Ngalikihinja
JF-Expert Member
- Sep 1, 2009
- 34,637
- 38,018
Na wanapata shida haswaaa...Kila siku mnatengeneza "movies" za kijinga na kufanya mambo ya hovyo sana kiasi kwamba mnawapa shida watetezi wenu wa mitandaoni. Kila jambo mnaboronga, mnadhani hao mliowaweka mitandaoni wawatetee nao ndiyo hawana hisia za utu kabisa?
Yaani mnadhani kusema uongo na kutetea ujinga unaoonekana shayiri dhahiri kwamba ni ujinga ni kazi rahisi? Mnadhani wao hawajui kwamba wanatetea mambo ya hovyo yanayodhuru taifa lao na vizazi vyao vijavyo?
Au mnadhani kwa kuwa "wanalipwa" basi watakuwa ni watumwa wa kusema yasiyowezekana na kuaminika kila siku? Hata kama wanatumia majina bandia lakini mjue na wao wanaujua ukweli hata kama wanaupindisha, siku ukweli ukizidi kina cha uwezo wao wa kuupindisha mjue watatapika hata yale msiyoyafikiria kwamba wanaweza kuyasema.
OLE WENU CCM!
1. La CAG na Spika kwenye neon DHAIFU, hawajui wasimame kwa nani.. Ndugai au ASSAD
2. La Kangi na CAG hawajui hata wasimame wapi, maana muongo anajulika… Maana hadi RAISI alishawahi sema kuna madudu huko kwenye SARE
3. La mshahara wa LISU na NDUGAI kuhusu mshahara nalo liliwapa shida sana… WAKABAKI KUSEMA HURUMA YA NDUGAI ETI NDO IMEPELEKEA MSHAHARA WA LISU ULIPWE..!!!
4. La ile bodi iliyovunjwa na huku ikapewa miaka mitatu nalo pa kusimama hawana
5. La TCRA na usajili wa simu kwa alama za vidole, wanatetema tu matipwatipwa hawatulii maana wamechanganywa vya kutosha
Yaani wanawafanya waweweseke ile mbaya… NA WANAWEWESEKA ZAIDI PALE BWANA YULE ANAPOKUWA KAKAA KIMYA, HAWAJUI YUPO UPANDE GANI...… MAANA WAO MARA ZOTE HUSIMAMA LILIKO JIWE.... sasa kama hawalioni lilipo wanahaha sana