CCM yanguruma Busanda; Wapinzani chali!

CCM yanguruma Busanda; Wapinzani chali!

Matokea ya uchaguzi jimbo la Busanda, yameanza kutoka ambako katika miji mikuu yote ya jimbo hilo, ni Chadcema inaongoza na kuiacha CCM kwa mbali wakati huko vijijini ni CCM inaongoza.

Shamra shamra za kusherehekea ushindi ni mijini kwa kuwafanya wafuasi na washabi wa Chadema kufurika mitaani kusherehekea ushindi hali inayoashiria wakijaambia matokeo ya jumla sio wao, mijini kutakuwa hapatoshi na hakukaliki.

Mpaka sasa Mji mkuu wa Busanda ni Chadema wakati kata maarufu ya Nyarugusu ni CCM.

Nitawaletea matokeo ya kata kwa kata kadri ninavyoyapata.

Ahsante sana, nina wasiwasi uhesabuji kura CCM wanaweza kuamua uahirishwe hadi kesho ili wafanye madhambi yao. CHADEMA ikishinda basi ni dalili nzuri sana kwa vyama vya upinzani 2010 hasa katika kuongeza idadi ya Wabunge wao.
 
Mpaka ssa kura zilizohesabiwa ni asilima 12,ktk hizo asilimia kimi na mbili ccm ina asilimia 53 na chadema asilimia 44.tofauti ni kura elfu saba
 
Tatizo ni kuwa Busanda hakuna umeme hivyo mawasiliano kuwa magumu na pande zote. Dr. Slaa hapatikani, Zitto anapatikana lakini hapokei, Mnyika hapatikani, Mbowe hapatikani na CCM wanapatikana... Nimepata kuongea na mwenyekiti wa CCM mkoa anasema wana uhakika wa ushindi.

Najaribu kumtafuta Zitto tena

Mkuu maji mazito, serikali haiwezi kuhamia Busanda kwenda kupata aibu. Tusubiri tamko lao, huenda wanakusanya dataz. Ila kama namba zao ni Public huenda kuna namna tusubiri.
 
Ni ngumu kujua data zote lakini mpaka sasa wakati wanaendelea kuhesabu chadema inaongoza kata mbili tu za katoro na kata anayotokea mgombea wa chedema....jumla ni kuwa ccm ina kura elfu kumi mpaka sasa na chadema wako elfu saba na mia sita

Kaka wakati CCM wanashangilia kuepuka na ushindi wa CHADEMA leo ambao ungeleta matatizo makubwa kwao 2010 ni lazima wa/mkumbuke kuwa mwaka 2005 CHADEMA walipata asilimia 3% za kura huko.

Ni kawaida vijijini kushindwa kuamini mabadiliko kwa haraka sana lakini ni wazi kuwa kuna mabadiliko makubwa ya kifikira yanayoendelea miongoni mwa watanzania.....

CHADEMA, wawe wameshinda ama wameshindwa wakitoka huko hakuna kurudi Dar, break iwe Biharamulo kuendelea na operesheni sangara ama operesheni ondoa ukiritimba wa CCM....

omarilyas
 
Kaka wakati CCM wanashangilia kuepuka na ushindi wa CHADEMA leo ambao ungeleta matatizo makubwa kwao 2010 ni lazima wa/mkumbuke kuwa mwaka 2005 CHADEMA walipata asilimia 3% za kura huko.

Ni kawaida vijijini kushindwa kuamini mabadiliko kwa haraka sana lakini ni wazi kuwa kuna mabadiliko makubwa ya kifikira yanayoendelea miongoni mwa watanzania.....

CHADEMA, wawe wameshinda ama wameshindwa wakitoka huko hakuna kurudi Dar, break iwe Biharamulo kuendelea na operesheni sangara ama operesheni ondoa ukiritimba wa CCM....

omarilyas
Kumbe Omary wewe CHADEMA...nilijua kuwa huna chama. Kwa nini ulikuwa unamsaidia salim kushinda CCM 2005 na huo ubunge wa Moro mjini utaenda na u-CHADEMA wako?
 
Kitu muhimu kujua ni kwamba wagombea wote na wapambe wao wana matokeo yote mpaka sasa,
Angalizo. Naomba tusije kuiga kale ka-utamaduni ka kuvuka bahari... Yeyote akishindwa ampongeze mwenzake tuende mbele.
 
Tatizo ni kuwa Busanda hakuna umeme hivyo mawasiliano kuwa magumu na pande zote... CCM wanapatikana...

Zitto anapatikana lakini hapokei...

Kama hapokei maana yake hapatikani.

Na kama "pande zote" hazipatikani, basi na CCM wasingepatikana.

Na kama CCM wanapatikana ina maana tatizo sio umeme...
 
Tatizo ni kuwa Busanda hakuna umeme hivyo mawasiliano kuwa magumu na pande zote. Dr. Slaa hapatikani, Zitto anapatikana lakini hapokei, Mnyika hapatikani, Mbowe hapatikani na CCM wanapatikana... Nimepata kuongea na mwenyekiti wa CCM mkoa anasema wana uhakika wa ushindi.

Najaribu kumtafuta Zitto tena
Hawapatikani kwa kuwa mambo ni magumu kaka hilo mbona ni rahisa sana kulijua...Kaka ndio siasa za ushindani...ila zitto anajibu meseji ukimwandikia
 
Hatukati tamaa kamwe hata Obama alipoteza uchaguzi alipogombea useneta kwa mara ya kwanza hakuna shida raha ni kua ujumbe sasa unaanza kuwafikia watu! hilo ndio suala muhimu! haijalishi ni lini mabadiliko haya yatakuja...! we will wait as long as it take!
 
Leo ni knock out tu...Chadema huko mikoani, na CUF huko visiwani.

=======

Wizi mtupu nao unashangiliwa! Wengi tulijua kuwa kuhamishia serikali yote Busanda ni dalili kuandaa mazingira ya wizi. Mawaziri wazima wananunua shahada za kupigia kura!

Good newz: Kwa ushindi wa CCM, Makamba, Msekwa, Lowassa, RA na wapambe wao, hawana lao tena ndani ya CCM na wakiwa na lao, basi Mkuchika, Malecela na timu yao iliyo Busanda, nao hawatakuwa na lao ndani ya CCM. Ni kugawana viti na meza tu.
 
Sasa jamani kina Invisible, Mkjj na wengine mnapoleta hizi data tafadhalini muongeze na analysis kidogo ili tujue kinachoendelea.

Mfano, CCM Rwamgasa wamepate zaidi 600, JE ilitegemewa waongoze au?? Je hiyo Rwamgasa ni kata au nini na je inawatu wengi sana?? Chadema walitazamia kushinda hapo nk

Ahsanteni sababu kabla ya kuhamia kwenye issue ya KING James usiku itakuwa vizuri kama chadema wameshinda wengine tupate moja baridi moja moto mapema.
 
=======

Wizi mtupu nao unashangiliwa! Wengi tulijua kuwa kuhamishia serikali yote Busanda ni dalili kuandaa mazingira ya wizi. Mawaziri wazima wananunua shahada za kupigia kura!
Kama mlijua hilo before, hatua gani mlichukua? Mtalia sana safari hii!
Mimi wacha nijiandae na kusheherekea ushindi double Visiwani na Bara!
 
Matokeo ya awali Busanda jumla ya vituo ni 380 na matokeo tayari vituo 253 namatokeo yake ni kama ifuatavyo ccm 19,190
chadema 14.024
cuf 372
udp 143 Mungu yupo pamoja nasi
 
Last edited:
Back
Top Bottom