengine kupata ulemavu kwa kumnadi ni FISADI papa pamoja na wenzake alioambatana nao. Hoja hizi hazijibiwi badala yake viwanda vya propaganda vimekuwa vikifanya CYBER BULLYING kwa yeyote anayehoji ama kukosoa.

Vinara wa uhuni huo wamekuwa wakiongea kwa kusema Dr. Slaa amechelewa na hakuna kinachobadilika na kinachoshangaza zaidi, yule waliyekuwa wanamnadi ni Rais wa mioyo ya Watanzania amepewa majina mapya ya Babu, Mzee, Kizee n.k. Pia wazungumzaji wanaotulazimisha tuwasikilize wao pekee wanajinasibu kuzungumza kwa niaba ya Watanzania wote. Hili ni kosa ambalo si muda mrefu watakuja kujutia na anguko lake si dogo.

Najua, nafahamu, natambua kuwa yeyote asomaye huu uzi anaelewa namaanisha nini lakini kwa kuwa tayari wengi wameshakula kiapo cha giza, wataporomosha matusi, kebehi na kubeza.

CHADEMA mnaodhani mmeshika mpini, tambueni kwamba Dr. Slaa hayupo peke yake. Kuna kundi kubwa la wanamageuzi wa kweli ambao wanamuunga mkono na wanajua cha kufanya ili kuondokana na upuuzi wa viongozi waroho kutaka kutumia njia za mkato kufanikisha malengo yao huku wakisigina misingi iliyofanikisha Chama kukubalika na wengi. Misingi ya kupambana na Ufisadi, ukiukwaji maadili ya uongozi na wizi wa amali za umma.

Dr. Slaa ni kioo, msimamo wake usiyoyumbishwa ni tunu pia ana mapenzi ya dhati kwa Taifa na watu wake.

Slaa bila shaka kahongwa hela ndefu sana na CCM, badala ya kupeleka maji vijijini nyie mnawahadaa wananchi,kwa nini mnatumia pesa nyingi kurudi ikulu mnalinda nini.Nimesoma magezeti napata shaka kuwa slaa anatumika na CCM ila sisi tunasema Mabadiliko ni lazima mwaka huu.

 
Watu tulisha chagua rais kabla hata hatuja jiandikisha ivii unafikiri watu walienda kulala vituoni ili wajiandikishe alafu wasikilize Sera. Watu walijiandikisha kwa lengo moja tuu kuchagua na kuitoa ccm
 
kama hayuko peke yake akaanzishe chama kama mwenzie Zito, huku Ukawa tulishamsahau na alishakosa mvuto siku mingi. Raisi wetu ni Lowasa
 
Mkuu Msanii ni kweli Dr. Slaa hayuko peke yake lakini yuko na nani leo? Wengine tulitahayari Lowasa kuwa na CHADEMA lakini nakuhakikishia tumetahayari zaidi Dr. Slaa kuwa na hao alio nao sasa. Dr. Slaa hakuwa mtu wa kutegemea aina ya watu alio nao sasa kutolea sauti yake. Naye kapoteza mwelekeo. Naye si mtu wa kufuatwa tena na watu makini.
 
Hii ni Vita

Huwezi kuimba mziki wa wana CCM eti tukuelewe

Eti watu wamebebwa na malori...Amedharaulika huko mtaani hadi basiiii .....

Na hatuwezi kukata tama katikati ya vita.....MATOKEO Ni swala linguine...BUT We are on a serious fight

Sumaye said Muda wote CCM imekuwa imejaza Mapandikizi Upinzani
 
Mvua inyeshe juwa liwake Lowassa ni RAISI kama hutaki hamia ccm uache porojo treniii inaendelea
 
Back
Top Bottom