shinji majige
JF-Expert Member
- Dec 13, 2014
- 560
- 214
Wewe km unaubia na hao mafisadi sema tu.
Una roho ngumu dada FF. Kwa mtu makini, wa chama tawala lazima ajiulize, nini kimetokea.Mfano, Mtwara mjini ngome ya CCM tangu tupate Uhuru leo matokeo yawe viti 53 upinzan na 58 CCM( wastani wa angalau 49%/51). Wewe hii haikuatui kweli kama wewe ni makini lazima utajiuliza kulikoni.
Hii ni mwanzo wa threat mbaya kwa CCM hivyo waondoe dosari. Matokeo yakiwa hivyo kwa ubunge kwa mfano, ni pigo kubwa tena sana, maamuz ya Bungeni kwa utaratibu wa Ndiyooooo hautakuwepo na hivyo kazi itakuwa ngumu sana. Wenzio wanapanga mikakati hawabweteki.
Hiyo haina wasi wasi kabisa, ukipiga hesabu kama unavyopiga wewe uakuwa unajidanganya, chukuwa matokeo ya Tanzania nzima halafu useme mna asilimia ngapi?
Usijidanganye, upinzani umeangukia pua.
Ataanza kufa kagame kabla ya ccm..... Ccm ndo imekufa kifo cha mende.
vipi umeshawasilisha fedha kwa bosi wako anayemiliki bodaboda unayopigia deiwaka???Aghhe escrow,mauaji ya tembe,sethi,ruge,tezi dume,nepi,wasira wa gombe mnafiki 6 lazma kuchafukoje
Leo hapa Lumumba hakukaliki.Hakusemeki jema. Hasira zimetanda. Nyaraka kalikali zinapita kutoka huku kwenda kule. Ofisi zetu hapa leo zinakuwa chungu.Kisa,UKAWA kushinda vijijini na kwenye ngome za CCM kama Monduli. Makada wanalaumiana,vikao visivyoisha.Lakini,ni vikao kwa kukalishwa na si kukaa.Kukalishwa na kusimangwa. Kukemewa. Kushambuliwa.
Inasemwa hapa kuwa lengo la CCM halijatimia.Iitakiwa CCM ishinde kwa asilimia 90. Hadi sasa,hali ni tete.Mikoa yetu tuliyokuwa tunaitegemea imetuangusha. Majimbo yetu yaliyokuwa imara,yamesambaratika. Wabunge wetu wanaojitutumua Bungeni kama majembe ya chama, hawajasaidia kupatikana asilimia 90. Mambo ni shaghalabaghala. Mchafukoge!
Kambi za Urais na Escrow zinatajwa kama sababu kuu. Ziara za Katibu Mkuu wa chama nazo zinapondwa kwa kukosa matunda ya maana. Hakuna pa kushika,hakuna wa kumtupia lawama za moja kwa moja. Lakini,wakuu wanamtafuta wa kumwangushia 'jumba bovu'.Mchawi wa matokeo haya.
Kwani ni dhambi wapinzani kushinda vijijini na kwenye ngome za CCM?
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
Hadi unatia huruma ulivyotepeta ngebe zote kwisha.
Hamna ujanja hata mseme nini, ukiwa hata 30% hamkufikisha? sasa ngojeni kipigo kingine takatifu 2015.
Kama kuna chama zaidi ya CCM kitaendesha Tanzania hii basi itakuwa kwenye uhai wa wajukuu zako uzeeni, si wewe wala wanao.
Hadi unatia huruma ulivyotepeta ngebe zote kwisha.