CHADEMA: Hatima ya Shibuda leo..

Mkuu nakubaliana na yote uliyosema hapo juu.Tatizo tulilo nalo ni kwamba vyama vya siasa ni lazima tuangalie katiba zetu na kanuni ili kukidhi matakwa halali ya kidemokrasia kwa maana ya kuzingatia demokrasia na falsafa iliyosimama nyuma yake.Hapa chini ni baadhi ya conditions amabzao zinaweza kutoa mwanya na nguvu kwa chadema kumfukuza mbunge yeyote ingawa sitaenda deep kwa sasa kwa sababu maalumu

Kwanza kabisa kuna wajibu kama huu kwa mwanachama:
5.3.4 Kushirikiana na wanachama na viongozi wengine wote katika kutekeleza sera na mipango ya Chama.”

.3 MAADILI

Maadili ya Chama ndiyo yatakayoainisha sifa, nidhamu, utii, uwajibikaji na dhamira yawanaChama, watendaji na viongozi wa Chama katika ngazi zote. Maadili haya yanajumuisha uongozi wa Mabaraza ya Vijana, Wanawake na Wazee.

2.4 ITIFAKI

CHADEMA kama Chama kinachokua na kupanuka kwa kasi kitaifa na chenye nia yakuchukua dola wakati wowote hakina budi kujiwekea taratibu mbalimbali ambazo zitakisaidia Chama kuendesha shughuli zake za Chama katika mtiririko wa aina fulanibila kuonyesha utofauti kati ya viongozi na ngazi mbalimbali za Chama. Nia ya kuwekataratibu hizi ni kuleta umoja na mshikamano ndani ya Chama na kukitambulisha

CHADEMA kama Chama kimoja.
Kwa hiyo itifaki ya Chama inajumuisha pia uongozi wa Mabaraza ya Vijana, Wanawake na Wazee ambayo ni sehemu tu ya muundo na uongozi wa chama.

Kufukuzwa Uanachama:

5.4.3 Kuachishwa ama kufukuzwa na tawi lake ama ngazi nyingine ya Chama, kwa mujibu wa katiba kwa kukosa sifa za kuendelea kuwa mwanachama ama kuwa na mwenendo usioendana na Itikadi, falsafa, madhumuni, kanuni, maadili na sera za Chama.

5.4.4 Bila kuathiri kifungu 5.4.3 cha katiba, Kamati Kuu inaweza kumwachisha amakumfukuza mwanachama yeyote kwa utaratibu utakaopangwa na kanuni za Chama.

Hizo ndiyo leaning walls/tables,

Sasa vipi kama tukitoa pendekezo la kutumia mbinu ya kisasa na ya kidemokrasia kwa mapana kwa kuitisha kura ya maoni jimboni ili kujua msimamo wa wanachama na wapiga kura wa jimbo la Maswa kuhuu tabia na mwenendo wa mbunge wao na pia kupata maoni yao juu ya adhabu itakayofaa/chukuliwa dhidi ya Mh.Shibuda

Sijui kama Collin Powel angekuwa mwanachama wa chama cha siasa Tanzania angekuwa nadni ya chama hicho baada ya kumpigia kampeni mgombea wa chama kingine.Je huu si usaliti kwa ideology na sera za chama husika?mwaka jana kwenye kampeni,tujiulize swali ambalo hatutaki au tumesahau kujiuliza,je kuna mgombea yoyote aliyempigia kampeni mgombea wa chama kingine?Tafsiri yake ni nini katika sera,philosophy and ideology of the party?

Julius Malema Mwenyekiti wa vijana wa ANC aliimba pamoja na wafuasi wake wimbo wa 'Kill the boers' ambao unaenda kinyume na falsafa ya sasa ya ANC na serikali yake ya kuponya majeraha ya kibaguzi,na hakufukuzwa lakini waliona fursa ya kum-shape psychologically ili awe fit na balozi mzuri wa kuponyesha majeraha na kujenga taifa moja kwa kutumia fursa komavu za kidemokrasia.

Tujiulize mbona ODM ya kenya hawakumfukuza Willium Ruto na akina Sally kosgei pamoja na sarakasi zote ndani ya chama chao,tuangalie faida waliyoipata as a serious political entity na hasara waliyoipata as a serious & weak political Entity.



Ben hapa kweli nakuunga mkono kupata maoni ya wengi kuwa wanamtaka au hawamtaki lakini unaona wewe mwenyewe mfano hapa JF wengi tunataka Shibuda aondoke kabisa ili iwe fundisho kwa wale wote wanaoenda kinyume na msimamo wa chama, any way najua CDM viongozi wetu ni watu makini sana tunaamini watafanya maamuzi sahihi..
 
Ni kweli kabisa mtu kama julius malema (President - ANC Youth league) kwa siasa za Tanzania angekuwa ameshafukuzwa zamani, ni mtu ambae ana ushawishi mkubwa sana ndani na nje ya ANC, na mara nyingi amekua akitoa mawazo yake nje ya vikao vya ANC ambayo mara nyingi yanapishana na sera za ANC, mfano mzuri ni ile sera ya nationalisation of mines, hii sio sera ya ANC lkn Malema siku zote anaisimamia, na mara nyingi sana amekuwa mstari wa mbele kupinga na kukosoa sera za ANC hadharani ambazo hazileti haki na usawa kwa kwa weusi

Ni kweli mkuu,hata ile position alyochukua against South Africa's position on Libya at UN security council ilikuwa even worse.Sipati Picha kama angekuwa mwenyekiti wa vijana wa chama cha siasa Tanzania.

Nilikuwa nae Nairobi last month aliniambia jinsi ilivyokuwa burning issue kwenye mkutanao wao wa party caucas uliofanyika Port Elizabeth mwezi April.It was a fire lakini walikuja na healing therapy na kumlea kisiasa ili awe consistent na party lines.He's a rare young Revolutionary comrade tulio nao Africa. Anyways,tutafika tu hata kwa Gharama ya Damu ili waafrika wapate ukweli na wafurahie kinyume na kile wanachodanganywa
 
Tatizo sio kumfukuza,tujiulize je anachokitetea Kinamaslai kwetu.Mimi nafikili kwanza tuanzie Hapo.
Mfinyanzi karibu Jf..achokitetea Shibuda hakina maslahi kwa Taifa au wewe unaona ongezeko la posho ktk vikao mbalimbali hasa vya wabuunge lina maslahi kwako?
 
Ni kweli kabisa mtu kama julius malema (President - ANC Youth league) kwa siasa za Tanzania angekuwa ameshafukuzwa zamani, ni mtu ambae ana ushawishi mkubwa sana ndani na nje ya ANC, na mara nyingi amekua akitoa mawazo yake nje ya vikao vya ANC ambayo mara nyingi yanapishana na sera za ANC, mfano mzuri ni ile sera ya nationalisation of mines, hii sio sera ya ANC lkn Malema siku zote anaisimamia, na mara nyingi sana amekuwa mstari wa mbele kupinga na kukosoa sera za ANC hadharani ambazo hazileti haki na usawa kwa kwa weusi

Kwa kweli kumfananisha Shibuda na Malema ni kumpaisha Shibuda. Pamoja na ujeuri wa Malema, mara zote anatetea wazawa au chama chake cha ANC. Malema hashabikii vyama vya upinzani. Sidhani kama Shibuda alikuwa anatetea wananchi au chama chake cha CDM. Kwa nini Colin Powell (rep) alimuunga mkono Obama(demo)? One can say, because they are both African-American. Naamini, muktadha wa haya mawili ni tofauti kabisa.

Mim sitashangaa kama watu wanaopenda chadema ianguke watataka kumtetea Shibuda. Kwanini Shibuda anashangiliwa sana na wabunge wa magamba anapoongea? Mwenendo wa Shibuda utakatisha tamaa wengi ambao wako 50-50, yaani watu ambao wako vuguvugu kiushabiki wa siasa . Mtu atajiuliza kwanini niwape kura hawa kama na wao hawawezi kuwajibishana?

Wakati mwingine, hata mm naombea hivi vyama uchwara vya upinzani vife ili tuweze kufikiria plan B, maana kila unapoanza kufikira kwamba upinzani unakua, ghafla chama kinaporomoka. Jamani kulikuwa na NCCR na CUF, viko wapi hivi vyama siku hizi? Chadema kimekuwa haraka haraka sana kuanzia 2005 mpaka leo, kiasi kwamba ukuaji wake unatishia uhai wake maana kinakua kwa idadi ya wanachama na wafuasi bila kukua mifumo ya kukiendesha chama. Chadema wasipokuwa makini, they are going the way of the Dodo!
 
shibuda lazima yafanyike maamuzi magumu ya kuumundoa kwani kwani anabomoa chama badala ya kujenga wananich tunamwona ,tunamsikia avyofanya hakuna wakati wa kupoteza mda bora jimbo liende kwa CCM kuliko kuwa na mbunge anayejifanya ni CHADEMA kumbe ni CCM
 
Ni kweli mkuu,hata ile position alyochukua against South Africa's position on Libya at UN security council ilikuwa even worse.Sipati Picha kama angekuwa mwenyekiti wa vijana wa chama cha siasa Tanzania.

Nilikuwa nae Nairobi last month aliniambia jinsi ilivyokuwa burning issue kwenye mkutanao wao wa party caucas uliofanyika Port Elizabeth mwezi April.It was a fire lakini walikuja na healing therapy na kumlea kisiasa ili awe consistent na party lines.He's a rare young Revolutionary comrade tulio nao Africa. Anyways,tutafika tu hata kwa Gharama ya Damu ili waafrika wapate ukweli na wafurahie kinyume na kile wanachodanganywa

..not so fast, we ar talking about a young man who is alleged to have unexplained wealth.
 
Hivi bado hajafukuzwa tu???

CHADEMA just be serious, mbona mnakua kama magamba?

Hawa watu itabidi wani-convince sana kuwaamini tena wasipo mfukuza
shumbuda,watakua wanalea tabia mbofu mbofu katika chama,...

ni chama kukosa mbunge kabisa,kuliko kuwa na mbunge kama shumbuda
 
Kwa kweli kumfananisha Shibuda na Malema ni kumpaisha Shibuda. Pamoja na ujeuri wa Malema, mara zote anatetea wazawa au chama chake cha ANC. Malema hashabikii vyama vya upinzani. Sidhani kama Shibuda alikuwa anatetea wananchi au chama chake cha CDM. Kwa nini Colin Powell (rep) alimuunga mkono Obama(demo)? One can say, because they are both African-American. Naamini, muktadha wa haya mawili ni tofauti kabisa.

Mim sitashangaa kama watu wanaopenda chadema ianguke watataka kumtetea Shibuda. Kwanini Shibuda anashangiliwa sana na wabunge wa magamba anapoongea? Mwenendo wa Shibuda utakatisha tamaa wengi ambao wako 50-50, yaani watu ambao wako vuguvugu kiushabiki wa siasa . Mtu atajiuliza kwanini niwape kura hawa kama na wao hawawezi kuwajibishana?

Wakati mwingine, hata mm naombea hivi vyama uchwara vya upinzani vife ili tuweze kufikiria plan B, maana kila unapoanza kufikira kwamba upinzani unakua, ghafla chama kinaporomoka. Jamani kulikuwa na NCCR na CUF, viko wapi hivi vyama siku hizi? Chadema kimekuwa haraka haraka sana kuanzia 2005 mpaka leo, kiasi kwamba ukuaji wake unatishia uhai wake maana kinakua kwa idadi ya wanachama na wafuasi bila kukua mifumo ya kukiendesha chama. Chadema wasipokuwa makini, they are going the way of the Dodo!

You said it boss,no wonder kuna mtu anatoa "likes" sana humu hajakupa maana umemgusa!
 
Fikra zilizokufa always huwafaa wafu mana dunia yao ni nyingine kabisa,Fikra hai always ni kwa walio hai so tuache mfu arudishwe kwenye wafu wenziwe na kutacha sisi tulio hai na huai wetu.Aipingae kweli ni shabiki wa uongo
 
Shibuda mtu wa shoka sana! CDM ebu achane kumnyanya Shibuda au kwa sababu msukuma, mbona kina Selasini wamesifia shule za kata kamsifia JK, mbona mlikuwa mmekaa kimya au kwa sababu ni Mchagga mwenzenu? Wasukuma zindukeni hamtakiwi CDM
 
Amin nawaambia,mtu kama shibuda ingempasa jiwe la kusagia lifungwe shingoni mwake akatupwe kwenye vilindi vya bahari.
 
Shibuda mtu wa shoka sana! CDM ebu achane kumnyanya Shibuda au kwa sababu msukuma, mbona kina Selasini wamesifia shule za kata kamsifia JK, mbona mlikuwa mmekaa kimya au kwa sababu ni Mchagga mwenzenu? Wasukuma zindukeni hamtakiwi CDM
Hawa jamaa wanaonewa sana,wabunge wao waliokuwepo mtandaoni tuliwauliza kuhusu posho(haswa mkopo wa magari)...walikuwa wanajing'atang'ata tu!!,mnyika alisema atakuja march nane...mpaka leo.Regia akasema nimeambiwa mshahara wetu ni siri kubwa...but people found out anywayz.
Ukijaribu kuchunguza,hawa wabunge kweli ni wanafiki tu,wote wanataka posho kubwa na Zitto kuongelea sitting allowances was a bit of suprise to them.Ndio maana utaona wanavyomchukia humu ndani.

Shibuda ni mchumia tumbo kama wabunge wengi tu mjengoni....acheni unafiki,hamna cha falsafa wala nini.Mlijua kabla,mkataka ruzuku iongezeke,sasa inawatokea puani.
 
By the way zitto is not trusted!!! anaonekana kuanzisha makundi ndani ya cdm just kwa kutumia ushawishi kidogo alio nao...Lakini sishangai just see the following analysis of kigoma politicians in cdm
Dr Aman Walid Kaburu------from kigoma....was in CDM kwa unafiki akarudi CCM
David Kafulila....From kigoma.....Was in CDM umbea na kutoa siri za chama caused him to go to NCCR MAGEUZI
Zitto Kabwe...From kigoma.....In CDM now but not Trusted.......to no one knows but i dought magamba part
from above analysis i don't tust zitto

kaka pleas stop,

haya maneno yako yanataka kuturudisha kule tulikovuka tayari, kule kwenye dhana ya cdm ni ya ukabila na ukanda.
so unapoaanza kuwataja watu wa eneo fulani kuwa hawaaminiki ni dalili ya wewe kutaka kutuchonganisha wanachadema.
Hili lako la kutoa takwimu za watu na liwe lako tu, na hutafanikiwa kuwahadaa wana chadema kwa mlengumo wako wa ulimi mnyoofu wa mipambino na pamabaja za ulimi.
ukabila na ukanda unaotaka kuupanda upya tulishauzika na hauoti kamwe.
 
Wanachama wa magamba mliochangia mada hii kwanza mna kilio kwenye chama chenu kauguzeni madonda yenu msilete za kuleta hapa,shibuda ni nani ndani ya chadema,kama alitumwa na magamba party eti kuisambaratisha chadema kama alivyofanya mrema amenoa atafukuzwa tu.analeta kiswahili cha kizanzibari tuone kama kitamsaidia maamuzi ya chama yatachukua mkondo wake.
 
Back
Top Bottom