Chadema kumfikisha mahakamani Nape Nnauye

kuropoka ropoka hivyo huku kunamponza nape...peleka mahakamani
 
WILSON MUKAMA aunganishwe na NAPE NNAUYE kwenye kesi hii ili naye akathibitishe Uingizwaji MAKOMANDOO na CHADEMA toka nje ya nchi 2011. Wote hawa wakishindwa Wahukumiwe KUNYONGWA na JK asaini hukumu hizo ili adhabu zitekelezwe mapema kabla ya 2015.
 
kiongozi nimekupa like tayari, ila mdogo wetu Nape atakapomaliza kuyasoma hayo uliyoandika, pale juu mashaka yatalindima akilini mwake, ni bahati mbaya huyu bwana hajiulizi maswali, yuko wapi TAMBWE? yuko wapi makamba? yuko wapi mangula? wapiga kelele wote out, tazama wanaofaidi ni walewale, Picha ndiyo inaanza.... watazamaji kaeni kimya


Mkuu Isaya

Ni mungu ametujalia watanzania upole, unyenyekevu na hofu ya mungu. Kwa kashifa za selikali ya mapinduzi nachelea kusema ingelikuwa inchi za wenzetu naamini kabisa watanzania wangepambana kuzidai haki zao. Haiingii akilini pale majambazi ya mali zetu yanapoendelea kula maisha kwa raha mustarehe ndugu, jamma na marafiki zetu wakiteseka kwa hali ngumu ya maisha tena ngumu kwelikweli.

Wanatokea watu wa aina ya Nape kukitetea chama kama hicho, ni aibu kubwa tena kubwa kujifanya kipofu kutoona unyanyapaa wa watanzania kwa kuiba na kushindwa kusimamia mali za watanzania kwa faida yetu sote.

Kama maisha yetu yangelikuwa bora unadhani nani angepiga kelele ya udini au hawa wanapendelewa na wale wanabaguliwa. Ni umasikini unatusumbua kiasi kwamba tunabaguana. Jf kwa sasa mchana, usiku wimbo ni dini yetu... dini yao ...Njaa mkuu mtu alieshiba vizuri, akapata elimu nzuri, akajifahamu na kufahamu ubaya wa ubaguzi hawezi kupiga kelele za ubaguzi kwasababu hana sabab na anasababu kwa sababu maisha yake ni bora.

Ni jukumu letu watanzia kupambana na wapumbavu wanaotugawa kwa misingi ya dini, ukanda na ukabila. Wenye fedha zao watatukimbia vurugu zikianza. Na huko kwa mungu hataenda shekhe wala padri wote na sisi mamuma tukiuwana tu haponi mtu kama kweli motoni kupo tutaangamia nakuchome milele.

Nape atulie, aache mageuzi yachukuwe mkondo wake. Nawaasa pia waislamu na wakristu tusitukanane wala kubaguana mbaya wetu ni ccm na serikali yake. Kama CDM haipandi jiunge Cuf au NCCR tukimzuunguuka adui kwa pamoja tutashinda, cdm wakipiga mbeya cuf wanapiga tanga, nccr wanapiga Tabora mwishowe kunakucha tunapata taifa la serikali yenye wabunge mchanganyiko na kuondoa upumbavu na uchafu wa kupitisha hoja mufilisi bungeni kwa kigezo cha uwingi wa wabunge wa ccm.

Mkuu niishie hapa nachukizwa sana nahawa ccm wanavotugawa na kutuchochea japokuwa mimi nasimama upande wa cdm- I should declear my side of interest.

Inshallah tutashinda Wengine wapambane upande wa cdm, wengine wapambane upande wa cuf na wangine nccr lazima kitaeleweka 2015 na nape atasimama kambi ya upinzani one day .
 
Hawathubutu,tusubiri kuwafikisha kwenye mkono wa sheria maana wao wako madarakani na mfumo wetu jinsi ulivyo,tunashindwa kuwawajibisha kama inavyotakiwa.Ndo maana unaona kesi za mahakamani zinamalizwa kisiasa,na ndiyo maana rais wa nchi anathubutu kuja na kusema hakukuwepo na rushwa kwenye issue ya radar.Ndo maana hata aliyekuwa mwanasheria mkuu alisema pesa za rushwa I million dollars ni vijisenti kama ukilinganisha na zile ambazo wenzake wanazo.Na huo ndo ukweli kwasababu keshasafishwa na mkuu wa nchi,pengine mkuu huyo akiogopa asije mwaga mboga.Ufisadi unalindwa na ofisi ya juu kabisa nchini.Hayo mengine yote ni mazingaombwe tu,hakuna aliyewajibika na hakuna atakayewajibishwa kama wataendelea kuwepo madarakani.


Kweli mkuu.

- Ndo sababu Nape anazunguuka sana kukitakasa chama

-Sijajuwa mpaka sasa zambia, Rwanda, Burundi, Kenya, Uganda ni sample tu kama vyama vilivyo pigania uhuru nakuupata bado viko madarakani - Kwa nini? mi sijui na ukiona mwenzio ananyolewa wee mwagia maji kichwa chako ujuwe kinafuatia

-Kule misri, saudi arabia hata iliyo kuwa ussr inatupa historia nzuri sana ya kwamba ccm watabakia wakitawala mpaka siku ya kiama kwa maono yako. Mim nimetia miwani ya mbao naona break even point inapita, point of distortion wameikamilisha wenyewe ccm kwa kutuingizia sum ya kubaguana kilicho baki ni breaking poin only.

-Hata kule walikoanzisha utawala wa vyama vingi hakuna anayedumu, siamini huyu ccm na matatizo yote haya atadumu vipi.


Ukiona wazee wanalalamika ujuwe hali si shwali, na unapokuwa madarakani we iba unavoweza, lakini wee siku ukishushwa ni kama gbagbo, charles teror, nk Kwani unadhan hata wakoloni wako uk walipenda kuondoka ah haya bwana.

Cdm wametangaza nia ya kumshitaki Nape rasmi, sasa tunasubili na wao ccm watangaze nia na kuitekeleza, kama sisi huku wapinzani hatujawagawana wanachama wa ccm kwa, hasira watakihama chama wakisikia, wakatajwa majina na kuambiwa shida mnazopata ni kwasabab ya hawa jamma na kufahamu hayo mapesa yalivoibiwa na kufichwa huko wakati tunaambiwa serikali haina fedha.

cdm, nccr na cuf wanangoja kwa hamu kugawana wanachama hata kama kesi mtajishindia lakin mioyo ya watanzania itakuwa imeujuwa ukweli na kufanya maamuzi sahihi.
 
Marafiki zetu wakubwa ni chama cha david cameroon wa uingereza.[/QUOTE

Naona umetoroka mzee kwenye mgomo wa sensa. Kukosa shule ni jambo baya sana. Ungepata japo shule ya form two kamwe usingekuwa unatoka povu hapa kuandika uozo.
 
hivi ile statement ya Mnyika kuwa ukimkimbiza kichaa anayekimbia na nguo zako hapa haiwezi ikatumika?
mpaka sasa simuelewi elewi Nape, hayupo kwenye lile group kweli?
 
Mkishindwaga Kesi hamkawii kusema Mahakama zina Shinikizwa na Hazipo Huru!Mkishinda hamsemi zipo kama zipo Huru!Mkweche siamini watu watu vyama vya siasa!Vyama vingi visivyo na Ukomo ni JANGA ktk nchi!Nchi imedumaa kwa ajili ya SIASA badala ya watu kuchapa Kazi na Kutumia fursa zilizopo!Wanasiasa wote Lao moja,kushibisha matumbo yao na kupumbaza wananchi ili kuwanyonya kiulaini!Mkweche Hana Chama!
 
Chadema bana kila siku wanalalamika hakuna haki mahakamani na amna imani na mahakimu na majaji sasa huyo Nape mtampeleka mahakama gani...

Atapelekwa mahakama hizo hizo na haki itateneka. Ila liwalo na liwe UJUMBE UMEFIKA
 
Vizuri sana hili ajue cha kuongea na waandishi wa habari
 
Kumbe mkuki ni kwa nguruwe tu ee?mbona mnyika na chadema wote kila siku wanazusha,wanaongea uongo,wanawapotosha wananchi au ndio ile nyani haoni kundule?


Wao wanaongea na ushahidi mkononi ndio maana dr juzi kaweka wazi hatoi ushahidi polisi tena kwani amesha choka atapeleka mahakamani awaangalie nao Kama nape Ana ushahidi hataomba msamaha Kama Hana basi ataomba tumsubirie mnyika ndani ya siku Saba...kuna umuhimu wa kuwekana wazi zaidi yatakayojiri katika hili Mh. Mnyika
 
Kumbe mkuki ni kwa nguruwe tu ee?mbona mnyika na chadema wote kila siku wanazusha,wanaongea uongo,wanawapotosha wananchi au ndio ile nyani haoni kundule?

Ningepata bahati ningeshauri CDM waachane na mambo haya.kama kasema uwongo au kweli hatua ya kwenda mahakamani itamuinua Nape na CCM yake.hii ni siasa tu hapa CCM wanawatafuta tu CDM waingie mkenge,ingekua wakati wa kampeni ingesaidia lakini hizi ni porojo hata CDM wanazo kama vile tukisema CCM wanaingiza silaha n.k
 
majaji siku hizi hawaeleweki eleweki jamaa anaweza kujikuta ana hali ngumu mno - ngoja tusubiri bosi wake mkama atasemaje kesho.

bado anafikiri hii nchi ni mali ya ccm na vyombo vyote vya dola na mihilili yote iko chini yake.
 
Kumbe mkuki ni kwa nguruwe tu ee?mbona mnyika na chadema wote kila siku wanazusha,wanaongea uongo,wanawapotosha wananchi au ndio ile nyani haoni kundule?

Kama ni uongo kuna hatua za kuchukua kuwawajibisha, kama hii ambayo CDM wanachukua dhidi ya NAPE. Nani amekuwa na jeuri ya kuwachukulia hatua? kwa nini hawachukui hatua? Fikiri!
 
Ningepata bahati ningeshauri CDM waachane na mambo haya.kama kasema uwongo au kweli hatua ya kwenda mahakamani itamuinua Nape na CCM yake.hii ni siasa tu hapa CCM wanawatafuta tu CDM waingie mkenge,ingekua wakati wa kampeni ingesaidia lakini hizi ni porojo hata CDM wanazo kama vile tukisema CCM wanaingiza silaha n.k


Acha tu wachukue hatua. Kwenye ukweli uongo hujitenga.
 
Ningepata bahati ningeshauri CDM waachane na mambo haya.kama kasema uwongo au kweli hatua ya kwenda mahakamani itamuinua Nape na CCM yake.hii ni siasa tu hapa CCM wanawatafuta tu CDM waingie mkenge,ingekua wakati wa kampeni ingesaidia lakini hizi ni porojo hata CDM wanazo kama vile tukisema CCM wanaingiza silaha n.k
Chama cha Siasa kupokea pesa chafu toka nje ya nchi -- unaita hi ni propaganda tu, hujui ina madhara makubwa kwa umma? nani atakipa chama ambacho kinapokea pesa toka nje ili wapate madaraka? kwa hili CDM move on kijana lazima atoe ushahidi - matamshi kama haya ni hatari kwa taifa na chama kuwa ujumla.
 
acha matusi basi mkuu,muwe wavumilivu na kujirekebisha mnapokosolewa.kwanini mlienda kuua kijana wa watu kule iramba.mungu hapendi mwambieni kitila na mnyika watubu kwa baba askofu hiyo dhambi ni kubwa sana


Kwa nini wanaogopa kuchukua hatua za kisheria?

"Ukweli utawaweka huru" Yohane 8:32
 
Back
Top Bottom