The lost
JF-Expert Member
- Jul 3, 2017
- 2,695
- 8,209
Ni mambo ya hovyo sana, na yalianza awamu ya tano na awamu ya sita wanayatenda. Kwao mwenyekiti kwanza, then chama halafu masilahi ya nchi na wananchi baadae. Kimekuwa chama cha hovyo kinachokumbatia na kuabudu ukuu wa mwenyekiti wa chama kuliko utaifa wetu. Chama hiki hakina tena tofauti na CCP cha China, chama cha kikomust cha North korea. Lakini pia kimekumbatia sera za hovyo za kutoheshimu utu na mawazo ya wengine. Chama hiki hakiamini katika majadiliano tena ya kisiasa na mazungumzo bali kinaamini katika dola na matumizi ya nguvu.