CCM tuna hali mbaya sana, inasikitisha kweli!

CCM tuna hali mbaya sana, inasikitisha kweli!

Angekuwa makini Mwakyembe, nchemba, Nape, Muhongo wasingeteuliwa kuwa mawaziri

Wasingeteuliwa kwa sababu UKAWA wanawaogopa?subirini Lowassa awe Rais ndio mchague watu wasio na madhara kwa UKAWA.
 
Kuna watu makini sana ambao anawashawishi , but he is taking his own time to ensure that he has cleaned the entire sector's before he hands over.
 
Mmmh! Kingunge? Ndo role model wako kwenye Siasa?. Malowassa yamebakibaki sana CCM. Screening ya kutosha inatakiwa kabla mtu hajateuliwa nafasi muhimu. Ukiwa na kiu siyo busara kunywa kila maji!!
 
Kauli ya mkongwe wa siasa Kingunge Ngombale Mwiru kuwa CCM imeishiwa pumzi ya kuendelea kutawala, sasa ndiyo inajidhihirisha ukweli wake.
Hivi inawezekanaje chama kinachotamba kuwa kina wanachama 6m plus nchi nzima halafu leo Rais Magufuli ashindwe kupick katika Umati huo, kupata 4 tu ambao ni qualified wa kuziba nafasi hizo za baraza la mawaziri ambazo hadi sasa zinaendelea kubakia vacant??!!!!

Siyo kwamba kashindwa anachokifanya ni kuwa makini ili asifanye makosa si kwamba watu hawapo na unapokuwa hapo hafanyikazi yeye peke bali anafanya na vyombo vya usalama.
 
Maji marefu darasa la nne, Deo Sanga la pili, Musukuma la saba, Jumanne Kishimba la saba, Njalu Silanga la nne sasa unategemea rais apate wapi mawaziri kama nyie CCM mlikataa wazo la Warioba kuwa mbunge walau aanze na digrii moja

mbowe la kwanza, sugu kindegateni, lema hajapiga skonga kabisa. ndio maana ukawa ni kutukana tu.
 
Mm niliwaza hvyo pia lkn kuna mda nikajipa jibu kuwa au anasubiri watu wa Zanzibar wafanye uchaguzi ndio awape uwaziri lkn bado na sita kidogo hapo.
Mfumo ungeruhusu angechagua nje ya chama chake but haiwezekani.

Labda asubiri wa Msumbiji! Kwani Dr Makame Mbarawa na Husein Mwinyi wanatoka wapi?
 
Tatizo ccm walisomesha watu ili waibe kwaiyo wasomi wote ccm ni wezi na ambao hawajasoma kama akina Sanga, lakairo, maji marefu, msukuma etc. ndio wanatumika kuficha mali walizoiba akina Chenge, Tibaijuka etc. Kwaiyo wote ni ukoo wa panya hata ukiangalia walioteuliwa ni Kama kaokoteza baada ya shinikizo la cc/NEC mfano muhongo wa escrow na mwigulu wa TRA na mwakyembe wa TPA/TRL.
 
upo sawasawa mkuu hili ni tatizo kwa ccm

Tukiweka ushabiki pembeni hili swala ni tatizo kwenye Chama rais kakidharau sana Chama na anajenga upinzani kwenye Chama dhidi ya serikali anayoiongoza.
 
Mwezi mzima TISS wameshindwa kumsaidia Rais kufanya upembuzi wa watu 277+, halafu kuna watu wanataka kuwapa sifa kwamba kidunia wanaongoza!!
Hao tiss naamini wamechangia
Sana kuifikisha nchi ilipo sasa.ni kun di la vilaza fulani hivi wasiojua majukumu yao.hawaaminiki
 
Kwanza nianze kwa kusema, nimesikitishwa na kukosekana kwa watu makini wa kujaza nafasi sita zilizobaki kwenye wizara muhimu katika baraza hili la mawaziri.

Nina amini kabisa hata wengine wanaweza kukubaliana na mimi kwamba Raisi Magufuli ni mtu makini kwenye kazi yake na kutopitishwa kwa watu kama Membe, Nyalandu, Asha Migiro, Tibaijuka, Chenge, Kagasheki ni kuonyesha kwamba kwa kiasi kikubwa ufanisi na 'makandokando' hayana nafasi kwenye serikali ya JPM.

Ila pia kurudi kwa watu kama Makamba na Muhongo ni kudhihirisha sio kila anayelaumiwa na kusemwa, "hafai", na ukweli daima usimama baadaye.

MSHITUKO mkubwa niliopata ni hasa kuhusiana na kukosekana kwa watu KAMILI 34 kwenye baraza la mawaziri hasa kwenye wizara muhimu sana ILHALI ccm tuna wabunge 277+... Mimi nimesikitika sana kwamba wana ccm hasa wateuliwa hawana uzoefu au weledi wa kujumlishwa kwenye kuongoza taifa to the extend that Raisi ilibidi atoke nje ya wabunge wa ccm wateule kwenda kutafuta walioko nje ili waje kujazia.

Kwa kipindi kirefu niliamini kwamba walioweka CCM dosari ni watu wachache wasiozidi 20 (hasa wale waliokuwa kwenye uongozi hivi karibuni), sikujua tatizo ni kubwa sana kiasi hiki kama alivyotuonyesha Raisi Magufuli.

Watu wote 277+ hata wale wasiofahamika hawafai? Hali ni mbaya ndani ya CCM.

SIKUJUA KAMA HALI NI MBAYA KIASI HIKI.

Ww hujui uongozi. Huelewi tu. Kuchagua watu nje ya wabunge ni halali kikatiba lakini pia ni faida kwa chama. Ili chama kuweza kupata support hata kwa watu walio nje ya system. Ni njia mojawapo ya kujenga chama. Hujui uongozi. Uwezo wako wa kuelewa mambo ya uongozi mkubwa wa nchi. Tena wa kisiasa kama huu ambapo lazima kazi zako zijenge chama chako.
 
Mleta mada falsafa ya Magufuli imekupita kimo kuielewa kwanini anafanya hivyo
For your information anao tayari ni swala la kuwataja tu ila anacheza na saikolojia kuwandaa kwamba nafasi hizo sio za kuchezea

Simple logic huwezi kuchagua wanafunzi wazuri kwanza katika walio bora halafu waliobaki ndio uchague wazuri zaidi
 
Hapa tunapata picha halisi ni kwa jinsi gani endapo kama baraza lingekuwa na wizara nyingi kama lilopita lingelikuwa na mawaziri mizigo tena isiyofaa kutua...
 
Tupo hapa tulipo kama taifa kwa sababu ya kuendekeza upuuzi huu wa vyama badala ya kutazama maslahi mapana ya taifa. Rais Magufuri teua watu wenye sifa bila kufungwa mikono na chama chake, maana nchi hii ni yetu sote.
 
Hao tiss naamini wamechangia
Sana kuifikisha nchi ilipo sasa.ni kun di la vilaza fulani hivi wasiojua majukumu yao.hawaaminiki

TISS ni wazuri, ila boss ndio kila kitu. Na ndio mana tunaona ripoti ya mambo ya TRA kutochukuliwa hatua awamu iliyopita.
 
Hapa tunapata picha halisi ni kwa jinsi gani endapo kama baraza lingekuwa na wizara nyingi kama lilopita lingelikuwa na mawaziri mizigo tena isiyofaa kutua...

Hata hii subiri subiri ya sasa, ni kama JPM amekosa pa kuangalia. Na kuwaweka kipolo ndio inazua maswali zaidi juu ya taswira za watu watakao jazwa hapo baadaye.
 
Mleta mada falsafa ya Magufuli imekupita kimo kuielewa kwanini anafanya hivyo
For your information anao tayari ni swala la kuwataja tu ila anacheza na saikolojia kuwandaa kwamba nafasi hizo sio za kuchezea

Simple logic huwezi kuchagua wanafunzi wazuri kwanza katika walio bora halafu waliobaki ndio uchague wazuri zaidi

Hayo maneno ya kwako au ya Magufuli!?so walochaguliwa hizo nafas ndo za kuchezewa?mdau wewe veeepeeee???
 
Back
Top Bottom