CCM yapasuka? Kinana ang'atuka...

kiukweli Nape anatakiwa ajitathimini mwenyewe kwanini watu wengi wanamnyooshea vidole?? mtasema ni zamu ya damu changa kuendesha cha kwa akili ipi?kimsingi ukiona hata katibu wa cha kakaa kimya kiasi hicho jua hamkani si shwari.Nape ndio kila kitu ndani ya ccm.hiyo ni hatari.ndio siasaaliyo chagua mwenyekiti wake. sasa ngoja wanachama wachachamae mtang'oka wewe na huyo jk wako
 
We Nape ulisema wanahabari wasiruhusiwe kuingia na kuandika habari ya vikao vyenu? na ukalaani juu ya baadhi ya wajumbe kuvujisha siri za vikao? Sasa na wewe unavujisha?

Basi ujue kuwa hata wale wajumbe wengine nao huwa kuna mambõ yana wakereketa na wanaamua kuja hapa JF na kuyamwaga kama ulivyofanya wewe. ili wapate amani ya roho.
 


Duh! Hii picha imeniacha hoi...ningekuwa Waziri wa Fedha nikitoka hapo nafanya kama alivyofanya Kinana!​
Huyo ni waziri wa fedha Dk William Mgwima, mkuu,ebu soma hii kitu,especially hapo kwenye bold,ina maana keshapeleka hiyo "taarifa rasmi" ya kuhusu uporaji na "pesa za uswisi" na mkulu hakufurahi?We'll soon connect the dots...
 
Mkuu hizi taarifa umezitoa wapi? Japokuwa hilo suala linawezekana likawa ni kweli maana muda wowote Magamba lazima wasambaratike ila ni vyema ukiweka chanzo cha taarifa yako ili watu wasiwe na shaka.
muda na saa aliyotuahidi MUNGU kuisambaratisha ccm ndio huu.wameanza kusambaratika mwisho chama chao kitabaki na watu wa mtwara lindi na bagamoyo tuu.hapo ndio ujue CHADEMA itachukua NCHI kiulaini.
 
Nilishawah kutabiri kuwa mwisho wa ccm ni mwaka 2012. Nafurah kuona utabiri wangu unaanza kufanya kazi.
Na mimi nilisha tabiri kuwa uchaguzi ndani ya chama chao hautawaacha salama,watafarakana mpaka mamluki wa humu jf wakose cha kuandika.
 
Mkuu mimi hata kuiangalia naiogopa manake hapo mkulu alikuwa kama zidane harufu ya kumpiga kichwa ilikuwa inakaribia.


Duh! Hii picha imeniacha hoi...ningekuwa Waziri wa Fedha nikitoka hapo nafanya kama alivyofanya Kinana!​
 
Jamaa katoa utetezi tu alafu kapotea.
Ameulizwa maswali ya msingi lakini hajajibu hata moja.
 
Ninachofahamu mimi ni kwamba, Kinana yupo katika kundi la wale wanaotaka akina EL& CO Ltd waondolewe kwenye uongozi wa juu wa chama. Tofauti ya Kinana na watu kama akina Sitta ni majukwaa ya kauli zao. Kinana amekuwa akitumia vikao halali vya chama wakati akina Sitta hata ukiwaalika kufungua shule ya chekechea; watatoa msimamo wao huko!

Sina shaka kwamba msimamo wa Kinana na Nape unawiana ingawaje tofauti yao ni ile ile iliyopo kati ya Kinana na Sitta! Jambo ambalo nashindwa kuanganisha dots ni tofaut kati ya Kinana na Nape ingawaje nahisi wanatofautiana katika namna ya uwasilishaji hoja.....tusisahau, Kinana ni kizazi kilichotokana na zama za chama kufuata maadili(usiniulize wht abt Sitta) so lazima awe anakerwa na staili za uendeshaji chama za akina Nape!! Hilo moja!

Lakini vilevile naamini Kinana alitarajia uchaguzi huu wa ndani wa CCM ungekuwa ndio mwisho wa akina EL.....sina shaka ameona ndoto zake zinaelekea kupeperuka kwa kuona nguvu ya akina EL inavyopasua anga za uchaguzi huo. Si ajabu KInana ameona harakati za wazi wazi za kuhakikisha akina EL wanabaki na kuchukua nafasi za juu kwenye chama!! Hapa kuna vita, kati akina Lowassa pamoja na Kinana.

Tusisahau miezi michache iliyopita tulijuzwa ufisadi wa Kinana humu jamvini.....nahisi huo ulikuwa ndio mwanzo wa vita hii!! Mwanzo wa kumtia adabu ili aache kuwasakama akina Lowassa!
 

Nyumba ya tembe ina nguzo kuu ndugu yangu japo fito nazo huchukua uzito lakini mkaazi wa tembeni huwa roho juu pale nguzo inapoguswa na mchwa kuliko kuliwa kwa fito

Sio jambo la kupewa wepesi kama unavyoshauri
 
Majibu ya Nape hayana tofauti na ya mwenyekiti wake ya kusema kuna watu wana viwanda vya uongo!
 
kuna jambo sijalielewa Kwani alichukuwa fomu ya kugombea au hakuchukua kabisa

msaada tafadhari
 
CCM kuna gharika kubwa liko njiani kwa hisani ya KUCHAKACHUA WENYEWE KWA WENYEWE kulinda zile koo maalumu kuendelea kuongoza kama kawaida.
 
HIVU KUBAINI YA KUA SIASA ZA CCM NI UCHWARA KUNAHITAJI KUUMIZA KICHWA?!!!!!!!!!!!!:frusty::rockon:
Asilani, haihitaji kuumiza kichwa kichwa! Hata hivyo, unavyokutana na msamiati kama huo ndani ya CCM basi unapaswa kuwa makini sana....! Hakuna tafsiri inayosimama peke yake kuhusu "Siasa Uchwara" ndani ya CCM! Unajua ninachomaanisha? Hata yule fisadi namba moja ndani ya nchi hii akitokea CCM kisha akachinjiwa baharini kwenye vikao vya chama, huyo nae atasema hizo ni "siasa uchwara!" Refer RA's Statement! RA nae alisema anaachana na "siasa uchwara." Leo Chenge akichinjiwa baharini, nae atasema Siasa Uchwara! Tatizo nionalo mimi ni kufahamu nani mwenye dhamira chanya ndani ya CCM na nani mwenye dhamira hasi! Laiti Mr. X tuseme ni mzalendo kweli kweli na mpinga ufisadi na Mr. Y ni kinyume cha Mr. X; then hapo endapo ukimsikia Mr. X anazungumzia siasa uchwara basi ungeweza kufahamu anamaanisha nini, na Mr. Y akitumia msamiati huo huo nae ungefahamu anachomaanisha! Kwa CCM ni ngumu kidogo kufahamu kwa yakini siasa uchwara inayozungumziwa hapo.....labda neno sahihi kidogo kwao lingekuwa kuachana na "siasa isiyo na maslahi binafsi"
 
Ile kashfa yake ya kufoji malipo ya ndege(Risiti feki) waliokuwa wanatumia kipindi cha kampeni iliishia wapi?:A S 39:
 
Mwacheni Msomali wa watu aachene na Siasa Uchwara! Kwanza akili yake imeshaanza kupata gia ya reverse kama ya Kingunge, badala ya kwenda mbele anarudi nyuma! Hawezi kushindana na wanasiasa uchwara kama akina Nnauye Jr na Mwigulu LM Nchemba.
 
Last edited by a moderator:
Siasa uchwara za CCM ndio sababu ya wengi kuachana na uongozi ndani ya CCM maana zinambegu ya ubaguzi mbaya sana.

Maana ukihoji tu au kupingana na wakubwa basi utasikia wewe sio raia wa Tanzania.

Alianza Generali ulimwengu(Mnyarwanda?), kisha Rostam Azizi(Mhindi?), sasa Abrahaman Kinana(Msomali?), atafuata Hussein Bashe(Msomali?), mwisho Salim Mohamed Salim(Mwarabu?)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…