James Martin
JF-Expert Member
- Apr 2, 2016
- 1,206
- 1,509
Siku chache zilizopita nilitoa maoni yangu kutathmini awamu hii ta tano. Niliandika kuwa pamoja na kuchukizwa na na baadhi ya mambo lakini namuunga mkono Magufuli. Niliandika pia siamini kama Rais anaweza kuyajua mambo yote ya moja kwa moja pale anapoingia madarakani, mambo mengine hujifunza akiwa ofisini. Kwahiyo, nilikuwa tayari kumuunga mkono Magufuli nikiamini kuwa atajifunza kutokana na makosa.
Kwa bahati mbaya nilifanya makosa. Kwanza, nataka kumweleza Magufuli kuwa kwasababu nilikuwa namuunga mkono haina maana nilikuwa nauchukia upinzani. Nathamini mchango wao na naamini kama serikali ikiachiwa ifanye inavyotaka bila kukosolewa itajisahau na kufanya mambo ya hovyo.
Pili, mambo wanayofanyiwa wapinzani hivi karibuni siyafurahii na siwezi kuvumilia upuuzi huu.
Link hapo chini kinaonyesha maoni yangu siku chache zilizopita nikimmunga mkono.
Magufuli nakuunga mkono lakini kuwa makini kwenye kipindi chako cha pili
Kwa bahati mbaya nilifanya makosa. Kwanza, nataka kumweleza Magufuli kuwa kwasababu nilikuwa namuunga mkono haina maana nilikuwa nauchukia upinzani. Nathamini mchango wao na naamini kama serikali ikiachiwa ifanye inavyotaka bila kukosolewa itajisahau na kufanya mambo ya hovyo.
Pili, mambo wanayofanyiwa wapinzani hivi karibuni siyafurahii na siwezi kuvumilia upuuzi huu.
Link hapo chini kinaonyesha maoni yangu siku chache zilizopita nikimmunga mkono.
Magufuli nakuunga mkono lakini kuwa makini kwenye kipindi chako cha pili