johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 83,968
- 141,976
Watu walio karibu na mgombea wa Uenyekiti wa Chadema mh Cecil Mwambe wamesema moja ya vipaumbele vya mgombea huyo ni kuhakikisha Chadema inajenga jengo la kisasa la makao makuu.
Ikumbukwe kuwa baada ya kuhama pale kisutu kwenye ofisi za rip Ndesamburo Chadema walijihifadhi mtaa wa Ufipa pale kinondoni kwenye nyumba ya NHC iliyokuwa chini ya rip Bob Makani. Baadae Chadema walifanikiwa kuimiliki nyumba hiyo na kuifanya kuwa makao makuu.
Wapambe wa Mwambe wanadai kuwa Chadema ni chama kikubwa kinachostahili kuwa na ofisi zenye hadhi yake kama lilivyo jina lake Chama cha Demokrasia na Maendeleo.
Pia Mwambe anatarajia kuupa nguvu umoja wao wa vijana yaani Bavicha ambao kwa sasa ni kama umekufa ganzi huko mikoani na kubakia Dsm tu.
Ni hayo tu kwa uchache.
Maendeleo hayana vyama!
Ikumbukwe kuwa baada ya kuhama pale kisutu kwenye ofisi za rip Ndesamburo Chadema walijihifadhi mtaa wa Ufipa pale kinondoni kwenye nyumba ya NHC iliyokuwa chini ya rip Bob Makani. Baadae Chadema walifanikiwa kuimiliki nyumba hiyo na kuifanya kuwa makao makuu.
Wapambe wa Mwambe wanadai kuwa Chadema ni chama kikubwa kinachostahili kuwa na ofisi zenye hadhi yake kama lilivyo jina lake Chama cha Demokrasia na Maendeleo.
Pia Mwambe anatarajia kuupa nguvu umoja wao wa vijana yaani Bavicha ambao kwa sasa ni kama umekufa ganzi huko mikoani na kubakia Dsm tu.
Ni hayo tu kwa uchache.
Maendeleo hayana vyama!