Watanzania jana wamekenua meno baada ya kipenzi chao Mheshimiwa Rais Kikwete kukidhi kiu yao ya kuvunjwa baraza la mawaziri na kusudio la kuwafikisha katika vyombo vya sheria waliohusika kufisadi mali za umma.
Hatua hiyo imezidi kukipaisha CCM na wakati huo huo kukiporomosha chama pinzani CHADEMA huku tukielekea 2015. Watanzania kutoka mashariki hadi magharibi, kaskazini mpaka kusini jana jioni walikuwa katika makundi wakisherekea hatua ya JK na kuipongeza CC ya CCM kuwa ina wapenda Tanzania na manufaa kwa Watanzania.
Poleni CHADEMA, tafuteni hoja nyingine, ya kuvunja baraza la mawaziri haina mshiko tena!
Naomba nikufafanulie jambo.
Bunge ndio lililoanzisha hoja ya kuwawajibisha mawaziri na watendaji waliohusika na ubadhirifu ulioonyeshwa kwe ripot ya CAG an ile ya kamati husika. Wapinzani ndani ya bunge wakatoa hoja kuwa kwa kuwa kila mwaka hayo yanajirudia na wahusika hawawajibishwi, woa wanaleta hoja ya kupiga kura ya kutokuwa na imani na PM. Wakiongozwa na Zitto Kabwe (Kamanda) wakaanza mchakato kama kanuni zinavyotaka, na wakapata 20% ya wabunge waliounga mkono hoja. Sasa basi
1. Kama kikwete asingeliridhia kubadili baraza kuwaondoa, sheria ingefuata mkondo wake Bunge lingeitishwa na kura kupigwa kutokuwa na imani na PM, ikishinda anaondolewa
2. CCM ni wengi bungeni, ila kumbuka wapinzani karibia wote waliunga mkono hoja hiyo wakiwemo wa CCM kadhaa. na ndani ya CCM kuna makundi ambayo hayajionyeshi waziwazi
- Kuna wanaopinga ufisadi ila kwa kuogopa
-Kuna wanaoumwa roho wenzao wanatafuna nao hawana nafasi na wanazitaka, baraza likivunjwa waweza kuambulia walao unaibu
-Kuna ambao wangetaka mtu mwingine awe PM kwa maslahi yao
-kuna ambao wangetaka kumwonyesha JK kuwa alikosea kuchagua PM
Wote hawa ni vigumu kuwabana endapo kura itakuwa ya siri.
3. kama JK akipuuza kura ikapigwa na PM akapigwa chini angekuwa ni PM wa pili katika awamu yake kupigwa chini kwa tuhuma hizohizo za ufisadi, hii ingempunguzia heshima sana, na ingeonyesha kuwa ni Raisi dhaifu kuliko wote.
Kwa sababu hizo alikuwa hana ujanja zaidi ya kutii maelekezo ya kamanda mdodo kabisa Zitto Kabwe, na NEC-CCM kubariki hilo bila ubishi