Ludovick anaweza kuwa na ubaya mkubwa kuliko ubora, na akawa mdanganyifu kambambe kulilko ukweli. Lakini hata jambazi siku inafika anakumbuka kulia 'mama yangu', mama ambaye kamuasi na kuyakataa mafundisho yake.
Umemshauri vizuri, kwamba aanze kutoa ushauri bora kwa ccm kama wanamsikiliza na kumwamini.
Upande mwingine, taarifa anayotoa si ya kuikubali moja kwa moja na wala si ya kuidharau moja kwa moja. Si vizuri kuamini kila kitu lakini pia ni vyema kutokudharau taarifa. Ludovick, hata kama ana mkataba wa uharamia na kundi lolote kwa ajili ya tumbo, huyu ni binadamu mwenye dhamira na nafsi ambavyo mara zote huwa vina nguvu ishindayo fedha, njaa na hata uchungu wa kifo.
Inteligencia na uongozi msikilizeni. Wasilianeni naye awaambie anachotaka mkifahmu, nanyi mkichunguze mpate ukweli. Si lazima kila kitu kiandikwe hapa mtandaoni. Hakuna hasara ya kujiridhisha kwamba anawadanganya kulioko majuto ya kudharau taarifa.
Utakuwa upuuzi wa aina yake kwenda kumsikiliza mhalifu eti akujuze wapi mhalifu mwenzie tafanya uhalifu kwenye Mali/Eneo lako.Ila cha msingi hapa ,ni wazi kuwa njama dhahiri iko njiani kufanywa/kutokea ndani ya CDM na hili si geni maana Madiwani toka Shinyanga wamelisema ,sasa inawezekana kukwama mpango wa kwanza Plani ya Pili iko njiani -Hivyo taarifa hii yaweza kuwa na harufu hivyo ni vizuri Idara husika ikafanye tathimini.