CCM kwachafuka,mchawi anatafutwa

CCM kwachafuka,mchawi anatafutwa

Mbaya sana hali kama hii na helcopta sijajua tatizo ni watendaji wa CCM au tatizo ni ahadi za chama hazitafsiriki
 
Wtz bado tunakihitaji sana CCM kuleta maisha bora kwetu. Ila njia nzuri kwa CCM kufanya hivyo ni kuwa chama cha upinzani!!! CCM kitakuwa chama bora sana cha upinzani ambacho kitaisimamia kweli kweli serikali ijayo kuhakikisha inatekeleza matakwa na mategemeo ya wananachi. kwa uzoefu wao wa kuwa madarakani CCM kitawafanya watawala wapya wasilale waendelee kujipanga na kuhakikisha wanafanya yale ambayo wananchi wanayatarajia kutoka kwenye serikali mpya. na hicho ndicho kitafanya maisha yetu yazidi kupaa watz. Ni vizuri CCM ikaanza kujipanga kama chama pinzani ili kije kutusaidia watz....Asanteni watz kwa kuona njia ya maendeleo iko wapi na inapatikanaje!! kwa heri CCM madarakani na karibu kwenye upinzani.
 
Leo hapa Lumumba hakukaliki.Hakusemeki jema. Hasira zimetanda. Nyaraka kalikali zinapita kutoka huku kwenda kule. Ofisi zetu hapa leo zinakuwa chungu.Kisa,UKAWA kushinda vijijini na kwenye ngome za CCM kama Monduli. Makada wanalaumiana,vikao visivyoisha.Lakini,ni vikao kwa kukalishwa na si kukaa.Kukalishwa na kusimangwa. Kukemewa. Kushambuliwa.

Inasemwa hapa kuwa lengo la CCM halijatimia.Iitakiwa CCM ishinde kwa asilimia 90. Hadi sasa,hali ni tete.Mikoa yetu tuliyokuwa tunaitegemea imetuangusha. Majimbo yetu yaliyokuwa imara,yamesambaratika. Wabunge wetu wanaojitutumua Bungeni kama majembe ya chama, hawajasaidia kupatikana asilimia 90. Mambo ni shaghalabaghala. Mchafukoge!

Kambi za Urais na Escrow zinatajwa kama sababu kuu. Ziara za Katibu Mkuu wa chama nazo zinapondwa kwa kukosa matunda ya maana. Hakuna pa kushika,hakuna wa kumtupia lawama za moja kwa moja. Lakini,wakuu wanamtafuta wa kumwangushia 'jumba bovu'.Mchawi wa matokeo haya.

Kwani ni dhambi wapinzani kushinda vijijini na kwenye ngome za CCM?

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam

Ccm wamechukua karibu nusu na robo ya nchi nzima!
 
Haijalishi tutashinda kwa asilimia ngapi ila ushindi ni ushindi tu

Mkuu umeanza kukubali eheeeeeee!!! Ila asilimia 90 sasa haijalishi tena!!! Tena hiyo mtakayoshinda ni kwa wizi tu hakuna uhalali. Ingekuwa halali hata 20% msingepata. Fieni mbali wezi wakubwa mnalindana tu. Thanks Prof. Kikwete kwa kutufikisha hapa. Our Gorbachev.
 
Last year 2009 CCM ilishinda uchaguzi huu kwa asilimia 96, this time tunataka kuona mmeongeza asilimia ngapi, uje kwa data sio kuhororoja kwa maneno ya mitaani.

Huu ndio mtizamo sahihi.
CCM kabla ya uchaguzi wa mitaa na CCM baada ya uchaguzi wa mitaa .. ! Ipi imeshinda kwa kishindo. ?
 
attachment.php
 
Leo hapa Lumumba hakukaliki.Hakusemeki jema. Hasira zimetanda. Nyaraka kalikali zinapita kutoka huku kwenda kule. Ofisi zetu hapa leo zinakuwa chungu.Kisa,UKAWA kushinda vijijini na kwenye ngome za CCM kama Monduli. Makada wanalaumiana,vikao visivyoisha.Lakini,ni vikao kwa kukalishwa na si kukaa.Kukalishwa na kusimangwa. Kukemewa. Kushambuliwa.

Inasemwa hapa kuwa lengo la CCM halijatimia.Iitakiwa CCM ishinde kwa asilimia 90. Hadi sasa,hali ni tete.Mikoa yetu tuliyokuwa tunaitegemea imetuangusha. Majimbo yetu yaliyokuwa imara,yamesambaratika. Wabunge wetu wanaojitutumua Bungeni kama majembe ya chama, hawajasaidia kupatikana asilimia 90. Mambo ni shaghalabaghala. Mchafukoge!

Kambi za Urais na Escrow zinatajwa kama sababu kuu. Ziara za Katibu Mkuu wa chama nazo zinapondwa kwa kukosa matunda ya maana. Hakuna pa kushika,hakuna wa kumtupia lawama za moja kwa moja. Lakini,wakuu wanamtafuta wa kumwangushia 'jumba bovu'.Mchawi wa matokeo haya.

Kwani ni dhambi wapinzani kushinda vijijini na kwenye ngome za CCM?

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam

Mkuu huwa ninakuaminia sana kwa post zako humu, hujawahi sema uongo. Acha wamalizane tu. Salaam kwa Napelepele Mwa Nnauye!!! Ha ha ha!!! Katibu alizunguka weeeee kumbe alikuwa anajikusanyia za kumaliza kazi ya maziko!!! Sasa mpambano unakuja katiba na uchaguzi 2015. Kila rangi wataona hawa.
 
hapo ndipo ninapokukubali mheshimiwa Asumpta
Huyu amekalia kuti kavu,kamwulize jimbo lake la nkenge kama ana uhakika
wa kulikomboa 2015.Zamani jimboni kwake haikuwepo UKAWA safari hii kwenye vijiji vya Buyango UKAWA imefika.
Inawezekana hata kwenye kura za maoni kwenye chama chake asipite.
Tusubiri,muda utaeleza yote.
 
Mlituona wananchi tumenyamaza mkaisi sisi ni mazuzu kumbe tumeyaweka moyoni huku nyama zikiumia
 
Nani aliwaambia wamruhusu PINDA kutangaza nia. Na bado. Hatuko tayari. Tunawachinja mapemaaa.

BRING BACK OUR MONEY.
 
Mkuu upo!!!! Tulia dawa iingie taratibu daktari asije akaweka katika flesh badala ya vain. Inaitwa intravenous fluid hiyo inauma balaa. Pole.

Naona mnajipa moyo.

Unanikumbusha hadithi ya "kufungwa twafungwa lakini chenga twawala".

Angalia msije kukataa takwimu.
 
Leo hapa Lumumba hakukaliki.Hakusemeki jema. Hasira zimetanda. Nyaraka kalikali zinapita kutoka huku kwenda kule. Ofisi zetu hapa leo zinakuwa chungu.Kisa,UKAWA kushinda vijijini na kwenye ngome za CCM kama Monduli. Makada wanalaumiana,vikao visivyoisha.Lakini,ni vikao kwa kukalishwa na si kukaa.Kukalishwa na kusimangwa. Kukemewa. Kushambuliwa.

Inasemwa hapa kuwa lengo la CCM halijatimia.Iitakiwa CCM ishinde kwa asilimia 90. Hadi sasa,hali ni tete.Mikoa yetu tuliyokuwa tunaitegemea imetuangusha. Majimbo yetu yaliyokuwa imara,yamesambaratika. Wabunge wetu wanaojitutumua Bungeni kama majembe ya chama, hawajasaidia kupatikana asilimia 90. Mambo ni shaghalabaghala. Mchafukoge!

Kambi za Urais na Escrow zinatajwa kama sababu kuu. Ziara za Katibu Mkuu wa chama nazo zinapondwa kwa kukosa matunda ya maana. Hakuna pa kushika,hakuna wa kumtupia lawama za moja kwa moja. Lakini,wakuu wanamtafuta wa kumwangushia 'jumba bovu'.Mchawi wa matokeo haya.

Kwani ni dhambi wapinzani kushinda vijijini na kwenye ngome za CCM?

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam

Wakuu CCM sasa imebakia hatua moja tu kabla ya kukata roho. Haiingii akilini CCM kuleta watu kutoka Zanzibar (jimbo la Kwahani) kuja kupiga kampeni na kuwaambia watu wa Tanganyika nani anafaa kutuongoza na nani hafai. Kitendo hiki sio tu kinawachukiza watanganyika dhidi ya CCM bali kinahatarisha hata maisha ya Wazanzibar wanaokubali kuja kufanya biashara hii kichaa. Wazanzibar 250 waliletwa na CCM kata ya Mikocheni kufanya kampeni na kupiga kura kusaidia CCM. Hii haikuwa siri kila mkazi wa mikocheni A analifahamu.
 
Nakubaliana na wewe dada. Wametulisha sana ugoro wao. Kuna siku tutaheshimiana. Tusubiri matokeo kamili

Hawana jipya hao, ukitazama nyuzi zao walizoleta humu wanazotangaza ushindi utacheka, wanashangaza kwanini hawaoneshi waliposhindwa?

Hapo sasa.
 
Back
Top Bottom