Mchambuzi
JF-Expert Member
- Aug 24, 2007
- 4,850
- 9,405
Ndugu wanajamvi,
Katika hotuba yake ndani ya Bunge la Katiba mjini Dodoma hivi karibuni, Rais Kikwete, pamoja na mengineyo, alinukuliwa akisema kwamba muungano wa serikali tatu uliopendekezwa katika rasimu ya katiba haufai kwa kuwa ni mfumo legevu na utawaongezea wananchi mzigo. Rais Kikwete pia alienda mbali na kueleza kwamba:
Hapa Rais Kikwete alikuwa akimaanisha mfumo wa serikali mbili ambao CCM imesema itauboresha, kama njia ya kuondoa kero za muungano zilizodumu kwa zaidi ya miaka 30. Kufuatia hotuba hii ya Rais Bungeni, huu ukawa ndio msingi wa hoja za kile kilichoitwa Maoni Ya Wengi ndani ya bunge maalum la Katiba. Na ni msimamo huu wa Maoni ya Wengi ambao pia ukapelekea upande mwingine wa hoja, ulioitwa Maoni ya Wachache, hatimaye kuamua kujiondoa katika bunge hili, chini ya mwamvuli wa UKAWA kwa nia ya kwenda kuwaeleza wananchi jinsi gani waliojiita wengi bungeni walivyoamua kupuuza maoni ya wananchi kuhusiana na rasimu ya katiba.
Kama tutakavyojadili, Muungano wa Serikali Mbili Zilzoboreshwa, kama unavyopigiwa kampeni na CCM, hautaimarisha Muungano na hautamaliza malalamiko, lawama na shutuma za kero za Muungano. Badala yake, Serikali mbili zilizoboreshwa, zitavunja na kuuzika Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Mjadala wetu umegawanyika katika sehemu kuu tatu.
Sehemu ya kwanza tutajadili:
· Muundo Wa Serikali.
· Madaraka ya Viongozi.
· Muundo Wa Bunge.
Hapa tutaonyesha jinsi gani masuala haya chini ya mfumo wa serikali mbili zilizoboreshwa yataenda kuvunja muungano.
Sehemu ya pili tutajadili:
· Mapato na Matumizi Ya Kuendesha Muungano.
· Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Kimataifa, Mikopo, na Misaada.
· Mapendekezo ya Baraza la Mapinduzi kuhusu masuala ya kuyaondoa katika Orodha ya mambo ya Muungano.
Vile vile, tutaonyesha jinsi gani masuala haya chini ya mfumo wa serikali mbili zilizoboreshwa yataishia kuvunja muungano.
Na Sehemu ya TATU tutajadili:
· Sheria Za Ndani na Nje ya Muungano.
· Mgongano wa Kikatiba.
· Kuzinduka kwa Utaifa kwa pande zote mbili za Muungano (Tanganyika na Zanzibar). Muungano.
Hapa pia tutaonyesha jinsi gani masuala haya chini ya mfumo wa serikali mbili zilizoboreshwa yataenda kuvunja muungano.
SEHEMU YA KWANZA
MUUNDO WA SERIKALI, MADARAKA YA VIONGOZI NA MUUNDO WA BUNGE
Katika hotuba yake bungeni, Rais Kikwete aliwahimiza wajumbe wa Bunge la Katiba juu ya umuhimu wa kuwaenzi Waasisi wa Muungano (Mwalimu Nyerere na Sheikh Karume), kwa vile wao walitaka na walituachia mfumo wa serikali mbili. Wanaojiita Maoni Ya Walio Wengi Bungeni, ambao wanapigia chepuo mfumo wa serikali mbili zilizoboreshwa wanafahamu kwamba muundo wa muungano ulioachwa na waasisi wetu ulikuwa ni muungano wa NCHI MOJA, yenye SERIKALI MBILI. Zanzibar ilikuwa ni SEHEMU YA JAMHURI YA MUUNGANO. Hiyo ndio hali ya Muungano ambayo Mwalimu Nyerere alipofariki kumi na tano iliyopita. Leo hii Zanzibar sio tu kwamba tayari imeshaondoa mambo mengi ya msingi juu ya muungano, bali pia, kwa mujibu wa marekebisho ya kumi ya Katiba (2010), Zanzibar haitambuliwi tena kama ni sehemu ya muungano, bali inatambulika (Kikatiba) kama nchi kamili, yenye bendera yake, wimbo wake wa taifa, na amiri jeshi mkuu.
Pamoja na Muungano sasa kuwa na Nchi MBILI, SERIKALI MBILI, CCM bado inasema kwamba serikali mbili hizi zitaziboreshwa, huku chama kikipendekeza kwamba katika katiba ijayo, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano (ambae leo hii ni Dr. Bilal), anyanganywe mamlaka aliyokuwa nayo ya kuwa msaidizi mkuu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano, na badala yake, mamlaka hayo yahamie kwa Rais wa nchi jirani ya Zanzibar. Kwa maana nyingine, chini ya serikali mbili zilizoboreshwa na CCM, Rais wa nchi jirani ya Zanzibar atakuwa ndiye msaidizi mkuu wa Rais wa Muungano kwa masuala ya Zanzibar, lakini pia atakuwa ni mmoja wa viongozi wakuu wa nchi (Tanzania). CCM haisemi lolote kuhusu kiongozi atakayekuwa msaidizi wa Rais wa Muungano katika masuala ya Tanganyika (ukipenda, sema - Tanzania Bara).
Mkataba wa Muungano (1964) uliweka utaratibu ambao Rais wa Muungano wa NCHI Moja, alikuwa na wasaidi wake wakuu wawili Makamu wa Kwanza wa Rais ambaye alikuwa anawajibika na masuala yote yasiyo ya muungano kwa upande wa Zanzibar (Marehemu Karume), na Makamu wa Pili wa Rais ambaye alikuwa anawajibika na masuala yote yasiyo ya muungano kwa upande wa Tanganyika (Marehemu Kawawa).
Chini ya Katiba Mpya, CCM inapendekeza kwamba Rais wa Zanzibar afanywe kuwa Makamu wa Rais wa Muungano bila ya kujalisha Rais wa Muungano anatokea upande upi wa Muungano. Kwa kufanya hivyo, CCM inadai kwamba hali hii itamwongezea Rais wa Zanzibar - madaraka na hadhi ndani ya serikali ya Muungano na pia nje ya nchi.
MGOGORO UTAKAOJITOKEZA KUTOKANA NA MAPENDEKEZO YA RAIS WA ZANZIBAR KUWA MAKAMU WA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO
Chini ya mfumo huu wa serikali mbili zilizoboreshwa, CCM haisemi iwapo Rais ni mmoja - yaani Rais wa Jamhuri ya Muungano, ni kiongozi gani ndiye atakayesimamia Mawaziri watakaokuwa wanasimamia mambo ya Tanzania Bara katika mfumo huu wa serikali mbili ulioboreshwa. Pamoja na kuendelea kupigia debe serikali mbili zitakazoboreshwa, CCM bado imeendelea kukaa kimya juu ya ufafanuzi wa masuala muhimu (kiutekelezaji), kwa mfano, - katika mazingira ya Zanzibar kuwa ni nchi kamili, yenye mamlaka kamili, ikitokea kwamba Rais wa Muungano anatokea upande wa pili wa muungano (Zanzibar), JE:
· Rais huyu kutoka nchi jirani ya Zanzibar atasimamia masuala yasiyo ya muungano - ya upande unaoitwa Tanzania Bara, ndani ya Jamhuri ya Muungano, kwa mamlaka yepi?
· Iwapo Rais wa Muungano atatokea panapoitwa Tanzania Bara, Rais huyu wa Muungano atakuwa na mamlaka yepi ya kusimamia mambo ya Tanzania Bara wakati yeye atakuwa amechaguliwa na wananchi wa pande zote mbili za muungano?
· Zipo wapi pande mbili za muungano bila ya kuwepo kwa Serikali ya Tanganyika?
CCM haina muda wa kutoa majibu kwa maswali haya muhimu. Kutokana na hali hii, serikali mbili zilizoboreshwa, hazitaboresha muungano bali zitajenga mazingira ya kuvunja muungano. Hii ni kwa sababu:
Tuseme Rais wa Muungano anatokea upande wa nchi jirani ya Zanzibar, ambaye chini ya mfumo wa serikali mbili ambao CCM inadai utakuwa umeboreshwa, Rais wa Zanzibar pia atakuwa ni Makamu wa Rais wa Muungano. CCM inapendekeza kuwa iwe hivyo bila ya kujali Rais wa Muungano atatokea upande upi wa Muungano. Kitakachotokea ni kwamba - siku moja, Rais wa Muungano na Makamu Wa Rais Wa Muungano, wote watakuwa wametokea nchi jirani ya Zanzibar. Kwa maana hii, inachokifanya CCM, aidha kwa makusudi au bahati mbaya, CCM inaweka mazingira ambayo Zanzibar hawataweza tena kutoa Rais wa Muungano. Hii ni kwa sababu:
Kama tulivyoona, chini ya serikali mbili zilizoboreshwa na CCM, Rais wa Zanzibar automatically, atakuwa pia ni Makamu wa Rais wa Muungano. CCM ikimsimamisha mgombea Urais wa Muungano kutokea nchi jirani ya Zanzibar, nchi ambayo pia automatically itatoa makamu wa Rais wa Muungano, chini ya mazingira ya sasa ya mfumo wa vyama vingi vya siasa nchini, wapiga kura kutoka upande wa inayoitwa Tanzania Bara, upande ambao una wapiga kura zaidi ya 90% ya wapiga kura wote wa Jamhuri ya Muungano, wengi ya wapiga kura hawa kutoka Tanzania Bara, hawatakubali kumchagua mgombea wa urais (CCM) kutokea nchi ya Zanzibar huku wakijua kwamba makamu wake pia anatokea huko huko nchini Zanzibar. Madhara yake ni yepi?
Ni kwamba chini ya mfumo wa Serikali mbili zilizoboreshwa na CCM, Zanzibar ianze kusahau kutoa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kitachofuatia ni Zanzibar kuanza kulalamika kwamba wanabaguliwa, wanonewa, wananyimwa haki ndani ya Jamhuri ya muungano, kwahiyo waachwe Wapumue. And interestingly enough, watakaongoza katika kutoa hoja hizi ni wale wale wazanzibari ambao Islaml Jusa alisema kwamba walipofika Dodoma Waliufyata. Ni wale wale ambao leo wanapinga kwamba wao sio wasaka tonge. Katika kundi hili, hatutashangaa kuja kuona viongozi kama Balozi Seif Iddi, Mohamed Seif Khatib, Hamad Rashid Mohamed, na wengine wakija unga mkono hoja hii. Hatujui bado, lakini haitashangaza! Hali hii haitadumisha au kuboresha Muungano bali itauvunja Muungano.
Kwa upande wa inayoitwa Tanzania Bara, iwapo Mgombea Urais wa Muungano atatokea nchi jirani ya Zanzibar huku wakijua kwamba makamu wake automatically pia atatokea Zanzibar, watakaoongoza katika kupinga hali hii haitakuwa watu wengine bali wale wale makada wa CCM ambao leo ndani ya bunge la katiba wanajiita Maoni ya Walio Wengi, wanaotetea mfumo huu huu wa serikali mbili zilizoboreshwa. Fitina zilizomkumba Dr. Salim Ahmed Salim 2005 hazitafua dafu kwa fitina zitakazojitokeza katika mazingira tunayojadili hapa. Wana CCM ambao watakuwa katika makundi ya kutafuta Rais wa Muungano wataendesha kampeni kubwa kupinga uongozi wa Muungano kwenda kwa nchi jirani katika kofia zote mbili za juu Rais wa Muungano na Makamu wa Rais wa Muungano.
Aidha kwa makusudi au kwa bahati mbaya, wanachoambiwa Wazanziri na CCM ni kwamba - chini ya mfumo wa serikali mbili zilizoboreshwa, Wazanzibari wajiandae kuwa ni wasindikizaji tu wa Uongozi katika Jamhuri ya Muungano. Pia CCM nayo ijiandae kutupiwa lawama na malalamiko mapya juu ya Ukoloni wa Tanganyika kwa Zanzibar. Mbegu ya kuvunjika kwa muungano itaanza kuchepuka.
Inaendelea bandiko linalofuatia
cc - Nguruvi3, @FJM,@ tpaul, @Mag3, @JokaKuu, @Mwigulu Nchemba, @Nape Nnauye, @MwanaDiwani,@zomba, @Ritz, @ZeMarcopolo, @Gamba la Nyoka, @Mtanganyika , @Mzee Mwanakijiji, @Pasco, @Kitila Mkumbo, @EMT, @MTAZAMO, @Kobello,@Jasusi, @zumbemkuu, @Mimibaba, @Zakumi, @Invisible, Tumaini Makene, @Yericko Nyerere, @FaizaFoxy, @Dingswayo, @Makusudically, @Tumaini Makene, @Nicholas, @Mtu wa Pwani, @jmushi1, @Mwita Maranya, @Ngongo, @zumbemkuu, Zitto, @Mzawa Halisi, Barubaru, Mindi, Kiganyi, @Communist, Dr. F. Ndungulile, Ezekiel Maige, Anna Tibaijuka, HKigwangalla, candidscope, tpaul, Tetty, TIMING, chama
Katika hotuba yake ndani ya Bunge la Katiba mjini Dodoma hivi karibuni, Rais Kikwete, pamoja na mengineyo, alinukuliwa akisema kwamba muungano wa serikali tatu uliopendekezwa katika rasimu ya katiba haufai kwa kuwa ni mfumo legevu na utawaongezea wananchi mzigo. Rais Kikwete pia alienda mbali na kueleza kwamba:
Sisi katika Chama Cha Mapinduzi, tunaamini mfumo wa Serikai Mbili, ndio murua na rahisi kutekelezeka.
Hapa Rais Kikwete alikuwa akimaanisha mfumo wa serikali mbili ambao CCM imesema itauboresha, kama njia ya kuondoa kero za muungano zilizodumu kwa zaidi ya miaka 30. Kufuatia hotuba hii ya Rais Bungeni, huu ukawa ndio msingi wa hoja za kile kilichoitwa Maoni Ya Wengi ndani ya bunge maalum la Katiba. Na ni msimamo huu wa Maoni ya Wengi ambao pia ukapelekea upande mwingine wa hoja, ulioitwa Maoni ya Wachache, hatimaye kuamua kujiondoa katika bunge hili, chini ya mwamvuli wa UKAWA kwa nia ya kwenda kuwaeleza wananchi jinsi gani waliojiita wengi bungeni walivyoamua kupuuza maoni ya wananchi kuhusiana na rasimu ya katiba.
Kama tutakavyojadili, Muungano wa Serikali Mbili Zilzoboreshwa, kama unavyopigiwa kampeni na CCM, hautaimarisha Muungano na hautamaliza malalamiko, lawama na shutuma za kero za Muungano. Badala yake, Serikali mbili zilizoboreshwa, zitavunja na kuuzika Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Mjadala wetu umegawanyika katika sehemu kuu tatu.
Sehemu ya kwanza tutajadili:
· Muundo Wa Serikali.
· Madaraka ya Viongozi.
· Muundo Wa Bunge.
Hapa tutaonyesha jinsi gani masuala haya chini ya mfumo wa serikali mbili zilizoboreshwa yataenda kuvunja muungano.
Sehemu ya pili tutajadili:
· Mapato na Matumizi Ya Kuendesha Muungano.
· Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Kimataifa, Mikopo, na Misaada.
· Mapendekezo ya Baraza la Mapinduzi kuhusu masuala ya kuyaondoa katika Orodha ya mambo ya Muungano.
Vile vile, tutaonyesha jinsi gani masuala haya chini ya mfumo wa serikali mbili zilizoboreshwa yataishia kuvunja muungano.
Na Sehemu ya TATU tutajadili:
· Sheria Za Ndani na Nje ya Muungano.
· Mgongano wa Kikatiba.
· Kuzinduka kwa Utaifa kwa pande zote mbili za Muungano (Tanganyika na Zanzibar). Muungano.
Hapa pia tutaonyesha jinsi gani masuala haya chini ya mfumo wa serikali mbili zilizoboreshwa yataenda kuvunja muungano.
SEHEMU YA KWANZA
MUUNDO WA SERIKALI, MADARAKA YA VIONGOZI NA MUUNDO WA BUNGE
Katika hotuba yake bungeni, Rais Kikwete aliwahimiza wajumbe wa Bunge la Katiba juu ya umuhimu wa kuwaenzi Waasisi wa Muungano (Mwalimu Nyerere na Sheikh Karume), kwa vile wao walitaka na walituachia mfumo wa serikali mbili. Wanaojiita Maoni Ya Walio Wengi Bungeni, ambao wanapigia chepuo mfumo wa serikali mbili zilizoboreshwa wanafahamu kwamba muundo wa muungano ulioachwa na waasisi wetu ulikuwa ni muungano wa NCHI MOJA, yenye SERIKALI MBILI. Zanzibar ilikuwa ni SEHEMU YA JAMHURI YA MUUNGANO. Hiyo ndio hali ya Muungano ambayo Mwalimu Nyerere alipofariki kumi na tano iliyopita. Leo hii Zanzibar sio tu kwamba tayari imeshaondoa mambo mengi ya msingi juu ya muungano, bali pia, kwa mujibu wa marekebisho ya kumi ya Katiba (2010), Zanzibar haitambuliwi tena kama ni sehemu ya muungano, bali inatambulika (Kikatiba) kama nchi kamili, yenye bendera yake, wimbo wake wa taifa, na amiri jeshi mkuu.
Pamoja na Muungano sasa kuwa na Nchi MBILI, SERIKALI MBILI, CCM bado inasema kwamba serikali mbili hizi zitaziboreshwa, huku chama kikipendekeza kwamba katika katiba ijayo, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano (ambae leo hii ni Dr. Bilal), anyanganywe mamlaka aliyokuwa nayo ya kuwa msaidizi mkuu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano, na badala yake, mamlaka hayo yahamie kwa Rais wa nchi jirani ya Zanzibar. Kwa maana nyingine, chini ya serikali mbili zilizoboreshwa na CCM, Rais wa nchi jirani ya Zanzibar atakuwa ndiye msaidizi mkuu wa Rais wa Muungano kwa masuala ya Zanzibar, lakini pia atakuwa ni mmoja wa viongozi wakuu wa nchi (Tanzania). CCM haisemi lolote kuhusu kiongozi atakayekuwa msaidizi wa Rais wa Muungano katika masuala ya Tanganyika (ukipenda, sema - Tanzania Bara).
Mkataba wa Muungano (1964) uliweka utaratibu ambao Rais wa Muungano wa NCHI Moja, alikuwa na wasaidi wake wakuu wawili Makamu wa Kwanza wa Rais ambaye alikuwa anawajibika na masuala yote yasiyo ya muungano kwa upande wa Zanzibar (Marehemu Karume), na Makamu wa Pili wa Rais ambaye alikuwa anawajibika na masuala yote yasiyo ya muungano kwa upande wa Tanganyika (Marehemu Kawawa).
Chini ya Katiba Mpya, CCM inapendekeza kwamba Rais wa Zanzibar afanywe kuwa Makamu wa Rais wa Muungano bila ya kujalisha Rais wa Muungano anatokea upande upi wa Muungano. Kwa kufanya hivyo, CCM inadai kwamba hali hii itamwongezea Rais wa Zanzibar - madaraka na hadhi ndani ya serikali ya Muungano na pia nje ya nchi.
MGOGORO UTAKAOJITOKEZA KUTOKANA NA MAPENDEKEZO YA RAIS WA ZANZIBAR KUWA MAKAMU WA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO
Chini ya mfumo huu wa serikali mbili zilizoboreshwa, CCM haisemi iwapo Rais ni mmoja - yaani Rais wa Jamhuri ya Muungano, ni kiongozi gani ndiye atakayesimamia Mawaziri watakaokuwa wanasimamia mambo ya Tanzania Bara katika mfumo huu wa serikali mbili ulioboreshwa. Pamoja na kuendelea kupigia debe serikali mbili zitakazoboreshwa, CCM bado imeendelea kukaa kimya juu ya ufafanuzi wa masuala muhimu (kiutekelezaji), kwa mfano, - katika mazingira ya Zanzibar kuwa ni nchi kamili, yenye mamlaka kamili, ikitokea kwamba Rais wa Muungano anatokea upande wa pili wa muungano (Zanzibar), JE:
· Rais huyu kutoka nchi jirani ya Zanzibar atasimamia masuala yasiyo ya muungano - ya upande unaoitwa Tanzania Bara, ndani ya Jamhuri ya Muungano, kwa mamlaka yepi?
· Iwapo Rais wa Muungano atatokea panapoitwa Tanzania Bara, Rais huyu wa Muungano atakuwa na mamlaka yepi ya kusimamia mambo ya Tanzania Bara wakati yeye atakuwa amechaguliwa na wananchi wa pande zote mbili za muungano?
· Zipo wapi pande mbili za muungano bila ya kuwepo kwa Serikali ya Tanganyika?
CCM haina muda wa kutoa majibu kwa maswali haya muhimu. Kutokana na hali hii, serikali mbili zilizoboreshwa, hazitaboresha muungano bali zitajenga mazingira ya kuvunja muungano. Hii ni kwa sababu:
Tuseme Rais wa Muungano anatokea upande wa nchi jirani ya Zanzibar, ambaye chini ya mfumo wa serikali mbili ambao CCM inadai utakuwa umeboreshwa, Rais wa Zanzibar pia atakuwa ni Makamu wa Rais wa Muungano. CCM inapendekeza kuwa iwe hivyo bila ya kujali Rais wa Muungano atatokea upande upi wa Muungano. Kitakachotokea ni kwamba - siku moja, Rais wa Muungano na Makamu Wa Rais Wa Muungano, wote watakuwa wametokea nchi jirani ya Zanzibar. Kwa maana hii, inachokifanya CCM, aidha kwa makusudi au bahati mbaya, CCM inaweka mazingira ambayo Zanzibar hawataweza tena kutoa Rais wa Muungano. Hii ni kwa sababu:
Kama tulivyoona, chini ya serikali mbili zilizoboreshwa na CCM, Rais wa Zanzibar automatically, atakuwa pia ni Makamu wa Rais wa Muungano. CCM ikimsimamisha mgombea Urais wa Muungano kutokea nchi jirani ya Zanzibar, nchi ambayo pia automatically itatoa makamu wa Rais wa Muungano, chini ya mazingira ya sasa ya mfumo wa vyama vingi vya siasa nchini, wapiga kura kutoka upande wa inayoitwa Tanzania Bara, upande ambao una wapiga kura zaidi ya 90% ya wapiga kura wote wa Jamhuri ya Muungano, wengi ya wapiga kura hawa kutoka Tanzania Bara, hawatakubali kumchagua mgombea wa urais (CCM) kutokea nchi ya Zanzibar huku wakijua kwamba makamu wake pia anatokea huko huko nchini Zanzibar. Madhara yake ni yepi?
Ni kwamba chini ya mfumo wa Serikali mbili zilizoboreshwa na CCM, Zanzibar ianze kusahau kutoa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kitachofuatia ni Zanzibar kuanza kulalamika kwamba wanabaguliwa, wanonewa, wananyimwa haki ndani ya Jamhuri ya muungano, kwahiyo waachwe Wapumue. And interestingly enough, watakaongoza katika kutoa hoja hizi ni wale wale wazanzibari ambao Islaml Jusa alisema kwamba walipofika Dodoma Waliufyata. Ni wale wale ambao leo wanapinga kwamba wao sio wasaka tonge. Katika kundi hili, hatutashangaa kuja kuona viongozi kama Balozi Seif Iddi, Mohamed Seif Khatib, Hamad Rashid Mohamed, na wengine wakija unga mkono hoja hii. Hatujui bado, lakini haitashangaza! Hali hii haitadumisha au kuboresha Muungano bali itauvunja Muungano.
Kwa upande wa inayoitwa Tanzania Bara, iwapo Mgombea Urais wa Muungano atatokea nchi jirani ya Zanzibar huku wakijua kwamba makamu wake automatically pia atatokea Zanzibar, watakaoongoza katika kupinga hali hii haitakuwa watu wengine bali wale wale makada wa CCM ambao leo ndani ya bunge la katiba wanajiita Maoni ya Walio Wengi, wanaotetea mfumo huu huu wa serikali mbili zilizoboreshwa. Fitina zilizomkumba Dr. Salim Ahmed Salim 2005 hazitafua dafu kwa fitina zitakazojitokeza katika mazingira tunayojadili hapa. Wana CCM ambao watakuwa katika makundi ya kutafuta Rais wa Muungano wataendesha kampeni kubwa kupinga uongozi wa Muungano kwenda kwa nchi jirani katika kofia zote mbili za juu Rais wa Muungano na Makamu wa Rais wa Muungano.
Aidha kwa makusudi au kwa bahati mbaya, wanachoambiwa Wazanziri na CCM ni kwamba - chini ya mfumo wa serikali mbili zilizoboreshwa, Wazanzibari wajiandae kuwa ni wasindikizaji tu wa Uongozi katika Jamhuri ya Muungano. Pia CCM nayo ijiandae kutupiwa lawama na malalamiko mapya juu ya Ukoloni wa Tanganyika kwa Zanzibar. Mbegu ya kuvunjika kwa muungano itaanza kuchepuka.
Inaendelea bandiko linalofuatia
cc - Nguruvi3, @FJM,@ tpaul, @Mag3, @JokaKuu, @Mwigulu Nchemba, @Nape Nnauye, @MwanaDiwani,@zomba, @Ritz, @ZeMarcopolo, @Gamba la Nyoka, @Mtanganyika , @Mzee Mwanakijiji, @Pasco, @Kitila Mkumbo, @EMT, @MTAZAMO, @Kobello,@Jasusi, @zumbemkuu, @Mimibaba, @Zakumi, @Invisible, Tumaini Makene, @Yericko Nyerere, @FaizaFoxy, @Dingswayo, @Makusudically, @Tumaini Makene, @Nicholas, @Mtu wa Pwani, @jmushi1, @Mwita Maranya, @Ngongo, @zumbemkuu, Zitto, @Mzawa Halisi, Barubaru, Mindi, Kiganyi, @Communist, Dr. F. Ndungulile, Ezekiel Maige, Anna Tibaijuka, HKigwangalla, candidscope, tpaul, Tetty, TIMING, chama
Last edited by a moderator: