CHADEMA msijidanganye, Dr. Slaa hayuko peke yake

CHADEMA msijidanganye, Dr. Slaa hayuko peke yake

Hizo taarabu za kusoma namba peleka chimwaga na Lumumba

Mpaka sasa ukawa wanaongoza kwa 94.5 %

Mnazunguka na wasanii kwenye kampeni

Mnafanya fiesta show nchi nzima

Hata ivyo mnawapa promote wasanii kazi zao zinaonekana ila kura ni lowasa na wabunge Wa ukawa

Hizo hesabu za kura za Ufipa?
 
Hata mimi natambua Slaa hayuko peke yake kuna nguvu kubwa ya system nyuma yake.
 
Baada ya Dr. Slaa kung'atuka siasa za kitapeli za CHADEMA na washirika wake, tumeshuhudia manguli na viwanda vya propaganda wa CHADEMA wakitumia kila mbinu kutuaminisha kuwa kila kitu ni shwari ndani ya Chama hicho na kikundi cha UKAWA. Hoja nyingi zinazokosoa kitendo cha CHADEMA hususani UKAWA kuonyesha taswira ya kununuliwa na mgombea wake wa urais ambaye walipita nchi nzima na kutumia rasilimali nyingi ikiwemo damu na wengine kupata ulemavu kwa kumnadi ni FISADI papa pamoja na wenzake alioambatana nao. Hoja hizi hazijibiwi badala yake viwanda vya propaganda vimekuwa vikifanya CYBER BULLYING kwa yeyote anayehoji ama kukosoa.

Vinara wa uhuni huo wamekuwa wakiongea kwa kusema Dr. Slaa amechelewa na hakuna kinachobadilika na kinachoshangaza zaidi, yule waliyekuwa wanamnadi ni Rais wa mioyo ya Watanzania amepewa majina mapya ya Babu, Mzee, Kizee n.k. Pia wazungumzaji wanaotulazimisha tuwasikilize wao pekee wanajinasibu kuzungumza kwa niaba ya Watanzania wote. Hili ni kosa ambalo si muda mrefu watakuja kujutia na anguko lake si dogo.

Najua, nafahamu, natambua kuwa yeyote asomaye huu uzi anaelewa namaanisha nini lakini kwa kuwa tayari wengi wameshakula kiapo cha giza, wataporomosha matusi, kebehi na kubeza.

CHADEMA mnaodhani mmeshika mpini, tambueni kwamba Dr. Slaa hayupo peke yake. Kuna kundi kubwa la wanamageuzi wa kweli ambao wanamuunga mkono na wanajua cha kufanya ili kuondokana na upuuzi wa viongozi waroho kutaka kutumia njia za mkato kufanikisha malengo yao huku wakisigina misingi iliyofanikisha Chama kukubalika na wengi. Misingi ya kupambana na Ufisadi, ukiukwaji maadili ya uongozi na wizi wa amali za umma.

Dr. Slaa ni kioo, msimamo wake usiyoyumbishwa ni tunu pia ana mapenzi ya dhati kwa Taifa na watu wake.
unajua maneno yako yanaonesha ulivyo kata tamaa kutokana na mtu mlie mtegemea angemaliza kazi kuiangamiza CHADEMA amepiga mpira nje kabisa na umekuwa wa kurusha kwahiyo mnafikiri bado kuna mtu mwingine mnaweza kumtumia!! mnaweza kumpata na akatumika lakini CHADEMA ITAZIDI KUIMARIKA ZAIDI NA ZAIDI. Jiulize pesa mlizotumia, muda na rasilimali zote mlizowekeza kwa Dr slaa ili aianmgamize CHADEMA n MLICHOPATA VINAUWIANA?? ni bora fedha hizo mngezielekeza kwenye kampeni za wagombea wenu ambao wengi hawajaanza kampeni kwa kukosa fedha halafu ninyi mnahangaika na Dr aliye expire!!
 
Hakuna tukio lisilokuwa na wafuasi wake,hata shetani alikuwa ni malaika mzuri na mtiifu wa mwenyezi Mungu.

Siku alipoasi na kutimliwa na mwenyezi Mungu aliondoka na kundi kuubwa la wafuasi wake na ndio hawa wanaotutesa hapa dunia.

Pamoja na shetani kuondoka na kundi lake kubwa,Mungu aliendelea kuwa Mungu yuleyule,mwenye weledi uleule,huku kundi kuubwa la malaika wakiendelea kumzingira na kumsudia kwa kusema kuwa wewe ni Bwana.

Na hakuna kilichoharibika kinyume na matarajio ya shetani pamoja na wafuasi wake.

Kwa hiyo hakuna jambo geni unaloweza ukalifanya ukiamini kuwa wewe ndiye wa kwanza kumbe hilo jambo lilishafanyika kabla yako.

andiko hili linasomeka vizuri sana...
 
Tunajua yuko na Josephine na MaCCM... na octoba tutawafunza adabu CCM na washirika wao wote
 
Lowasaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaawaaaaaaaaaaaaasaaa<>Mabadilikooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooo
 
Hao unaosema ni wengi na wapo na Dr Slaa ni sisiem.
Hatubadiliki wajameni, Rais ni Lowassa tu.
Kamuulize Nchimbi alivyopata shida kumnadi Magufuli uwanja wa Maji Maji...
Rais wetu ni...Lowassaaaaaa...
 
Enyi wafwata upepo kesho mtakosa muelekeo.. Lowasa hawezi leta mageuzi,kama vilaza wengi mnavyoamini.
 
Mtoa mada endelea kupambana mradi maisha yanasonga mbele. sisi tushajua propaganda na ghiliba dhidi ya CHADEMA; tayari tumeshaamua kufanya mabadiliko makubwa ya chama na mfumo Oktoba itatoa majibu sahihi goli la mkono lisipofanya kazi yake. Mlofanya siasa kazi/ajira msihofu tutazalisha ajira za kutosha kwa ajili yenu na watanzania wote kwa ujumla.
 
Akimbie chadema ndio akimbilie ccm?? Kama sio unafiki ni nin.. Mimi nampenda hata yeye ndio inspirational factor kwangu.. Ila nimempuuza.. Ni Sawa na kuandaaa pilau la nyama Safi afu ufike wakat wakula ulitie mchanga na mafuta ya taa.. PILAU HALILIKI TENA JUHUD ZOTE ZA AWALI ZINAGEUKA KUWA UCHAFU.. NA UNAMWAGA CHOONI AMA JALALANI
 
Back
Top Bottom