Kila siku mnatengeneza "movies" za kijinga na kufanya mambo ya hovyo sana kiasi kwamba mnawapa shida watetezi wenu wa mitandaoni. Kila jambo mnaboronga, mnadhani hao mliowaweka mitandaoni wawatetee nao ndiyo hawana hisia za utu kabisa?
Yaani mnadhani kusema uongo na kutetea ujinga unaoonekana shayiri dhahiri kwamba ni ujinga ni kazi rahisi? Mnadhani wao hawajui kwamba wanatetea mambo ya hovyo yanayodhuru taifa lao na vizazi vyao vijavyo?
Au mnadhani kwa kuwa "wanalipwa" basi watakuwa ni watumwa wa kusema yasiyowezekana na kuaminika kila siku? Hata kama wanatumia majina bandia lakini mjue na wao wanaujua ukweli hata kama wanaupindisha, siku ukweli ukizidi kina cha uwezo wao wa kuupindisha mjue watatapika hata yale msiyoyafikiria kwamba wanaweza kuyasema.
OLE WENU CCM!