Geita kuna Mengi ya kutujuza zaidi ya huyu Mpayukaji anayelilia Tonga hasa baada ya kujitia kitanzi cha madeni akidhani atasubiriwa mpaka auze twiga wote.Tupe taarifa za wale wakimbizi wa pale mahakama ya mwanzo Nyankumbu na maendeleo yao kisha tuambie nini kinaendelea na wale wadau wa Magwangala kule nyuma ya mgodo upite na Hospitali ya wilaya juu ya wizi wa vifaa vya gharama na matumizi mabaya ya ruzuku wanayopewa na Mgodi na usisahau kupita kwa Mkurugenzi wa wilaya juu ya kashfa za ngono katika ofisi ya elimu ya wilaya na matumizi mabaya ya madaraka ya Baraza la madiwani.Ukitoka huko Msalimie Vicky Kamata Mbunge wa viti maalum ambaye hajui hata Geita inafananaje.
nenda adc sisi chadema atukutaki
Katika hali isiyo ya kawaida waziri huyu aliyetemwa ambae anaonekana kama kondoo wa kuchinjwa kinyuma na walipigwa chini wengine ameonekana akiwa anasononeka sana na kuvuliwa kwake kwa uuzaji wa TWIGA na Wanyamapori ambao yeye anakiri akipata muda atasema wale wanyama walikuwa wa nani liwalo na liwe, Akiendelea kukinyamba chama chake kwa kutanabaisha kuwa safari imefika kikomo na sikio la kufa halisikii dawa.....akiwa kama abiria ndani ya basi ajualo linaenda kupinduka sasa Maige kufanya uamuzi wa busara kuamua kushuka kwenye basi hilo......ntawajuza lini na wapi ngojea niendelee kupelemba habari hizi kwakina baadae ni dadavue humuhumu jamvini.....JF reporter Geita
Hatupokei wezi, anajua kwa vile 2015 tunahamia magogoni ndiyo ahamie? kama yeye si fisadi alishindwa nini kuwazuia au kufichua anayehujumu rasilimali za nchi kwa manufaa binafsi? Kuitaka CDM ni tamaa zake za madaraka? He is just a dreamer hatakiwi huku.