CCM wameanza kuisoma namba kabla ya UKAWA

CCM wameanza kuisoma namba kabla ya UKAWA

Akumbuke na kumuadabisha aliyeiua Kiwira Coal Mines

sio aliyeua... ni ALIYEJIUZIA...na ni yule aliyekuwa akijikomba kwake kwa kumpigia kampeni majukwaani akichelewa kuadabishwa pindi makufuli akiingia madarakani. pamoja na hayo yote, lazima kibano kimkute.
 
wananchi wamechagua magufuli kuleta mabadiliko ya kweli sio geresha ya CCM-B/ukawa. sijui wewe unachekelea nini. CCM-A ni mbele kwa mbele wanaosoma namba ni CCM-B/ukawa. magufuli=mabadiliko ya kweli.

mkuu, kumbuka hapa sio facebook. unapoandika maoni kwenye jukwaa nyeti kama jf unapaswa kushirikisha akili ipasavyo.
 
msiwe na papara,,mnasahau mapema sana watanzania,,,,utasemaje mtu mtendaji wakati hajachagua hata PM mtendaji wake mkuu wa mambo ya serikalini?,,hajachaguliwa spika msaidizi wa kupitisha sharia atakazotumia kufanikisha ahadi zake.....baraza la mawaziri litakalomsaidia kufanya kizii,,,raisi hupimwa kwa siku 100,,,,,viongoz wenu wanajua akuwashika kweli kweli
 
Sie ndo tulitaka hivyo
Napenda akifyeka kabisa ni viti maalum pamoja na ruzuku kwa vyama. Lazima namba wataisoma tu, waliokuwa wazembe na wezi

Hata mimi hakuna kinachonikela kama madiwani na wabunge wa viti maalum. Wa nini hao!!!!!!!
 
Nyie tumeshawasomesha namba kwa kumuweka mamvi nje. Sasa tunaanza kazi. Hiyo ndio maana yake. Tulieni boriti liingie huko tunduni

Hivi ukisoma ulichoandika kama binadamu mwenye akili timamu unajisikiaje..
 
Hivi kusema kitufe cha kulike nimekikosa ni fashion ushamba? maana kama unatumia. browser other than app ya jamiiforums huwezi kukiona naona imeshakua wimbo wa Haifa sasa....ingawa Sijajua kwenye topic thoo.....

wewe uliyeandika haya ndiye unaonekana mshamba. ukikuwa utaelewa maana yake.
 
Aanze na wabunge wanao tetea chama badala ya wananchi na kuitikia ndiyoooooooo bila kujua hoja gani imetolewa na wanao lala bungeni

magufuli atakuwa sio mtu wa kusaini kila ujinga unaopitishwa bungeni kwa staili ya ndioooooo!
 
Watu mtaani et"sisi hatuna rais"hebu nyie mnaowasiliana naye mwambieni mishahara ya walimu na askari ni midogo hapa tz.

Mishahara ya askari ni mikubwa kwa sababu wanapiga wapinzani wanaoipinga CCM.
 
Waliokuwa wanadhani ni UKAWA pekee wataisoma namba walikuwa wanaota,

Magufuli bado anaendelea kufagia nyumba yake mliozoea kula vya kunyonga sasa mtaisoma, hakuna cha vimemo na bado.

Sioni shida zaidi ya kujisikia Raha pale Magufuli anapotenda kwa kutumia Ilani ya UKAWA.

Kifupi wanaUKAWA tunaweza kujikuta huyu mtu anafanaan na sisi kuliko maCCM yenyewe, na pengine akizidiwa huwa nachukua ushahuri kwa MAMVI kuliko MACCM wenzie.
 
Sioni shida zaidi ya kujisikia Raha pale Magufuli anapotenda kwa kutumia Ilani ya UKAWA.

Kifupi wanaUKAWA tunaweza kujikuta huyu mtu anafanaan na sisi kuliko maCCM yenyewe, na pengine akizidiwa huwa nachukua ushahuri kwa MAMVI kuliko MACCM wenzie.
Binafsi nafurahi kuona tuliyokuwa tunadai yakitekelezwa haijalishi yanatekelezwa na nani.

WanaCCM walidhani Magufuli atakuwa rais wao pekee yao.
 
Anatekeleza Sera za ukawa CCM haina Sera ya kufuta safari za nje Na mabalozi kuwajibika
 
safari za nje zimesitishwa watoto na ndugu za wanufaika ambao ni wana ccm wanalia,

rweyemamu ameambiwa afungashe virago ikulu atakuwa anaiona ikulu kwenye tv ameanza kuisoma,

ruge tenda za matamasha ya ikulu zimeyeyuka alikuwa anaingia ikulu kama choo cha stand sasa ameanza kuisoma,

posho za wabunge nje ya vikao zimefyekwa wataisoma,

reshuffle la madc linakuja...humo mwote hakuna ukawa hata mmoja wataisoma,

hadi sasa wanaccm ndio walioanza kulia hata kabla ya ukawa.

Waliokuwa wanadhani ni ukawa pekee wataisoma namba walikuwa wanaota,

magufuli bado anaendelea kufagia nyumba yake mliozoea kula vya kunyonga sasa mtaisoma, hakuna cha vimemo na bado.

kulialia bungeni mwiko maanamano hola mtaisoma namba
 
kulialia bungeni mwiko maanamano hola mtaisoma namba
Mtaelewa tu wepi wanaoisoma namba,

bodi ya hospitali ya Muhimbili imevunjwa na mkurugenzi wake kusimamishwa hawa walikuwa UKAWA Hahahaaa.... na bado, waambie TANESCO waliokuwa wanahujumu kwa kufungulia maji usiku wajiandae kunyolewa baada ya hapo anaelekea Bandari kaambiwa kuna UKAWA wengi kule, tutaheshimiana tu.


Rais Dk.Magufuli amefuta bodi ya afya Muhimbili na kumsimamisha kazi mkurugenzi mkuu wa Hospitali hiyo leo.
 
Sioni shida zaidi ya kujisikia Raha pale Magufuli anapotenda kwa kutumia Ilani ya UKAWA.

Kifupi wanaUKAWA tunaweza kujikuta huyu mtu anafanaan na sisi kuliko maCCM yenyewe, na pengine akizidiwa huwa nachukua ushahuri kwa MAMVI kuliko MACCM wenzie.

Unakosea sana kumfananisha Magufuli na ukawa, Sidhani kama Magufuli anaweza kusimama mbele ya TV na kuwasafisha mafisadi kama UKAWA!
 
Unakosea sana kumfananisha Magufuli na ukawa, Sidhani kama Magufuli anaweza kusimama mbele ya TV na kuwasafisha mafisadi kama UKAWA!

Vp inaelekea unamjua sana Rais wetu. Ile mahakama ya mafisadi ameshaanza kuijenga???nadhani ulikuwa priority no.1.....tunaisubiri kwa hamu huku kwetu
 
Mtaelewa tu wepi wanaoisoma namba,

bodi ya hospitali ya Muhimbili imevunjwa na mkurugenzi wake kusimamishwa hawa walikuwa UKAWA Hahahaaa.... na bado, waambie TANESCO waliokuwa wanahujumu kwa kufungulia maji usiku wajiandae kunyolewa baada ya hapo anaelekea Bandari kaambiwa kuna UKAWA wengi kule, tutaheshimiana tu.

Nikupe angalizo tu...Rais ni watu wote na sio wa chama.Na sidhan kama yupo kwa hilo lengo unalolisema hapo juu..Epuka sana uchochezi,kila mtu atawajibika kwa nafasi yake kama ni Mtumishi wa serikali hii haijalishi ana itikadi ipi.ila usitamke kitu ambacho hujakisikia kutoka kwake coz kinaweza kukuletea madhara.kumbuka kuna watu wana Tabia ya kucopy vitu huku na kuanza kuvisambaza
 
Atathubutu kugusa magendo ya RIDHIWAK KIKWETE? Je lile "tundu" la iliyokuwa Home shopping Centre? Wale washenzi hawakuwa wakilipa kodi tangu wafungue kampuni..
 
Back
Top Bottom