S. S. Phares
JF-Expert Member
- Nov 27, 2006
- 2,138
- 82
Nilikuwa maeneo ya Shirati wakati wa mchakato wa CCM kumpata mgombea wa Rorya. Huyu Maina Owino alikuwa katika wale waliokuwa wanamtia kitimutimu Prof. Sarungi. Wengine wakati huo walikuwa Prof. Bwathondi wa Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI), na mwingine kama kumbukumbu zangu alikuwa mfanyakazi ama lecture wa institute moja.
Sasa kuwa Maina Owino alijitoa sababu ya kashfa hilo napingana nalo, na sipingani nalo kuwa namtetea. La hasha sijuani naye, na vile vile sikipendi chama tawala kwa kinachotufanyia, nadhani sina haja ya kuyataja hapa yanayofanywa na CCM.
Ila makubaliano yalikuwa Maina Owino ajitoe, ampishe Mzee. Ili miaka ijayo, yaani 2010, Mzee naye atamsaidia Maina kwa kampeni. Ikumbukwe kuwa wakati wa mchakato huu, kulikuwa na ugomvi wa dhahiri kati ya Sarungi na Bwathondi. Maina akiwa kundi la Sarungi.
Ninayo zaidi, lakini fedha tu za kumwaga, huyu kijana alikuwa nazo. Hivyo kujitoa kwake kulikuwa ni kuwa anasubiri akabidhiwe kijiti.
Wanabodi, nathani wote tunaona jinsi gani JF ilivyosambaa na jinsi watu wengi wasivyopenda udaku.
Mkuu Makelele heshima mbele kwa kusimamia ukweli kama unavyoufahamu wewe.
Tunasubiri kujua iwapo alichemsha huko Daruso...kama ilivyo hili la Ubunge ukweli utawekwa wazi.