CCM yaunda 'ukawa' yake dhidi ya CHADEMA

CCM yaunda 'ukawa' yake dhidi ya CHADEMA

Sio wa kwanza wewe kusema hivyo. Alianza Wassira kunako 2010. Akapotea yeye kwanza.
Kipindi cha wasira ulikuwa utawala wa shamba la bibi.
Ikulu grasi ziliisha kila mkisusa mnaitwa ikulu kunywa juis mnaondoka na glasi.Utawala wa sasa hakuna ubwege kama huo.
 
Wanaosema kuwa cdm imekufa hawajui walitendalo
Mwaka 2015 CHADEMA na vyama vingine vya CUF, NCCR - Mageuzi na NLD, viliunda umoja uliojulikana kama UKAWA dhidi ya Chama cha Mapinduzi CCM kwa lengo la kuiondoa madarakani.

Mwaka huu 2020 CCM imeunda muungano wake na vyama vingine vya CUF, NCCR na TLP dhidi ya CHADEMA.

Ina maana CCM pamoja ya kuwa ina dola imeshindwa kupambana na CHADEMA peke yake hadi inaazima majeshi ya kukodi? Halafu bado kuna watu wanasema CHADEMA imekufa.


Picture speeks a thousand words.

ACT-Wazalendo wanabaki kama watazamaji au swing voters?
 
Ule mziki wa 2015 mpaka leo CCM wameingiza ubaridi hawatamani kabisa kusikia neno CDM.
Mkuu,kama sheria ingeruhusu matokeo ya uraisi kupingwa mahakamani,basi amin amin nakwambia sasa hivi tungekuwa tunaongea mengine.
Vijana waliokuwa wakimtumikia kafiri pale Masaki wanakiri kabisa ngoma ilikuwa vise versa.
 
Mkuu CCM ya sasa hata isipopiga kampeni ushindi ni 98% Kwasababu Chadema imechokwa sana na Watanzania kwa tabia zake kutumika na Mabeberu.

Ni wazi hatutakuwa na mpinzani mwenye ushawishi km Lowasa kwa miaka 50 ijayo.
Chadema bado inanguvu kubwa
 
Quinine,

CCM imeshatambua kwamba inapambana na wananchi, siyo Chama.

Nguvu na ujumbe wa vitisho ambavyo wamekuwa wakipewa CHADEMA ni ujumbe kwenda kwa wananchi kwamba hata mtumie mbinu gani hampati kitu. Ujumbe huo pia unawalenga walio ndani ya CCM kwamba mkijifanya ku side na wananchi mjue hampo salsma, sasa hivi hata Jaji Warioba, Kabudi na akina Polepole wameshaikana ile rasimu ya katiba ya wananchi ambayo kwao walishaiona kama ni misahafu.

CHADEMA inapinzwa tu na wananchi wengi waliochoka, sababu CHADEMA kama chama hawana jipya wala tofauti na NCCR, CCM na CUF, kamavwangekuwa na kitu cha tofauti kamwe wasingefanya mabadiliko ya dakika za nyongeza kwenye nafasi ya mgombea wa nafasi ya urais.

Siku zote nitaendelea kumheshimu sana Dr. Slaa kwa mikakati na nguvu aliyoitumia kuijenga CHADEMA na kupelekea wananchi kuamua kukiunga mkono, pili msimamo wake wa kusimamia anachokiamini. Tatu utiifu wake kwa mamlaka zake za uteuzi, tuliona alivyokua mtiifu na mnyenyekivu kwa Mbowe na sasa alivyo kwa Magufuli.

CHADEMA haina cha tofauti, watu ndiyo wameamua kuichagua na nguvu inayotumika ni dhidi ya watu diyo CHADEMA. Kama kuna point itainekana CHADEMA ni threat kiasi hicho basi ingefutwa kitambo tu.
Mkuu uko sahihi kwa kiasi flani.
Mm natamani tungebeti kukiingiza chama chochote cha upainzani madarakani ili kuondoa hofu ya kuwa bila chama tawala maisha hayapo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom