Sir John Roberts
JF-Expert Member
- Mar 1, 2017
- 9,618
- 15,942
Nimefuatilia kwa umakini sana huo mkutano wa UVCCM taifa ambapo vijana kadhaa (chipukizi) wamepiga kampeni kitaifa kuchaguliwa katika nafasi mbalimbali za uongozi.
Chupukizi ndani ya CCM siyo kitu kipya tangu tunasoma huko chipukizi ilikuwepo lakini naona kama mwaka huu imekuja kivingine kabisa. Watu wazima viongozi wakishiriki kuwapigia kampeni watoto wao ili wachaguliwe katika nafasi mbali mbalimbali za uongozi ndani ya chama.
Siyo jambo baya lakini naona mapungufu kadhaa ambayo kama Chama kitaacha yaendelee basi CCM huko mbeleni kitakua ni mali ya watu wenye uwezo na viongozi serikalini. Nasema hivyo kwa sababu gani?
1. Tumeona watoto wote waliokua wanawania hizo nafasi ni watoto aidha wa wafanyabiashara wakubwa au viongozi wakubwa serikalini utasikia majina kama Nchemba, mahiga , sheta n.k na kiuhalisia watakaowezs kuwa na ubavu wa kufanya kampeni ni wenye uwezo wa kifedha na ushawishi unadhani atatoka mtoto wa mvuvi kule ukerewe aje kuwania nafasi za kitaifa kama hizo uwezo huo anaupata wapi? Hapa CCM tumefeli na mwisho siyo mzuri.
2. Hawa watoto kuanza kuwaweka kwenye majukwaa ya kisiasa kwa umri wao si sahihi kabisa. Umri huo watoto tunawanyima haki zao za msingi kama watoto kuanza kuwafanya wafikirie mambo makubwa ambayo ni tofauti na umri walio nao. Chipukizi ibaki kama ilivyokua mashuleni lakini kuanza kuipa attention za kitaifa kiasi hiki naona kama ni ujinga uliopitiliza. CCM inaelekea kubaya.
3. Naendelea kusisitiza kuwa CCM ni chama cha wakulima na wafanyakazi labda kama hiyo slogan siku hizi haipo tuambiwe. Kuna dalili viongozi wanaanza kuwaingiza watoto wao kwenye chama mapema kama ndio sehemu ya kupatia maisha huko baadae. Chama siyo mali ya viongozi. CCM kama mtashindwa kulikemea hili huko mbele naona kabisa mkijichimbia kaburi.
Ukifuatilia maoni ya watanzania wengi hata baada ya huu uchaguzi utagundua wengi wanaona ni kama watoto wa viongozi wanaandaliwa kuja kurithi nafasi za wazazi wao. CCM mkiliendekeza hili hiki chama huko mbeleni kitakua na hali ngumu nawaambia ukweli kutakua na matabaka ambayo mmeyajenga wenyewe. Nakumbuka marehemu Magufuli katika hotuba yake moja alipinga hili suala na mimi nilimuunga mkono sasa yamerudi.
Nikuombe mama samia wewe ndio mwenyekiti wa CCM taifa unapoona madhaifu kama haya kemea na usiruhusu CCM ikawa ni mali ya watu wachache. Hili la chipukizi nategemea utalitolea maekelezo mapema iwezekanavyo.
Ni mimi mwanachama mwandamizi wa CCM .
Sir John Roberts.
Chupukizi ndani ya CCM siyo kitu kipya tangu tunasoma huko chipukizi ilikuwepo lakini naona kama mwaka huu imekuja kivingine kabisa. Watu wazima viongozi wakishiriki kuwapigia kampeni watoto wao ili wachaguliwe katika nafasi mbali mbalimbali za uongozi ndani ya chama.
Siyo jambo baya lakini naona mapungufu kadhaa ambayo kama Chama kitaacha yaendelee basi CCM huko mbeleni kitakua ni mali ya watu wenye uwezo na viongozi serikalini. Nasema hivyo kwa sababu gani?
1. Tumeona watoto wote waliokua wanawania hizo nafasi ni watoto aidha wa wafanyabiashara wakubwa au viongozi wakubwa serikalini utasikia majina kama Nchemba, mahiga , sheta n.k na kiuhalisia watakaowezs kuwa na ubavu wa kufanya kampeni ni wenye uwezo wa kifedha na ushawishi unadhani atatoka mtoto wa mvuvi kule ukerewe aje kuwania nafasi za kitaifa kama hizo uwezo huo anaupata wapi? Hapa CCM tumefeli na mwisho siyo mzuri.
2. Hawa watoto kuanza kuwaweka kwenye majukwaa ya kisiasa kwa umri wao si sahihi kabisa. Umri huo watoto tunawanyima haki zao za msingi kama watoto kuanza kuwafanya wafikirie mambo makubwa ambayo ni tofauti na umri walio nao. Chipukizi ibaki kama ilivyokua mashuleni lakini kuanza kuipa attention za kitaifa kiasi hiki naona kama ni ujinga uliopitiliza. CCM inaelekea kubaya.
3. Naendelea kusisitiza kuwa CCM ni chama cha wakulima na wafanyakazi labda kama hiyo slogan siku hizi haipo tuambiwe. Kuna dalili viongozi wanaanza kuwaingiza watoto wao kwenye chama mapema kama ndio sehemu ya kupatia maisha huko baadae. Chama siyo mali ya viongozi. CCM kama mtashindwa kulikemea hili huko mbele naona kabisa mkijichimbia kaburi.
Ukifuatilia maoni ya watanzania wengi hata baada ya huu uchaguzi utagundua wengi wanaona ni kama watoto wa viongozi wanaandaliwa kuja kurithi nafasi za wazazi wao. CCM mkiliendekeza hili hiki chama huko mbeleni kitakua na hali ngumu nawaambia ukweli kutakua na matabaka ambayo mmeyajenga wenyewe. Nakumbuka marehemu Magufuli katika hotuba yake moja alipinga hili suala na mimi nilimuunga mkono sasa yamerudi.
Nikuombe mama samia wewe ndio mwenyekiti wa CCM taifa unapoona madhaifu kama haya kemea na usiruhusu CCM ikawa ni mali ya watu wachache. Hili la chipukizi nategemea utalitolea maekelezo mapema iwezekanavyo.
Ni mimi mwanachama mwandamizi wa CCM .
Sir John Roberts.