CHADEMA kuzoa wasanii mastaa kugombea ubunge 2015

CHADEMA kuzoa wasanii mastaa kugombea ubunge 2015

Kwa Lady Jaydee hapo sidhani kama itawezekana maana nimjuavyo mume wake najua atamshauri vizuri. Naona CHADEMA walivutika sana ule wimbo wa TEJAAA. walidhani kuwa alikuwa anamaanisha teja wa unga kumbe ni teja wa mapenzi
 
Habari yenyewe ni udaku mtupu!
Majibu ya JB yamemaliza kila kitu.....HAKUNA HAJA YA KUJADILI HII KITU
Habari leo waje na nyingine hii imekosa mashiko kabisa!
 
7345193192_19bc26b004_o.jpg
00100efe_medium.jpeg

Arnold
Alois Schwarzenegger Governor of California

Yaani wewe ni mburula sana. kwani mtu akiwa beach anavaa mavazi gani? Huyo Afande Sele yupo jukwaani. ni aibu kwa chadema
 


TAARIFA KWA WANA CHADEMA MOROGORO.

Gazeti la Habari Leo la siku ya leo tarehe 2 Septemba lenye kichwa cha habari "Chadema kuzoa wasanii mastaa" pamoja na mambo mengine, mwandishi amemnukuu mmoja wa wasanii toka mkoa wa Morogoro akisema amewahi kuombwa na viongozi wa mkoa wa CHADEMA kugombea Ubunge.

NAOMBA KUWEKA KUMBUKUMBU SAHIHI.
1. Mimi ndiye mwenyekiti wa CHADEMA mkoa wa Morogoro, ninayeongoza Baraza la Uongoz la mkoa lenye wajumbe wa5 tu tangu mwaka 2009.
2. Katika vikao vyetu vyote hukujawahi kuwepo kwa AGENDA ya kumuomba/ kumshawishi mtu yeyote kugombea nafasi yoyote.
3. Hatujawahi kumuomba Afande Sele kugombea. Mbali na hilo hatujawahi hata kumuomba tu kujiunga na CHADEMA.
4. Kwa upande wa gazeti la Habari leo, naungana na kauli ya JB kwamba, kuna dalili za wazi kwamba habari hii imepikwa na mwandishi mwenyewe.

Asanteni Makamanda.
PUUZENI TAARIFA HII2 hours ago
 
Wamo,
Judith Wambura (Lady Jay Dee) anaandaliwa jimbo moja Musoma,
Selemani Msindi (Afande Sele) anaandaliwa jimbo la Morogoro Mjini
Fredy Maliki (Mkoloni) anaandaliwa jimbo moja mkoani Tanga.
Jacob Steven (JB) anaandaliwa jimbo moja la jijini Dar es salaam.

Inasemekani ni kutokana na ushawishi wa wabunge vijana Halima Mdee, Zitto Kabwe, Joseph Mbilinyi na John Mnyika.

Chanzo Habari Leo.

CHADEMA haiwezi kumuandalia mtu jimbo....
Mtu mwenyewe ndo hujiandaa kwa ajili ya jimbo!
Japokuwa wasanii kugombea ni haki yao kama watanzania,...
Tuache kuwasemea......!
 
Yaani wewe ni mburula sana. kwani mtu akiwa beach anavaa mavazi gani? Huyo Afande Sele yupo jukwaani. ni aibu kwa chadema

Vipi kuhusu DIAMOND PLATINUM anayecheza suruali ikiwa kata K mbele ya Mzee Sitta, Waziri Kombani na Mchungaji Rwakatare???!
 
CHADEMA haiwezi kumuandalia mtu jimbo....
Mtu mwenyewe ndo hujiandaa kwa ajili ya jimbo!
Japokuwa wasanii kugombea ni haki yao kama watanzania,...
Tuache kuwasemea......!

Kama mtu anaandaliwa na kulazimishwa kugombea urais kama ilivyotokea kwa Dr Slaa 2010 na 2015, itashindikana kwa nafasi za ubunge? acheni cheap politics hapa. hapa kuna ma great thinkers na si wote wana akili za bavicha
 
TAARIFA KWA WANA CHADEMA MOROGORO.

Gazeti la Habari Leo la siku ya leo tarehe 2 Septemba lenye kichwa cha habari "Chadema kuzoa wasanii mastaa" pamoja na mambo mengine, mwandishi amemnukuu mmoja wa wasanii toka mkoa wa Morogoro akisema amewahi kuombwa na viongozi wa mkoa wa CHADEMA kugombea Ubunge.

NAOMBA KUWEKA KUMBUKUMBU SAHIHI.
1. Mimi ndiye mwenyekiti wa CHADEMA mkoa wa Morogoro, ninayeongoza Baraza la Uongoz la mkoa lenye wajumbe wa5 tu tangu mwaka 2009.
2. Katika vikao vyetu vyote hukujawahi kuwepo kwa AGENDA ya kumuomba/ kumshawishi mtu yeyote kugombea nafasi yoyote.
3. Hatujawahi kumuomba Afande Sele kugombea. Mbali na hilo hatujawahi hata kumuomba tu kujiunga na CHADEMA.
4. Kwa upande wa gazeti la Habari leo, naungana na kauli ya JB kwamba, kuna dalili za wazi kwamba habari hii imepikwa na mwandishi mwenyewe.

Asanteni Makamanda.
PUUZENI TAARIFA HII2 hours ago

CHADEMA wanaweweseka sana. SUGU mwenyewe amekiri kuwa anafanya jitihada za kuwashawishi wasanii kujiunga CHADEMA. sasa mbona wanaanza kufarakana? au ndo tayari vita ya kugombea majimbo imeanza
 
Hiyo ndio taarifa Rasmi za Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Morogoro
Mkuu pamoja na taarifa rasmi na fupi ya ufasaha wa kiwango cha juu bado kuna watu wamekomalia habari hiyo ya gazeti la kijinga Habari leo. Mpu.uzi siku zote sio yule aliyeianzisha habari ya uongo ila ni yule anayejua kuwa ni uongo naye akakazania kuwa ni kweli. Washabiki wa CCM wanatia kinyaa wakati mwingine,hata kama ni kuendesha propaganda bado wanatakiwa waendeshe propaganda zenye akili na mashiko sio kugagamala na ujinga kama huu.
Chadema ni chama makini siku zote, sisemi kuwa hao hawafai ila habari hiyo ya kuwashawishi haipo hivyo ni ujinga kuijadili. Labda kama walishawishiwa na HABARI LEO.
 
CHADEMA wanaweweseka sana. SUGU mwenyewe amekiri kuwa anafanya jitihada za kuwashawishi wasanii kujiunga CHADEMA. sasa mbona wanaanza kufarakana? au ndo tayari vita ya kugombea majimbo imeanza
Ficha upumbavu wako....
 
Hata kama wana nia hiyo itabidi waangalie na ntu wa kumweka co dizain ya watu kilevi kama hao
 
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimeendelea kuwavuta wasanii kujiunga na chama hicho, ambapo sasa wasanii wanne wa muziki wa kizazi kipya, maarufu Bongofleva na filamu, wanatarajiwa kutangazwa kuhamia chama hicho wiki hii.

Afande Sele alikana kujiunga na chama hicho na kusemao …tena hata vijana wengi na baadhi ya wazee wamenitaka nigombee ubunge kwa kupitia CHADEMA lakini nimekataa. “Pia Sugu ni mshikaji wangu na anapokuja Morogoro, vijiwe vyake ndio vyangu naye vijana wameshamfuata wakimwambia anishawishi nigombee ubunge kupitia CHADEMA, amekuwa akiniambia vijana wananitaka lakini mimi sitaki, sijawahi kujiunga na chama chochote na naona mbunge wa sasa (Abdulaziz Aboud) anafanya kazi nzuri.

Vilevile amekanusha kushawishiwa na viongozi wa kitaifa wa CHADEMA au wabunge, ingawa amekiri kuna wabunge wa chama hicho kuwa ni marafiki zake wakiwemo Mbilinyi na Zitto. Kwa upande wa Jaydee alisema hafuati itikadi ya chama chochote cha siasa na hapendi siasa kutokana na imani kuwa siasa ni uongo na yeye hapendi uongo. Alisema hana nia ya kujiunga na chama chochote cha siasa wala kugombea ubunge kupitia chama chochote.


JB alikana na kusema; “mimi na siasa ni vitu tofauti, sijawahi kufuatwa na mtu wa CHADEMA na angalau kungekuwa na dalili basi uniulize, hiyo ni taarifa ya kutengenezwa na wewe ndiye uliyetengeneza hakuna aliyekupa ni udaku huo.”


Kwa upande wa Mkoloni, alisema hajawahi kufuatwa wala kushawishiwa kujiunga na chama chochote, isipokuwa ni mwanachama wa muda mrefu wa CHADEMA na amekuwa akishiriki kampeni, mikutano ya hadhara na matukio yote ya uhamasishaji ndani ya chama hicho. . “Sijawahi kuombwa nigombee jimbo, na kuhusu nia ya kugombea, ni mapema mno kuzungumzia suala hilo sasa na hata kanuni za chama...

Source:HabariLeo

GREEN: Lengo la mleta habari ni kumpigia debe mbunge wa sasa wa MOROGORO mjini ambaye ndiye mlipa mpiga zumari!
RED+BLUE: Maelezo ya majibu kwa mwandishi ambayo hakujishughulisha kuyapitia...Wakati kichwa cha habari kikisema CHADEMA yazidi kuwashawishi wasanii, mahojiano ya mwandishi na wasanii yanaonesha kuwa wengi wao waekataa!
Lakini kwa sababu mwandishi alishalipwa ujira alisonga mbele na kubembeleza kafiri..!
 
Hawa na elimu kama wanashindwa hata kujua haki zao za msingi unataka leo aje kuwa mbunge hii nchi inapotea mvuta bangi huyo ataweza kweli kujenga hoja kwenye bunge letu shule zenyewe darasa la 5 chadema kweli chama kinacho poteza muelekeo kama wabunge wenu ndio hawa wasanii hamtopata kura zetu
 
Back
Top Bottom