CHADEMA kina wanachama wangapi?

Ndio wafanye utaratibu wa kuwafanya mashabiki wawe wanachama na kukusanya wanachama zaidi ili come 2015 wavune kura nyingi.

asante mkuu,hilo ndio neno na kuna watu wanaenda kwenye mkutano wana pesa na wanahitaji kadi ila hawajui wazipate wapi na hawana muda wa kuzitafuta kwenye mashina au ofisi za chadema.
 
kwani wanaopiga kura ni wanachama au wananchi/washabiki?
 
CDM ni hisia na ufaham, na sio vitambaa na magwanda kama u_ccm.
 
Heri mimi ni mwanachama hai tangu 2007"
 

mbona swali la mwanakijiji lipo waz we taja idadi ya wanachadema tujijue tupo wangap mipango bila takwimu ni sawa na kazi bure
tuache ushabiki kwenye mambo ya msingi kijana
 
Waungwana napenda kuwapasha hiki kuwa chama chenye wabunge wa upinzani wengi Mjengoni Dodoma, kimekubwa na masahibu gani, kwa nini kina wafuasi wengi huku kikiwa na idadi ndogo ya wanachama wanaokadiriwa kutofika LAKI MBILI (200,000). Wakerekeretwa mliopo JF manatakiwa mkashaurine kupitia vikao vyenu halali na kujitathimini namna ya kutanua wigo wa wanachama. Wenzenu CCM hadi Februari 28, 2013 ilikuwa na wanachama wasiopungua MILIONI SITA (6,000,000). Mheshimiwa Mnyika jitihidi kukitangaza chama na kuingiza wanachama wengi badala ya ktumia muda na nguvu nyingi katika vita dhidi ya Professa Maghembe, kwa vilehoja zako ni dhaifu hivyo utaangukia pua.
 
Kama na wewe ni miongoni mwa hao 6,000,000, no wonder miaka 51 sasa tangu uhuru lakini tunashauriwa ''kukimbia wakati wengine wanatembea'' (Alisemaga Gorani Haideni).

Kumbe wewe ndiye uliyewasumbua walimu wetu waliosahihisha mitihani ya kidato cha nne kwa kuwachorea Zombi...
 
Huna lolote wewe nadhani usipo post lolote hapa hutalipwa na Nape au vipi????

 
duh una moto kweli hata kaburu alisema mandela hawezi kuongoza sa
 

Matola ni ccm!!! bado sijakubali.

Nakubaliana na matola kwamba ni ngumu sana kutunza kumbu kumbu ya wanachama hata ktk ngazi ya kata/shehia/ kijiji/mtaa/. Kwa mfano mijini watu wanahama kila siku hivyo ni ngumu sana mtu kuanza kutafuta ofisi ya Chadema na kujisajili upya kama mwanachama x aliyehama kutoka tawi z. Hii ni kazi ngumu sana -wanachama wa vyama vyote hawafanyi hiivyo. Ndo maana mwaka wa kupiga kura ya maoni ya wagombea udiwani ndani ya ccm makatibu wanageuka kuwa almasi ghafla. Kwanini? Ndo watakaotengeneza list ya wapiga kura.

Hata wenyeviti au watendaji wa vijiji/mitaa wanaolipwa mishahara nimewauliza mara nyigi kuhusu idadi ya watu wanaowaongoza - HAWANA. Kwa hiyo, kama mtendaji wa mtaa hana idadi ya wakazi wake ina maana kuwa hata mkurugenzi wa wilaya na mkuu wa wilaya hawana idadi kamili ya wakazi wao (isipokuwa mwaka wa sensa tu -baada miaka 10) Sasa kuuliza swali kama hili kwa chama cha upinzani chenye ruzuku ndogo siyo kututendea haki.
 
Idadi kamili ya wanachama wa cdm haijulikani wengi wanaungaunga leo wapo kesho hawapo no wonder kila mikutano yao wanaojitokeza kujiunga ni walewale
 

Mafalili,
Jimbo la ukonga mwaka jana december tulipeleka majina ya wanachama Laki 4 na nusu halafu unasema Chadema nchi nzima wawe wanachama laki mbili tu?????? Aibu yako. Nyinyi mnaotunga story za uwongo ndo mnatuharibia JF.
 
Mwanajiji ushauri mmoja.

Wakati wa uchaguzi wanaccm siyo lazima wapige kura kwa mwanaccm mwenzao na siyo lazima wanachadema wote wapige kura kwa mwanachadema mwenzao.

Haiwezekani chadema wakamsimamisha Fisadi jimbo la x halafu utegemee kila mwenye kadi ya Chadema atampigia kura huyo fisadi kuwa Mbunge. Kwa hiyo, upigaji kura unategemea mgombea mwenyewe wakati wa uchaguzi, agenda, nk.

Pili usilinganishe USA na Tz. Marekani kuna wapiga kura wa aina tatu, Democrat, republican na wasio na upande au wanaosubiri kampeni aka swing states.Hawa wanasubiri agenda, mgombea, sera nk Sasa lazima ujue Tanzania wanachadema na wanaccm siyo kama Reps na Dems. Nchi nzima ni swing state itategemea mgombea, agenda zakeetc.

Hata hivyo, Tofauti hapa tu ni kwamba ccm kama chama imejichafua kitaasisi kiasi ambacho wakimchagua mgombea mzuri bado atakuwa na wakati mgumu kwa kuwa watu wamewakatia tamaa.

For sure, in this regard,partisanship is very useless wakati wa kupiga kura.
 
mimi huwa nachukia sana watu wanafiki,hao ndo wapo kwa washabiki wengi wa chadema,inaniuma sana yaani watu unawaona wakijazana kwenye mikutano ya chadema na kufurahia sera lakini kwenye kupiga kura hawaonekani.kwa
utafiti wangu mdogo nliyoufanya nmegundua watu wengi wasiopga kura ni watu wanaoichukia CCM hvyo kupelekea kuikosesha chadema kura.kama hauwamini fanya simple survey utagundua watu wasioipenda CCM ndio hawapigi kura matokeo yake wanaishia kupiga kelele tu mtaani yaan wamejaa unafiki tu!!
 
Huna tofauti na sokwe unashindwa kuainisha matatizo ya tz eti unahangaika na cdm, utoroshwaji wa twiga wetu kwenda nje,madini kuporwa,tembo wanaisha,mabilioni yanafichwa nje nk hayo huyaoni eti? bk7 shame on u na waliokutuma
 
Wambie hao chama cha mafisi waruhusu uandikishaji wapiga kura wapya afu kutokee uchaguzi kidogo ndo mtajuta kuzaliwa nyie nyinyiem
 
OK, pitia Lumumba hapo maana siku hizi dau limepanda hadi buku saba jero
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…