Baada ya malalamiko ya waliojitoa CHADEMA (Viongozi waandamizi) niliunganisha dots za tabia ya Mheshimwa Tundu Lisu na kuona alikuwa hajaacha uanasheria mhivyo mtambuwe anachokiona mwanasheria kuwa kosa litabaki kuwa kosa na analoliona lipo right litabakia kuwa hivyo.
No Reform no Election aliilenga kwa wenzake chama kibadilike kimsikilize mtu mmoja tu kama hilo haliwezekani hagombei mtu.
Mheshimiwa Mbowe aliweza kula na vipofu na alikula vizuri tu. na Chama kilikuwa na kufikia tishio kwa utawala uliopo madarakano kupitia Uchaguzi mkuu.
Je Lisu ni pandikizi la CCM ndani ya Chadema ? Unaweza kusema haiwezekani ila pia unaweza kuhisi inawezekana Huyu mtu alitembelewa mara mbili tatu na wakuu mbali mbali wa CCM wakidai kumjulia hali,wengine tukijiuliza inakuwaje ? Na wengine tukiona ni ubinadamu.
Leo hii Chadema wanagawana mbao ,inasemekana hakuna kikao wala kamati au maandazi yaliokutana tokea Lisu aokote ukuu wa Chadema,ukuu ambao aliupata kwa mapambano ndani na kwenye mitandao.
Lisu si mwanasiasa ni mwana sheria ingawa wapo waliona yote hayo na huyapa haki zake sawa. Lisu alitunga sheria kwenye ubongo wake akizipitisha ndani ya kifua chake na kuzitekeleza bila ya kumshauri mwengine ni yeye tu,Jamani Lisu ndie mwenyekiti inabidi mumsikilize na mkubaliane nae ,si ruhusa kukataa au kupinga.
Chadema hadi sasa wapo njia ya panda ,nayaona yale ya CUF na Lipumba ambae alitumika na kufanikiwa kuivuruga CUF ,leo hii hajulikani yeye na chama chake wamefifia kabisa hawasikiki labda ukikaribia msimu wa ruzuku wakatiwe chao na CCM na ndipo inapoelekea CHADEMA chini ya Mwanasheria Tundu.
Naona ni bora Chadema ikakaa chini na kuitisha kikao cha kitaifa emergency ,iwe hivyo na kukinusuru hiki chama hata ikibidi Tundu Lisu afukuzwe au aondolewe ,kuna mambo ni magumu lakini inapobidi ni lazima yafanywe ,sidhani kama Chadema itapotea kama itamtoa kafara Tundu.
Kwa vyama vyote epukeni kubadilisha wakuu wa Chama hasa Wenyeviti ,Mbowe ameifikisha mbali sana Chadema ilikuwa waachiwe mpaka atakapojiuzulu au kufariki ,sio mnabadilisha badilisha kwa kuwa tu mtu mmoja anataka awe yeye, ndio mmeona kavuruga kila kitu.
Mwenyekiti awe kama mzee wa kimila au mkuu fulani hivi mfano wa akina Mkwawa ,iwe hivyo ,nafikiri ACT wamezuia kubadilisha mwenyekiti wao japo kuna kauchaguzi ni tayari wameshajiwekea ile nafasi sio ya kubadilishwa badilishwa ,kama Uraisi wa nchi kila baada ya miaka kumi.
Chama cha siasa ni taasisi inayotakiwa idumu kwa muda mrefu sana sana na vyeo vyake visiwe vya kuchezea chezea ikiwa hakuna tuhuma zenye uhakika wa mia kwa mia. Chadema walikuwa hawana haja ya kubadilisha Mwenyekiti na nikimalizia Mwenyekiti si lazima awe mgombea wa Uraisi wa Tanzania.
No Reform no Election aliilenga kwa wenzake chama kibadilike kimsikilize mtu mmoja tu kama hilo haliwezekani hagombei mtu.
Mheshimiwa Mbowe aliweza kula na vipofu na alikula vizuri tu. na Chama kilikuwa na kufikia tishio kwa utawala uliopo madarakano kupitia Uchaguzi mkuu.
Je Lisu ni pandikizi la CCM ndani ya Chadema ? Unaweza kusema haiwezekani ila pia unaweza kuhisi inawezekana Huyu mtu alitembelewa mara mbili tatu na wakuu mbali mbali wa CCM wakidai kumjulia hali,wengine tukijiuliza inakuwaje ? Na wengine tukiona ni ubinadamu.
Leo hii Chadema wanagawana mbao ,inasemekana hakuna kikao wala kamati au maandazi yaliokutana tokea Lisu aokote ukuu wa Chadema,ukuu ambao aliupata kwa mapambano ndani na kwenye mitandao.
Lisu si mwanasiasa ni mwana sheria ingawa wapo waliona yote hayo na huyapa haki zake sawa. Lisu alitunga sheria kwenye ubongo wake akizipitisha ndani ya kifua chake na kuzitekeleza bila ya kumshauri mwengine ni yeye tu,Jamani Lisu ndie mwenyekiti inabidi mumsikilize na mkubaliane nae ,si ruhusa kukataa au kupinga.
Chadema hadi sasa wapo njia ya panda ,nayaona yale ya CUF na Lipumba ambae alitumika na kufanikiwa kuivuruga CUF ,leo hii hajulikani yeye na chama chake wamefifia kabisa hawasikiki labda ukikaribia msimu wa ruzuku wakatiwe chao na CCM na ndipo inapoelekea CHADEMA chini ya Mwanasheria Tundu.
Naona ni bora Chadema ikakaa chini na kuitisha kikao cha kitaifa emergency ,iwe hivyo na kukinusuru hiki chama hata ikibidi Tundu Lisu afukuzwe au aondolewe ,kuna mambo ni magumu lakini inapobidi ni lazima yafanywe ,sidhani kama Chadema itapotea kama itamtoa kafara Tundu.
Kwa vyama vyote epukeni kubadilisha wakuu wa Chama hasa Wenyeviti ,Mbowe ameifikisha mbali sana Chadema ilikuwa waachiwe mpaka atakapojiuzulu au kufariki ,sio mnabadilisha badilisha kwa kuwa tu mtu mmoja anataka awe yeye, ndio mmeona kavuruga kila kitu.
Mwenyekiti awe kama mzee wa kimila au mkuu fulani hivi mfano wa akina Mkwawa ,iwe hivyo ,nafikiri ACT wamezuia kubadilisha mwenyekiti wao japo kuna kauchaguzi ni tayari wameshajiwekea ile nafasi sio ya kubadilishwa badilishwa ,kama Uraisi wa nchi kila baada ya miaka kumi.
Chama cha siasa ni taasisi inayotakiwa idumu kwa muda mrefu sana sana na vyeo vyake visiwe vya kuchezea chezea ikiwa hakuna tuhuma zenye uhakika wa mia kwa mia. Chadema walikuwa hawana haja ya kubadilisha Mwenyekiti na nikimalizia Mwenyekiti si lazima awe mgombea wa Uraisi wa Tanzania.