CECAFA Senior Challenge: Kutoka Uganda

CECAFA Senior Challenge: Kutoka Uganda

Tangu mzozo wa Lake Nyasa uanze siwezi kupenda Malawi hata kama wangevaa njano na kijani! Nadhani unafikiria wekundu wa Msimbazi.

Fu.ck the politics and let the game speak of itself...
Wanyasa wamependeza kwa uzi wao safi, my favourite color combo ni kijani na nyeupe, kama Gor Mahia, Wolfsburg, Werder Bremen, Celtics za Mangaung na Glasgow et cetera. Ujinga wa Yanga na Simba huwa hauko akilini mwangu, ukipita kwenye uzi kuna mahali nimeandika Yanga hoyeee wakati nikiripoti Niyonzima kuwa nahodha leo, ukija kichwa kichwa unaeza kunipakazia u-Yanga.
Viva la Coastal Union SC, 11 Ngamiani Street, Tanga Metropolitan.
 
Malawi wamekosa magoli ya wazi kabisa...
 
Naona beki wa Rwanda anataka kumfunga kipa wake...
 
Malawi wanafanya mabadiliko, Harawa anatoka na Bokosi anaingia...
 
Rwanda wanakosa goli tena, Niyonzima anapiga krosi safi kabisa, mshambuliaji wao ameshindwa kumaliza...
 
Haruna Niyonzima anafunga goli safi kabisa, goli toka nje ya 18.
Bonge moja la shuti...
 
Monday, November 26, 2012



IMG_3414.jpg

Beki wa Zanzibar, Nassor Masoud ‘Chollo', (kushoto) akitafuta mbinu za kumtoka beki wa Eritrea, katika mchezo wa Kundi C, Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge kwenye Uwanja wa Mandela, Namboole jioni hii. Timu hizo zilitoka sare ya bila kufungana.
IMG_3409.jpg

Kiungo wa Zanzibar, Khamis Mcha ‘Vialli', (kulia) akigombea mpira na beki wa Eritrea, katika mchezo wa Kundi C, Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge kwenye Uwanja wa Mandela, Namboole jioni hii. Timu hizo zilitoka sare ya bila kufungana


Imewekwa na MAPARA at 7:07 PM
 
hii timu yetu ya tanganyika inacheza lini?
 
Back
Top Bottom