Victor Yohana
Member
- Apr 30, 2013
- 31
- 31
Na Victor Yohana
(uvccmichenjezya@gmail.com)
Mapema mwaka huu tulitangaziwa kuwa Dunia imeingiwa na ugonjwa wa CORONA. Tanzania ilikuwa nchi moja wapo ambayo ilishukiwa kuwa kuna watu wana dalili za virusi vya CORONA alimaarufu COVID -19.
Wakati Dunia ikiendelea kutafuta tiba, Tanzania ilikuwa ikiendelea na vikao vya bajeti (Bunge). Rais Magufuli ambaye ni kiongozi wa nchi aliliongoza Taifa kwenye kupambana na vita hii, huku akiwasisitizia Watanzania kumuomba Mungu. Alisema Mungu ndiye Mweza wa yote, hivyo katika yeye TUTASHINDA! Alizungumza maneno haya mazito nchi nyingi Duniani zikiwa lockdown. Lakini yeye alisema hawezi kuwaweka Watanzania lockdown, kwani madhara ya lockdown ni makubwa kuliko Ugonjwa wenyewe.
Wakati Rais akitamka hayo, Wabunge kupitia CHADEMA walikimbia bungeni na kuwataka Wafuasi wao kutoshiriki mikusanyiko yoyote ikiwemo Ibada. Walisema Watanzania wengi wanakufa na serikali inaficha. Lakini walipoulizwa kati yenu Wabunge mnaoeneza mambo hayo, ni nani familia yake imekufa kwa CORONA? Hawakutoa majibu zaidi ya kubwabwaja maneno na kujifungia ndani.
Wakati CHADEMA wakikimbia Bungeni, wachambuzi wa Mambo ya siasa tuliandika kuwa CDM wametazama mbele na kuona Uchaguzi utakuwa mgumu kwao. Walitaka watumie kigezo cha CORONA ili serikali iingie king na uchaguzi uahirishwe kwa sababu ya CORONA. Walijua ni ngumu kushinda uchaguzi huu, ndio maana waliamini Uchaguzi ukiahirishwa basi watapata nafasi ya wao kuendelea kula posho mwaka mwingine.
Kama kweli CHADEMA walikimbia Bungeni kwa sababu ya CORONA wakiamini kuwa mikusanyiko ni hatali kwao, kwa nini wanafanya kampeni huku wakiruhusu mikusanyiko. Kwani leo CORONA wametangaziwa kuwa imeisha? Kwa nini wasisusie Uchaguzi kama walivyofanya jaribio la kususia Bunge?
Hawa hawakukimbia Bunge kwa sababu ya CORONA, walikimbia Bunge kwa sababu ya kutaka kushawishi Dunia kuwa Tanzania kuna CORONA ili uchaguzi uahirishwe waendelee kuongoza majimbo yao wakati wananchi wamekwisha kuwachoka. Walitaka kutumia CORONA kama kichaka cha kujificha kwenye aibu ya matokeo ambao hadi sasa CCM inakadiriwa kuwa itashinda kwa zaidi ya asilimia 80.
Mbona hawajawatangazia Watanzania kuwa CORONA tuliyokimbia IMEKWISHA? Kama CORONA ipo, hawaoni mikutano wanayofanya ni kuongeza Maambukizo ambayo wao walikimbia Bungeni?
*NINAWAOMBA WATANZANIA WAWAJIBU KWA KUWANYIMA KURA, KWANI WALITUHUJUMU KWENYE BUNGE LA BAJETI*.
(uvccmichenjezya@gmail.com)
Mapema mwaka huu tulitangaziwa kuwa Dunia imeingiwa na ugonjwa wa CORONA. Tanzania ilikuwa nchi moja wapo ambayo ilishukiwa kuwa kuna watu wana dalili za virusi vya CORONA alimaarufu COVID -19.
Wakati Dunia ikiendelea kutafuta tiba, Tanzania ilikuwa ikiendelea na vikao vya bajeti (Bunge). Rais Magufuli ambaye ni kiongozi wa nchi aliliongoza Taifa kwenye kupambana na vita hii, huku akiwasisitizia Watanzania kumuomba Mungu. Alisema Mungu ndiye Mweza wa yote, hivyo katika yeye TUTASHINDA! Alizungumza maneno haya mazito nchi nyingi Duniani zikiwa lockdown. Lakini yeye alisema hawezi kuwaweka Watanzania lockdown, kwani madhara ya lockdown ni makubwa kuliko Ugonjwa wenyewe.
Wakati Rais akitamka hayo, Wabunge kupitia CHADEMA walikimbia bungeni na kuwataka Wafuasi wao kutoshiriki mikusanyiko yoyote ikiwemo Ibada. Walisema Watanzania wengi wanakufa na serikali inaficha. Lakini walipoulizwa kati yenu Wabunge mnaoeneza mambo hayo, ni nani familia yake imekufa kwa CORONA? Hawakutoa majibu zaidi ya kubwabwaja maneno na kujifungia ndani.
Wakati CHADEMA wakikimbia Bungeni, wachambuzi wa Mambo ya siasa tuliandika kuwa CDM wametazama mbele na kuona Uchaguzi utakuwa mgumu kwao. Walitaka watumie kigezo cha CORONA ili serikali iingie king na uchaguzi uahirishwe kwa sababu ya CORONA. Walijua ni ngumu kushinda uchaguzi huu, ndio maana waliamini Uchaguzi ukiahirishwa basi watapata nafasi ya wao kuendelea kula posho mwaka mwingine.
Kama kweli CHADEMA walikimbia Bungeni kwa sababu ya CORONA wakiamini kuwa mikusanyiko ni hatali kwao, kwa nini wanafanya kampeni huku wakiruhusu mikusanyiko. Kwani leo CORONA wametangaziwa kuwa imeisha? Kwa nini wasisusie Uchaguzi kama walivyofanya jaribio la kususia Bunge?
Hawa hawakukimbia Bunge kwa sababu ya CORONA, walikimbia Bunge kwa sababu ya kutaka kushawishi Dunia kuwa Tanzania kuna CORONA ili uchaguzi uahirishwe waendelee kuongoza majimbo yao wakati wananchi wamekwisha kuwachoka. Walitaka kutumia CORONA kama kichaka cha kujificha kwenye aibu ya matokeo ambao hadi sasa CCM inakadiriwa kuwa itashinda kwa zaidi ya asilimia 80.
Mbona hawajawatangazia Watanzania kuwa CORONA tuliyokimbia IMEKWISHA? Kama CORONA ipo, hawaoni mikutano wanayofanya ni kuongeza Maambukizo ambayo wao walikimbia Bungeni?
*NINAWAOMBA WATANZANIA WAWAJIBU KWA KUWANYIMA KURA, KWANI WALITUHUJUMU KWENYE BUNGE LA BAJETI*.