CECAFA Kagame Cup 2012 - Live updates

Wako huko kwa bahati mbaya lakini kimsingi Yanga ni CCM, hata wakipata goli utawasikia CCM CCM CCM.....unaonaje soka la wekundu wa msimbazi
 

Kaka, siku hizi watanzania siasa za CHADEMA NA CCM zimewaharibu vichwa. Kila kitu tunagombana, yani akili zinaruka hata kama hakuna ukweli mradi tu mtu anatetea chama chake. I love CDM and YANGA as well..lakini si kweli eti SIMBA ni ya CDM. RUBBISH
 
Yanga=CCM...hivyo hata kuropoka kwenu kunafanana kabisa na mijitu ya pale bungeni....ulisema mechi hii itaenda matuta ukabeza mechi inayofata sasa mechi imeisha ndani ya dakika 90, unasemaje....

mkuu pole sana siasa imekulemaza..hata hivyo kazi unayo boko keshafanya mambo.!
 
....lazima tujute wana Simba, benchi la ufundi lazima litueleze kwa kina kulikoni....marking ya Simba si nzuri kwakweli.
 
Simba kazi wanayo.. Hawatoki leo kwa Azam naona wameshikwa vibaya yaani wamepakatwa.!
 
Simba kazi wanayo.. Hawatoki leo kwa Azam naona wameshikwa vibaya yaani wamepakatwa.!

njoo na uchambuzi wa maana, sote tunajua kwamba Azam anaongoza; ila tunaka kuujulisha umma kwamba mechi kwa ujumla hikoje, neno kupakatwa ni zuri baada ya dk 90.
 
Bado Azam 1-0 Simba dakika 30 huu ndio mwanzo wa urafiki wa Simba na Azam kuvunjika!
 
Simba hawa mie natayarisha bakora timu ikifungwa tutaonana Msimbazi!
 
Kaseja anafanya kazi kubwa sana, mabeki wanampa mtihani; hawatoi ushirikiano mzuri.
 
Nadhani Kiprecheche, Erasto Nyoni, na Boko watamchosha sana Kaseja leo...!

Ushauri wangu kwa Benchi la Ufundi la Simba - Ni makosa kumuanzisha Boban.. na gharama yake itakuwa kubwa...!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…