Nimekuwa nikufuatilia mwenendo wa cdm hasa baada ya kumalizika kwa uchaguzi mkuu mwaka 2010 , nilichogundua ni kwamba hiki chama kimekuwa kinatumia njia mbali mbali ili kuwahadaa watanzania kuwa cdm inapendwa na watanzania hasa kwa kufanya yafuatayo:
- kukusanya michango kutoka kwa wananchi maskini wa Tanzania.
- kutumia picha za kampeni za uchaguzi wa mwaka 2010 na kuziweka kwenye magazeti na mitandao ya kijamii ili kuwadaa watanzania kuwa mikutano cdm inahudhuriwa na umati wa watu.
- kulalama kwenye mikutano kuwa Tanzania ni nchi maskini sana bila ya wao kutoa njia mbadala ya kupunguza umaskini.
- kuwa na matumizi yanayozidi mapato ya chama kwa mwezi.