CCM kwachafuka,mchawi anatafutwa

CCM kwachafuka,mchawi anatafutwa

vuta nikuvute muongo mzushi wewe vikao gani vikae halafu saa tatu wewe uturushie taarifa. CCM ina utaratibu wa kuitisha vikao na unachoshangaza ni kuwa umekuwa msemaji wa tume ya uchaguzi au tamisemi...ukawa haijashinda kihivyo unakuza tu .kupata mitaa miwili kati ya mitaa 250 ya ccm sio ushindi bali ni kujikongoja..subiri matokeo kamili acha kurauka
Leo hapa Lumumba hakukaliki.Hakusemeki jema. Hasira zimetanda. Nyaraka kalikali zinapita kutoka huku kwenda kule. Ofisi zetu hapa leo zinakuwa chungu.Kisa,UKAWA kushinda vijijini na kwenye ngome za CCM kama Monduli. Makada wanalaumiana,vikao visivyoisha.Lakini,ni vikao kwa kukalishwa na si kukaa.Kukalishwa na kusimangwa. Kukemewa. Kushambuliwa.

Inasemwa hapa kuwa lengo la CCM halijatimia.Iitakiwa CCM ishinde kwa asilimia 90. Hadi sasa,hali ni tete.Mikoa yetu tuliyokuwa tunaitegemea imetuangusha. Majimbo yetu yaliyokuwa imara,yamesambaratika. Wabunge wetu wanaojitutumua Bungeni kama majembe ya chama, hawajasaidia kupatikana asilimia 90. Mambo ni shaghalabaghala. Mchafukoge!

Kambi za Urais na Escrow zinatajwa kama sababu kuu. Ziara za Katibu Mkuu wa chama nazo zinapondwa kwa kukosa matunda ya maana. Hakuna pa kushika,hakuna wa kumtupia lawama za moja kwa moja. Lakini,wakuu wanamtafuta wa kumwangushia 'jumba bovu'.Mchawi wa matokeo haya.

Kwani ni dhambi wapinzani kushinda vijijini na kwenye ngome za CCM?

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
 
Ziara za kinana na nape niza kuwahadaa wananchi..imagine wanapiga pocha wakiendesha mitumbwi, mara wakikifanya wana jenga wanapiga picha wakibeba tofali au wakilima au wakipanda treni yaani usanii mtupu.sasa matunda yake ndio hayoo mtabakia ma mapingamizi
 
Ziara za kinana na nape niza kuwahadaa wananchi..imagine wanapiga pocha wakiendesha mitumbwi, mara wakikifanya wana jenga wanapiga picha wakibeba tofali au wakilima au wakipanda treni yaani usanii mtupu.sasa matunda yake ndio hayoo mtabakia ma mapingamizi
Hao wamewapiga hela management yao, unajua wametafuta namna ya kupiga hela.
 
Matokeo yatatolewa lini?

Hujakosea Matokeo ya ujumla mmeshinda .. LAKINI ... NDIO MATEGEMEO YENU.

PILI Kiujumla Mmefanikiwa zaidi ... linganisha kabla ya uchaguzi na baada ya uchaguzi. ?

Fasta ...Lete jibu kamili hapa. NB hakuna manunguniko na visingizio.

Bottom line mmepigika. Tulieni Maumivu Yapitishe dawa kwenye misuli.
 
Katika overall performance naamini CCM itakuwa juu dhidi ya vyama vya upinzani. Muda si mrefu mtamsikia Mheshimiwa katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hiki kinachosemekana kinatafuta mchawi akijitutumua kwamba "tumepata ushindi wa kishindo" dhidi ya wapinzani. Lakini hawezi kwenda mbali zaidi kwa namna yoyote na kueleza wameshuka kwa kiasi gani. Kwa hiyo hata kama CCM watapata viti vingi zaidi ukweli ni kwamba imeshuka kiwango na kuaminika kwake kwa kiasi kikubwa sana kwa sababu viti vingi vya uenyekiti na ujumbe wa mtaa/ vijiji walivyokuwa navyo navyo sasa vimechukuliwa na upinzani.

Kwa upinzani hii ni nafasi nzuri zaidi ya kuendelea kuonyesha imani yao kwa wananchi na kuendelea kufikisha elimu katika maeneo ambayo wananchi "hawajajitambua". Na wapinzani nao kama kuna kiti mmepoteza katika kijiji au mtaa wowote ni wakati mzuri wa kutafakari "ni kwa nini" kabla ya uchaguzi mkuu wa 2015 ambao tunategemea hata kama hamtashinda nafasi ya urais basi tupate idadi kubwa zaidi ya wabunge na madiwani.
 
Huu ni mwanzo, bado tutawanyongea chini na katiba yenu ya CCM hapo April na kuwaua kabisa itapofika October

Kwa haya mamb niliyo yashuhudia Kyela kwa CCM kupigwa kama mbwa mwizi nakuhakikishia mkuu HAKUNA KURA ZA MAONI za KATIBA MPYA April 2015~

Kuna kijana ana miaka 19 kashinda uenyekiti wa Kijiji Kyela anaitwa Timth Kimwaga,huyu kijana kila mkutan yy alikuwa anamshambulia Mwakyembe tu kwa kukana maandiko yake kuhusu serikali tatu wakati anachukua PhD yake!

Katiba mpya hii Kyela inayo husishwa na Chenge mla rushwa HAIWEZI pita Mbeya!!
 
Unapogangwa ni vema na ni busara ... kuvumilia uchungu wa sindano kwani kusema kweli .. ni dawa tu .. dawa inaingia.

Tulieni Vumilieni ... Taifa linapona.

wewe daktari kabisa maana ushauri wako uliotukuka umekaa kisomi kweli kweli
 
Ziara za Katibu Mkuu wa chama nazo zinapondwa kwa kukosa matunda ya maana.
Ulitegemea kura zitapatikane wapi kwa mbinu kama hizi zilizopitwa na wakati.

th
 
Unafiki tu...

Haya ndio maneno yaliyobaki mdomoni mwako, pole sana tena mshukuru mbinu mliotumia ya uandikishaji wa siri na mapingamizi ya hovyo


wapi bibi yako FaizaFoxy aje akusaidie
 
Last edited by a moderator:
Jambo ambalo naweza nikalisema ni kwamba watanzania wameanza kujitambua.
 
Kahama Chadema
 

Attachments

  • 1418628395354.jpg
    1418628395354.jpg
    52.8 KB · Views: 723
ukombozi wa mtanzania dhidi ya utawala mbovu umewasili sasa. Shime Watz hakuna kurudi nyuma. ni wajibu wetu kuikomboa na kuiweka upya nchi yetu. tuna safari ndefu ya kuifanya nchi hii iwe na viongozi wawajibaki kwa wananchi. ila safari ndio tumeianza na tunaenda vyema. tusimamie mafanikiio haya madogo na tuzidi kwenda mbele. Kuna kila la kheri huko mbele mradi tusitetereshwe kwa namna yoyote ile. People....
 
Back
Top Bottom