Saint Ivuga
JF-Expert Member
- Aug 21, 2008
- 55,028
- 59,657
shibuda kapinga sera cha chadema....
Tangu shibuda aingie cdm, alichukuliwa kwa tahadhari zote. Hivyo usitegemee atakuwa ana impact yoyote zaidi ya hicho kiti cha ubunge!Nyie CDM hamna ubavu wa kumfukuza Shibuda; maana mlipomchukua mlifikiri mmefanikiwa; lakini sasa akiwa ndani au nje ya CDM atawamaliza maana mmemeza ndoano. Hahaha! Tusubiri maana ndoa sasa imekuwa ndoano.
Ipi imetangulia kwako...ilani ya CDM au kauli ya Zitto?kama hyo ilikua ilani ya cdm, kwa nini zito alikua anawakilisha kama hoja yake? akawapa kazi ngumu akina mbowe kutangaza kuwa ni mpango wa cdm sio ya mtu mmoja, naona sasa cdm wanazidiwa na power strugleendeeni kumalizana tu ccm hamitoi kwa style hii
Tunahitaji nguvu ya pamoja tunapokuwa kwenye mapambano kama ilivyo sasa cdm dhidi ya magamba. Hatuwezi kufikia malengo ya vita hii kwa kurudishana nyuma sisi wenyewe kama anavyofanya shibuda.Anastahili kusamehewa iwapo ataomba msamaha kwa wanachama wotw na kuahidi kutopingana tena na mwelekeo wa wengi.Hivi unadhani kama wanachama na wapenzi wa cdm wakilipigia kura swala hili kuna mtu wangapi wata unga mkono kauli ya shibuda eti ni uhuru wa mawazoa? Ni lazima tukubaliana pia kuwa siyo kila mtu anaweza kutoa wazo la kujenga nchi yetu hata kama kuna uhuru wa mawazo!Je wazo la shibuda linajenga nchi yetu au linabomoa japo ni wazo huru?Tuwe wakweli katika dhamiri zetu na siyo kutetea kila kitu.Tuwaache cdm waamue hatima ya shibuda wanayohaki ya kumpa adhabu yoyote na kusiwe na impact yoyote kwenye chama.Umepotoka na kinyume chake ni sahihi...Tunahitaji wanasiasa wenye mawazo huru wengi zaidi ili tutoke hapa tulipo kama taifa, ule wakati wa fikra sahihi kwa jina la chama umekwisha...
Nasikia Kabourou anataka kurudi......Aliondoka Kabouru katibu wa mkuu atakuwa Shibudu.
Hatukatai Shibuda asipewe onyo..lakini huyu jamaa amepitiliza hata hiyo adhabu unayosema apewe maana jana TBC Taifa wameripoti alikuwa Mbeya kwenye mkutano wa CCM..pia hatukatai aende kwenye mikutano ya chama chochote ila kinanisikitisha mimi huyu jamaa huwa hahudhurii maandamano ya CDM sasa swali la kujiuliza hapa ni kweli Shibuda mfuasi mwaminifu wa CDM?..mimi binafsi naona hapana huyu ni mwongo tena asipofukuzwa kuna siku ataleta madhara hasa chama kinapotaka kufanya mamuzi magumu shibuda atatutenga..jamani nasema tena tunarudia kusema BORA AFUKUZWE SASA KULIKO AENDELEE KUWEPO halafu 2014 ajiuzulu then atupake matope tukiwa tunaelekea kwenye uchaguzi mkuuSpeaker,
Nakubaliana kabisa na utaratibu wa kutoa adhabu ya kumfukuza mtu uanachama pale anapokiuka taratibu. Ninaamini pia kuhusu kuonya kwanza kabla ya kutoa adhabu hiyo. Ndio maana naamini kuwa, kutokana na uchanga wa Shibuda ndani ya chama na malengo ya chama kwa hv sasa, anastahili kupewa ONYO kwa sasa! Ni mtazamo wangu huu! Kwenye soka kuna kadi ya njano na nyekundu hata kama ni mechi ya kirafiki! Na refa ananafasi ya kuamua kulingana na alivyoona kosa lilivyofanyika aina ya adhabu ya kutoa. Ndio maana nasisitiza kuwa kamati iangalie kanuni, taratibu na katiba, kisha waangalie mkosaji na namna kosa lilivyofanyika ndio watoe maamuzi. Kwa maoni yangu wampe onyo kali tu kwa sasa!