CHADEMA kina wanachama wangapi?

CHADEMA kina wanachama wangapi?

WanaJF,

Kwa masikitiko makubwa sana nieleze tu kuwa, CHADEMA kimezidi kupoteza wanachama wake wengi hivi karibuni hali inayopelekea ku kufanya chama hicho kupoteza sifa ya kuwa chama kikuu cha upinzani nchini.

Kwa mujibu wa viwango vya kimataifa kwenye masuala ya kisiasa, chama kikuu cha upinzani ni kile ambacho kina wanachama walau nusu ya idadi ya wanachama wa chama tawala!.

Takwimu ya idadi ya wanachama kwa mujibu wa ripoti:

...CCM hadi kufikia March 20 ilikuwa na wanachama 7,892,453.

...CHADEMA hadi kufikia March 20 ilikuwa na wanachama 456,227.

...ACT hadi kufikia March 20 ilikuwa na wanachama 124,567. Baada Zitto kuingia ACT, wanachama waliongezeka hadi kufikia 259,548 sawa na ongezeko la asilimia 100.

...Idadi ya wanachama wote wa CUF, TLP, NCCR na UDP ni sawa na idadi ya wanachama wa CHADEMA.

...Kwa mujibu wa viwango vya kimataifa, CHADEMA kwa sasa ni chama kilichounda kambi ya upinzani bungeni. Lakini hakina sifa ya kuitwa chama kikuu cha upinzani nchini.[/QU

Hammida Dada a.k.a (HAMMY D) mbona unaweweseka dada tulia dawa ikuingie.
 
Hadi mwaka 2010 Chama cha Mapinduzi kilikuwa na wanachama takribani milioni tano kwa mujibu wa alkiyejuwa katibu mkuu wakati ule Bw Yusuph Makamba. Idadi hii ni ongezeko kutoka wanachama milioni tatu hivi waliokuwepo mwaka 2000. Ili kuweza kuelewa mwelekeo wa chama kikuu cha upinzani nchini na hasa kukubalika kwa ajenda yake ni vizuri kujiuliza CDM sasa hivi sasa wanachama wangapi wente kuveba kadi? Na wanachama hawa wametawanyika vipi katika nchi yetu?

Idadi ya wanachama wa chama cha siasa (siyo mashabiki) inaweza kujulikana to almost exact figures.

a. Mwanachama anapojiunga analipia kadi kwenye tawi lake
b. Kila tawi lina orodha ya wanacham wake
c. Mwanachama akihama tawi kuna utaratibu kuwa kule anakoenda atajiunga na tawi jipya na rekodi zitaonesha hivyo
d. Kila tawi linatuma idadi ya wanachama wake makao makuu
e. Kuna utaratibu wa kuupdate idadi ya wanachama (wanaoingia na kutoka)
f. Kwa kuangalia idadi hizo unaweza kuona movement ya wanachama na kupata demographia ya wanachama wako (vijana, wazee, kina mama, mijini, vijijini n.k).
g. Kulipa ada za kila mwezi za chama. Mfumo mbaya ni kulipa kwa mwaka! Ni vizuri kuweka quarterly fees ili kila baada ya miezi mitatu walio wanachama (loyal party members) wanaenda kulipa ada zao. Hii inakupa mwanga.
h. censored.

Sasa kujua hili la wanachama ni kuijua base yako. Huwezi kujenga chama kwa kutegemea independents au undecided voters. Ni kwa kutegemea your core supporters ndio chama kinaweza kusimama.
Kutokana na mfumo wa RUSHWA, wanachama wa CCM huwa wanaongezeka kipindi cha uchaguzi wa ndani, kumpata mgombea ubunge na udiwani,

Kadi huwa zinagawiwa, sio tu bure na hela juu, unapewa kadi na msimbazi wawili au mmoja kulingana na ulivyo ili umpigie kura kwenye kura za maoni

niliwahi kuwa katibu wa UVCCM tawi, na hili ni tatizo lililo nifanya nitoke CCM, baada ya kutokubaliana na huo mfumo
 
CHADEMA kinaonekana kuwa chama kisichojali sana kuwa na wanachama wengi bali wafia chama. Niliongea na mtu wangu pale CDM ili tufungue tawi nikaomba anisaidie kupata kadi kama hamsini hivi mana nilishaoganise wapenzi tufungue tawi. jamaa aliniambia jambo la maana sana alisema falsaa ya chama ni kuwa na wanachama wafia chama na si kuuza mikadi ama kuwa na wanachama kwa kusikiliza hotuba mkutano mmoja. CHADEMA inatamani zaidi kuwa na wafia chama. Sasa unaweza jijibu mwenyewe CCM , ACT na CHADEMA nani mwenye wafia chama wengi? Je humu jf ,face book nani ana wafia chama wengi ? wale wasiotaka chama chao kiguswe hata na jambo la kweli wapo kupigania tu hao ndio washindi na ni vigumu kuwajenga
 
WanaJF,

Kwa masikitiko makubwa sana nieleze tu kuwa, CHADEMA kimezidi kupoteza wanachama wake wengi hivi karibuni hali inayopelekea ku kufanya chama hicho kupoteza sifa ya kuwa chama kikuu cha upinzani nchini.

Kwa mujibu wa viwango vya kimataifa kwenye masuala ya kisiasa, chama kikuu cha upinzani ni kile ambacho kina wanachama walau nusu ya idadi ya wanachama wa chama tawala!.

Takwimu ya idadi ya wanachama kwa mujibu wa ripoti:

...CCM hadi kufikia March 20 ilikuwa na wanachama 7,892,453.

...CHADEMA hadi kufikia March 20 ilikuwa na wanachama 456,227.

...ACT hadi kufikia March 20 ilikuwa na wanachama 124,567. Baada Zitto kuingia ACT, wanachama waliongezeka hadi kufikia 259,548 sawa na ongezeko la asilimia 100.

...Idadi ya wanachama wote wa CUF, TLP, NCCR na UDP ni sawa na idadi ya wanachama wa CHADEMA.

...Kwa mujibu wa viwango vya kimataifa, CHADEMA kwa sasa ni chama kilichounda kambi ya upinzani bungeni. Lakini hakina sifa ya kuitwa chama kikuu cha upinzani nchini.[/QU

Hammida Dada a.k.a (HAMMY D) mbona unaweweseka dada tulia dawa ikuingie.
Sijui umesoma shule gani na umekula maharage gani mkuu
 
Kwa Takwim Zilizofanywa Na Chadema Ni Msingi, Na Data Zilizopo Kwa Katibu Mkuu Taifa, Chadema Imeweka Lekodi Afrika Kwa Kuwa Na Wanachama Wengi Kikiongoza Tanzania Kwa Kuwa Na Wanachama Zaidi Ya Milion 10, Huku Ccm Kikishuka Kutoka Wanachama Milioni Tano Mpaka Milion Tatu Na Upuzi, Hii Ni Kutokana Na Chadema Kusimika Viongozi Toka Ngazi Ya Ubalozi Mpaka Taifa, Na Watu Walijitokeza Kugombea Ubunge Mwaka Huu, Zaidi Ya Elfu Nne NChi Nzima,
 
Hivi kwa nchi yetu kuwa mwanachama wa chama cha siasa ni lazima kuwa na kadi? Je kuichangia chama bila kuwa na kadi ni kosa? Kwa ufahamisho tu...Marekani ina wapiga kura zaidi ya milioni mia moja (>100,000,000) lakini idadi ya wenye kadi za chama hawazidi milioni tatu (<3,000,000) sawa na asilimia tatu (<3%). Kadi inatakiwa pale tu unapotaka kugombea uongozi ama ndani ya chama au kwenye chaguzi mbali mbali za uongozi serikalini. Kwa mfano wengi wanaoitwa "Democrats" asilimia zaidi ya tisini (>90%) si wanachama kwa maana ya kuwa na kadi, ni washabiki tu. Umuhimu wa kuwa na kadi ya chama hapa Tanzania ulikuwa ni wakati wa mfumo wa chama kimoja ambapo kadi ilikuwa ni kama paspoti ya kupata huduma za kijamii.
 
Chadema hawapendi ushauri,wanajifanya wanaijua siasa..kuna sehemu hadi leo hawajafika wanakimbilia ulaya na usa..ili walipane per diem nene.

Kusini uko kuna maeneo walisikia tu cdm walipita kisingizio msiba wa Makani au bajeti haitoshi, ila bajeti ya kufanya mikutano Arusha haikosekani.

Matokeo ya udiwani ni ujumbe mzuri kwa ukaidi wao.

Embu washauri ACT labda watakuelewa
 
Habari.
Si vibaya kujua haya ni wajibu wa kila Mwanachama wa Chama cha Siasa kujua idadi kamili ya wanachama nchi Nzima.

Je Chadema Ukawa kwa ujumla ina wanachama wangapi hadi hivi sasa?
 
Matokeo ya kula za maoni ndan ya CHADEMA ambayo yanaendelea kutolewa yanahashilia kuwa chama bado kinahitaji kuongeza nguvu ya kusajili wanachama wapya .

Mtu anashinda kwa kula 88 na kula zilizopgwa ni zaid ya kula mia moja ukizngatia jimbo lina wapiga kula zaid ya 50000.

2010 vita ya CCM ndani kwa ndani ilichangia sana CHADEMA ikazoa Wabunge katika maeneo ya mijini kama Dar na Iringa.

Kuna umuhimu wa chama kuzidi kusajili watu ili kuwa na safari ya uhakika.
 

Attachments

  • 1437449099608.jpg
    1437449099608.jpg
    31.7 KB · Views: 913
  • 1437449147792.jpg
    1437449147792.jpg
    34.1 KB · Views: 781
  • 1437449176267.jpg
    1437449176267.jpg
    37.8 KB · Views: 777
Back
Top Bottom