CHADEMA huwatetea wananchi kwenye mambo gani?

CHADEMA huwatetea wananchi kwenye mambo gani?

Kila kona ni kilio cha Tozo kiasi kwamba Watu hawaelewi kinacholiliwa ni nini hasa

Binafsi najiuliza Chadema hujinasibu kuwa wao ni watetezi wa wananchi, je huwa wanatutetea kwenye mambo gani?

Mungu ni mwema wakati wote!
Lakini shaka na kinana wanakiimarisha chama 20225 ni kupita bila kupingwa tena
 
Kwani chadema mnatetea nini sasa? Ushoga?
.
IMG_20211130_182246.jpg
IMG_20211011_195427.jpg


Sent from my SM-N9150 using JamiiForums mobile app
 
Kwani wakati wanateswa na utawala dhalimu mbona mlikaa kimya kwa kuona hayawahusu. Acha nao wakae kimya hayawahusu.
 
Uko sahihi bwashee. Chadema ya kutetea wananchi ilikuwa enzi za Dr slaa, hii ya sasa ni genge la wahuni fulani wachumia tumbo na walamba asali tu.
Kwani wananchi nao waliwatetea chadema wakati wanateswa na magu,KILA mmoja apambane na hali yake
 
Binafsi najiuliza Chadema hujinasibu kuwa wao ni watetezi wa wananchi, je huwa wanatutetea kwenye mambo gani?
Kwa nini usilaumu CCM wanaoleta matatizo, badala yake unalaumu CHADEMA kwa kutotetea wananchi wanaopata matatizo yanayoletwa na CCM? Huoni kusubiri matatizo yatokee halafu yaje yatetewe ni mlolongo mrefu kuliko kuzuia matatizo yasitokee? Wenye dhamana ya kuongoza serikali ni CCM, CHADEMA katika uwakilishi wa wananchi haina nguvu bungeni
 
Hata wao wanatambua juhudi kubwa Zinazofanywa na mh Rais wetu, wanatambua na wanaona namna fedha hizo zinavyotumika katika kusimamisha miradi mbalimbali ya maendeleo inayogusa maisha ya watu, wanatambua kuwa Ni lazima nchi ijengwe na wananchi wenyewe na kwamba hata huko ulaya walipitia huku tuliko sisi

Tumuunge mkono mh Rais na tumsemee mh Rais kwa kazi kubwa anazozifanya
 
Kila kona ni kilio cha Tozo kiasi kwamba Watu hawaelewi kinacholiliwa ni nini hasa

Binafsi najiuliza Chadema hujinasibu kuwa wao ni watetezi wa wananchi, je huwa wanatutetea kwenye mambo gani?

Mungu ni mwema wakati wote!
Ndio matokeo ya kuiba uchaguzi na kuzima mikutano ya hadhara. Sasa ngoja tule jeuri ya CCM (JPM na Mwigulu/zungu) na bado. Tulikuwa tunatoa maziwa sasa twatoa damu baadae ni usaha na kifo.
 
Mbona wakati wa JPM awakukaa kimya ...unajua kwanini ? Chadema ni vibaraka wa mafisadi wa nje na ndani ya nchi wala siyo watetezi wa haki ndiyo maana kwa sasa wamenyamaza tofauti na kipindi cha JPM kwa sababu tayari mafisadi wa ndani na nje ya nchi wameshika uongozi na hapo sasa ndipo chadema imejimaliza kabisa yenyewe .
Ukweli ni kwamba chadema ni genge la wahuni tu hakuna chama pale msipoteze muda wenu bure ...mbinu ya sisi wananchi kupambana na wahuni wa ccm na chadema ni kuwa na msimamo wa kuwa kataaa katika kila jambo la uchawa na upumbavu kama sensa nk
Sasa kwanini mnataka wawatetee na kwenye kila kosa la ccm analaumiwa chadema?

Mimi nadhani ni wakati sahihi wa ccm kufanya kazi yake bila kuingiliwa na wapinzani wanaowatetea mabeberu kwakuwa hata bungeni hawapo,

Inafika wakati hata wao chadema mnawachanya wakisimama kuwateteeni mnawapinga na kuwakejeli huku mkifurahia maumivu yao wanayoyapata na wakikaa kimya nyienyie ambao ndio huwa mkiwapinga mnaanza kuleta kelele nyingine kuwa chedema mbona ipo kimya haitetei watu...Sasa sijui nyie ni jamii ya watu gani msiojua uelekeo wenu.Tambueni mnachotaka.
 
mlipopeleka wabunge wa ccm tu bungeni na kuzuia mikutano ya vyama vya siasa mlitegemea chadema wawasemee toka wapi?

Wakidai katiba mpya itakayozuia mambo kama haya mnasema wana uchu wa madaraka.
Hawa watu ni wa ajabu sana lengo lao ni kusikia Chadema imeshafutwa hapo watapumua la sivyo wataendelea kuteseka mpaka mwisho wa dunia kwa sababu ya CHADEMA.
 
Back
Top Bottom