CCM mwendo mdundo! CHADEMA yaanguka

CCM mwendo mdundo! CHADEMA yaanguka

Poor unataka kila mida tuchangie na kusifia chadema, mlikuwa mnataka baraza libadilishwe yap JK amekubali kulisuka upya sasa mnahaha baada ya kukosa biti ya kucheza nayo mtaani mtaenda kwa matukio huku kina mbowe,slaa na josephine wakiendelea kuzitengeneza
hii thread yako haina mshiko tafuta wakina rejao wachangie huu umbea wako
 
Watanzania wanachotaka ni unafuu wa maisha na utekelezaji wa ilani. Kuvunja baraza in hatua ndogo tu kwani mfumo wa utawala ni mbovu. Hata akiteua jipya na hali ikabaki hivi tutaendelea kulia na kuwa maskini. Angalia maige juzi tu hapa tayari ana miliki nyumba ya mabilioni. Tuna safari ndefu
 
Amekidhi vipi matakwa ya watanzania? uone atakachokiteua na baada ya hapo mwone nini kinachofuata? huko ni kutapatapa kwao maana hawajui nini cha kufanya na itawagharimu sana CCM, huyu jamaa nadhani mpaka kumaliza muda wake atakuwa ameota vidonda vya tumbo. Kumtoa Jairo tu ilikuwa issue
 
Upinzani wekeni kando, JK amekidhi matakwa ya watanzania, leo roho kwatu!!!

Nilitegemea kwa sababu uko humu kwenye jamii ya ma great thinker ungekuwa una huwezo wa kutumia ubongo ipasavyo,kumbe haiko hivyo,baada ya kusikitika kuwa una rais ambaye anaendeshwa kwa kuangalia upepo we unafurahia,katika maisha yangu sijaona gamba gumu kuelewa kama wewe, hemu jiulize je jk alikuwa wapi siku zote kutofanya maamuzi kama haya! yani me najua vijana wa magamba ni wagumu kuelewa lakini si kiasi hiki! yani kusoma hujui ata picha huoni? eti ccm mwendo mdundo wakati upepo tu umewapeleka ,je kimbunga kinacho kuja?.Amani kwako
 
Watanzania jana wamekenua meno baada ya kipenzi chao Mheshimiwa Rais Kikwete kukidhi kiu yao ya kuvunjwa baraza la mawaziri na kusudio la kuwafikisha katika vyombo vya sheria waliohusika kufisadi mali za umma.

Hatua hiyo imezidi kukipaisha CCM na wakati huo huo kukiporomosha chama pinzani CHADEMA huku tukielekea 2015. Watanzania kutoka mashariki hadi magharibi, kaskazini mpaka kusini jana jioni walikuwa katika makundi wakisherekea hatua ya JK na kuipongeza CC ya CCM kuwa ina wapenda Tanzania na manufaa kwa Watanzania.

Poleni CHADEMA, tafuteni hoja nyingine, ya kuvunja baraza la mawaziri haina mshiko tena!
hapo kwenye red chunga sana mkuu.
- Mh. Nundu keshasema wazi kuwa alizungukwa na Naibu wake akishirikiana na mkuu wake
- Naibu waziri Mh. Nyarandu katoa memo na Waziri kasema Mkuu wake top figures wanajua kinachoendelea
- Mh. Maige pia kaweka wazi kuwa hawezi kujihudhuru, unadhani twiga wale walenda Arabuni bila Magogoni kujua!?
- Hapo Yupo Mh. Ngeleja na RICHMOND/DOWANS zake ambapo RA aliwahi kumtaja 'mhusika' kwenye vikao vyenu
- ...na hapo bado Mkullo hajaripuka.

Kwa haraka unaweza kudhani mmezishika mahakama na vyombo vya usalama lakini hii nchi ujumla wake ni ya Watanzania na kinachotokea ni ujanjaujanja na uongo ambavyo wahenga walisema njia zao daima ni fupi.

Fikiria tena kabla ya kuleta hii kitu jf au iondoe kama unaweza

 
Watanzania jana wamekenua meno baada ya kipenzi chao Mheshimiwa Rais Kikwete kukidhi kiu yao ya kuvunjwa baraza la mawaziri na kusudio la kuwafikisha katika vyombo vya sheria waliohusika kufisadi mali za umma.

Hatua hiyo imezidi kukipaisha CCM na wakati huo huo kukiporomosha chama pinzani CHADEMA huku tukielekea 2015. Watanzania kutoka mashariki hadi magharibi, kaskazini mpaka kusini jana jioni walikuwa katika makundi wakisherekea hatua ya JK na kuipongeza CC ya CCM kuwa ina wapenda Tanzania na manufaa kwa Watanzania.

Poleni CHADEMA, tafuteni hoja nyingine, ya kuvunja baraza la mawaziri haina mshiko tena!

Mzoga unapokuwa na matumaini ya kurudishiwa uhai.
 
Watanzania jana wamekenua meno baada ya kipenzi chao Mheshimiwa Rais Kikwete kukidhi kiu yao ya kuvunjwa baraza la mawaziri na kusudio la kuwafikisha katika vyombo vya sheria waliohusika kufisadi mali za umma.

Hatua hiyo imezidi kukipaisha CCM na wakati huo huo kukiporomosha chama pinzani CHADEMA huku tukielekea 2015. Watanzania kutoka mashariki hadi magharibi, kaskazini mpaka kusini jana jioni walikuwa katika makundi wakisherekea hatua ya JK na kuipongeza CC ya CCM kuwa ina wapenda Tanzania na manufaa kwa Watanzania.

Poleni CHADEMA, tafuteni hoja nyingine, ya kuvunja baraza la mawaziri haina mshiko tena!
Mbona unaonekana kuwa mwenye AKILI NA UWEZO MZURI TU? Sasa nashangaa jinsi unavyowaza na kuchambua mambo. Unashangilia Chama kinachovunja baraza la mawaziri! Unachoshangilia ni nini? Kwamba watu wameharibu unao kuwa ni ushindi? HILI NI JAMBO LA AIBU kwa kila moja wetu awe CCM au Upinzani. NI AIBU KWAKO, KWANGU NA KWA WOTE WAPENDA :shocked:MAENDELEO.:shocked::crying:
 
Wewe ni KENGE.. mbumbumbu na juha kupata tokea katika ulimwengu huu.. Jk, salama ya uongozi wake ilikua ni kulivunja Baraza la Wachumia tumbo..
Na endapo asingefanya hilo,Nguvu ya umma ingemtia adabu na angeweka historia kuwa Rais wa kwanza East Afrika kuondolewa kwa shinikizo la Wenyenchi...
CDM ilihamasisha watu,na watu wakaitikia na wazalendo MP wa CCM waliunga mkono..
Chezea CDM wee...
Watanzania jana wamekenua meno baada ya kipenzi chao Mheshimiwa Rais Kikwete kukidhi kiu yao ya kuvunjwa baraza la mawaziri na kusudio la kuwafikisha katika vyombo vya sheria waliohusika kufisadi mali za umma.

Hatua hiyo imezidi kukipaisha CCM na wakati huo huo kukiporomosha chama pinzani CHADEMA huku tukielekea 2015. Watanzania kutoka mashariki hadi magharibi, kaskazini mpaka kusini jana jioni walikuwa katika makundi wakisherekea hatua ya JK na kuipongeza CC ya CCM kuwa ina wapenda Tanzania na manufaa kwa Watanzania.

Poleni CHADEMA, tafuteni hoja nyingine, ya kuvunja baraza la mawaziri haina mshiko tena!
 
Kwa mtanzania mwenye ufahamu, huu ni udhaifu wa washauri wanaokizunguka chama. Jambo lililoanzia bungeni ni bora lingeishia bungeni kuliko kupokonywa na chama. Udhaifu unakwenda kwa wabunge wa CCM kuwa hawawezi kutoa maamuzi dhidi ya serikali isipokuwa chama tu. Upinzani unanyanyuliwa kwa kutofikiria washauri wa chama. CC ingepaswa kukaa kabla ya bunge baada ya kupokea ripoti ya mkaguzi wa serikali ingeonesha umakini wa wajumbe wa CC kukiongoza na kukishauri chama. Ushauri wa bure, " Wajumbe wa CC amkeni msingojee shinikizo kutoka upande wowote kuitisha vikao kujadili mustakabali wa nchi hii, kwani ubadhilifu umefanyika juzi mpaka mkae vikao jana? mbona magazeti yaliripoti? Mnakidhoofisha chama badala ya kukinyanyua"

Tunakoelekea umuhimu wa upinzani unazidi kuimarika badala ya kushuka hivyo nafasi ya CCM kutawala daima inafifia.
 
Watu wanaoleta habari ambazo hazijafanyiwa uchunguzi,inatakiwa wapigwe BAN kwani wanapoteza muda wa GREAT THINKERS kusoma mipasho yao.
 
Narudia tena WEKENI KANDO UCHADEMA; shime tukubali RAIS wetu ni msikivu. AU nyie mlitaka mpandie hiyo hoja na kuingia barabarani. JK na CCM imewashika kitovuni, mnapata shida kupumua.

Siyo ajabu nyie ni mto na CCM ni bahari!!
 
Watanzania jana wamekenua meno baada ya kipenzi chao Mheshimiwa Rais Kikwete kukidhi kiu yao ya kuvunjwa baraza la mawaziri na kusudio la kuwafikisha katika vyombo vya sheria waliohusika kufisadi mali za umma.

Hatua hiyo imezidi kukipaisha CCM na wakati huo huo kukiporomosha chama pinzani CHADEMA huku tukielekea 2015. Watanzania kutoka mashariki hadi magharibi, kaskazini mpaka kusini jana jioni walikuwa katika makundi wakisherekea hatua ya JK na kuipongeza CC ya CCM kuwa ina wapenda Tanzania na manufaa kwa Watanzania.

Poleni CHADEMA, tafuteni hoja nyingine, ya kuvunja baraza la mawaziri haina mshiko tena!

Na tunaandaa maanadamano nchi nzima kupongeza maamuzi magumu ya rais kikwete na cc
 
Jipeni moyo tu siku yenu ya kulia na kusaga meno yaja!

Kitendo cha Kikwete kuridhia kulivunja baraza la mawaziri kinakiimarisha Chadema zaidi kuliko CCM, wananchi wanajua wazi kuwa bila ya Chadema Kikwete asingechukua uamuzi aliochukua. Zaidi ya hilo namna ambavyo Kikwete anaonekana kutojiamini kunadhihirisha kuwa CCM siyo chama makini hadi kikateua mtu asiyejiamini kuchukua maamuzi magumu
 
Back
Top Bottom