CCM Kukubali Mjadala Katiba Mpya, Tumpongeze Rais Samia

benzemah

JF-Expert Member
Nov 19, 2014
1,503
2,980
Wakati fulani mwaka 2018, aliyekuwa rais wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli akizungumza katika kongamano la kujadili hali ya siasa na uchumi alisema

"SERIKALI YAKE HAINA MPANGO WA KUANZISHA UPYA MCHAKATO WA MAGEUZI YA KIKATIBA KWA SABABU KUNA MASUALA MENGINE YENYE KIPAUMBELEKWA SERIKALI"

Rais Magufuli alisema wazi kuwa hategemei kutenga fedha kwa ajili ya watu kula wakakae bungeni kujadili katiba, na akasisitiza kuwa hata kama kuna mtu (Wahisani) wako tayari kuipa Tanzania fedha kwa ajili ya mchakato wa Katiba basi pesa hizo zitolewe zikajenge Reli.

Huo ndio ulikuwa msimamo wa Hayati Dkt Magufuli ambapo ni dhahiri kuwa aliamini Katiba sio mwarubaini wa kila kitu

Miaka takribani Minne baadae, mwaka 2022, Rais Samia Suluhu Hassan anafanya kila jitihada kurejesha hali ya utengamano wa Kitaifa. Amekutana na makundi mbalimbali wakiwemo viongozi wa vyama vya upinzani ambao wengine walikimbia nchi na wengine walikuwa gerezani

Kubwa zaidi ni utayari wake wa kuruhusu mawanda ya kidemokrasia kuendelea kutanuka pamoja na Serikali na Chama chake CCM kuweka wazi kuwa milango ya mchakato wa kupata Katiba Mpya iko wazi hivyo kwa sasa itafutwe namna bora ya kufufua mchakato wa kupata katiba mpya ambao ulianza mwaka 2011 na kukwama mwaka 2014

Pamoja na mengi lakini kwa hili Rais Samia Suluhu Hassan anastahili pongezi kwani ni wazi angeweza kuwa na maamuzi kama ya mtangulizi wake lakini yeye ameamua kuruhusu kuanza kwa mchakato huu muhimu kwa Taifa na ni matumaini yetu, Serikali ya awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu, itatupatia Katiba Mpya Watanznia.

Mungu Ibariki Tanzania.
Samia-Suluhu-Hassan-Address.jpeg
 
Mimi naomba tu kuchukua nafasi hii kujipongeza baadhi yetu humu jukwaani kwa kupaza sauti zetu, ingawa kuna wakati tulikejeliwa na PRO CCM.

Lakini pia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Kiukweli na wenyewe wamejitahidi sana kusimama kwa niaba ya Watanzania wanaotaka uwepo wa Katiba Mpya.

Mwisho kabisa nimshukuru Rais wa sasa kwa usikivu wake, kiasi cha kukubali hoja za baadhi ya Watanzania wanaotaka Katiba Mpya. Kiukweli na yeye pia anastahili pongezi. Na iwapo atatanguliza maslahi ya Taifa mbele, basi ajiandae tu kuingia kwenye historia ya kuwa Rais msikivu kuwahi kutokea nchini.

Rai yangu: Rais Samia atengeneze mazingira yatakayo zuia makundi ya kisiasa kuuteka huu mchakato wa kupatikana kwa Katiba Bora kama ilivyokuwa kipindi kile kati ccm vs ukawa. Yaani Katiba iwe na manufaa kwa Watanzania wote! Na siyo kikundi cha watu wachache! Isiwe katiba ya ccm, Chadema, au watu fulani! Iwe ni Katiba ya Watanzania wote.


Tunataka Katiba itakayolinda raslimali zetu, kwa manufaa ya kizazi cha sasa na pia kizazi kijacho!, nk.
 
Wakati fulani mwaka 2018, aliyekuwa rais wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli akizungumza katika kongamano la kujadili hali ya siasa na uchumi alisema

"SERIKALI YAKE HAINA MPANGO WA KUANZISHA UPYA MCHAKATO WA MAGEUZI YA KIKATIBA KWA SABABU KUNA MASUALA MENGINE YENYE KIPAUMBELEKWA SERIKALI"

Rais Magufuli alisema wazi kuwa hategemei kutenga fedha kwa ajili ya watu kula wakakae bungeni kujadili katiba, na akasisitiza kuwa hata kama kuna mtu (Wahisani) wako tayari kuipa Tanzania fedha kwa ajili ya mchakato wa Katiba basi pesa hizo zitolewe zikajenge Reli.

Huo ndio ulikuwa msimamo wa Hayati Dkt Magufuli ambapo ni dhahiri kuwa aliamini Katiba sio mwarubaini wa kila kitu

Miaka takribani Minne baadae, mwaka 2022, Rais Samia Suluhu Hassan anafanya kila jitihada kurejesha hali ya utengamano wa Kitaifa. Amekutana na makundi mbalimbali wakiwemo viongozi wa vyama vya upinzani ambao wengine walikimbia nchi na wengine walikuwa gerezani

Kubwa zaidi ni utayari wake wa kuruhusu mawanda ya kidemokrasia kuendelea kutanuka pamoja na Serikali na Chama chake CCM kuweka wazi kuwa milango ya mchakato wa kupata Katiba Mpya iko wazi hivyo kwa sasa itafutwe namna bora ya kufufua mchakato wa kupata katiba mpya ambao ulianza mwaka 2011 na kukwama mwaka 2014

Pamoja na mengi lakini kwa hili Rais Samia Suluhu Hassan anastahili pongezi kwani ni wazi angeweza kuwa na maamuzi kama ya mtangulizi wake lakini yeye ameamua kuruhusu kuanza kwa mchakato huu muhimu kwa Taifa na ni matumaini yetu, Serikali ya awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu, itatupatia Katiba Mpya Watanznia.

Mungu Ibariki Tanzania.
View attachment 2269674
Rais Samia ni wa kupongezwa sana sana.

Amekonga nyoyo za watanzania.
 
Wakati fulani mwaka 2018, aliyekuwa rais wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli akizungumza katika kongamano la kujadili hali ya siasa na uchumi alisema

"SERIKALI YAKE HAINA MPANGO WA KUANZISHA UPYA MCHAKATO WA MAGEUZI YA KIKATIBA KWA SABABU KUNA MASUALA MENGINE YENYE KIPAUMBELEKWA SERIKALI"

Rais Magufuli alisema wazi kuwa hategemei kutenga fedha kwa ajili ya watu kula wakakae bungeni kujadili katiba, na akasisitiza kuwa hata kama kuna mtu (Wahisani) wako tayari kuipa Tanzania fedha kwa ajili ya mchakato wa Katiba basi pesa hizo zitolewe zikajenge Reli.

Huo ndio ulikuwa msimamo wa Hayati Dkt Magufuli ambapo ni dhahiri kuwa aliamini Katiba sio mwarubaini wa kila kitu

Miaka takribani Minne baadae, mwaka 2022, Rais Samia Suluhu Hassan anafanya kila jitihada kurejesha hali ya utengamano wa Kitaifa. Amekutana na makundi mbalimbali wakiwemo viongozi wa vyama vya upinzani ambao wengine walikimbia nchi na wengine walikuwa gerezani

Kubwa zaidi ni utayari wake wa kuruhusu mawanda ya kidemokrasia kuendelea kutanuka pamoja na Serikali na Chama chake CCM kuweka wazi kuwa milango ya mchakato wa kupata Katiba Mpya iko wazi hivyo kwa sasa itafutwe namna bora ya kufufua mchakato wa kupata katiba mpya ambao ulianza mwaka 2011 na kukwama mwaka 2014

Pamoja na mengi lakini kwa hili Rais Samia Suluhu Hassan anastahili pongezi kwani ni wazi angeweza kuwa na maamuzi kama ya mtangulizi wake lakini yeye ameamua kuruhusu kuanza kwa mchakato huu muhimu kwa Taifa na ni matumaini yetu, Serikali ya awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu, itatupatia Katiba Mpya Watanznia.

Mungu Ibariki Tanzania.
View attachment 2269674
Hilo ni balaa sawa na balaa lingine tu, katiba ya nchi haiwezi kutegemea CCM ikubali au ikatae. Good is good by itself. kama kuwa na katiba mpya ni muhimu itakuwa muhimu hata kama CCM haipendi
 
Hizo zinaenda kuliwa tu na katiba haitapatikana tatizo la chadema akili zao ni kama za panzi wanasahau haraka sana
 
Nina wasiwasi na hiyo Katiba Mpya itakayokuja kama kweli itaweka uwanja sawa wa kisiasa kwa vyama, ili hili lifanyike naamini Samia kwanza anatakiwa kupunguza ile mihemko yake ya ni zamu ya mwanamke 2025, iliyowaondoa kina Lukuvi wizarani.

Lakini kama bado anayo hiyo mihemko, hakuna chochote cha maana kitakachofanyika, ni maigizo matupu na kupoteza pesa za walipa kodi kama ilivyotokea kwa "mentor" wake JK.
 
Hii katuni inaweza kuwa na ukweli.

Mwaka jana Maza alidai kuwa katiba Tusubiri kwanza kwa kuwa ana rekebisha uchumi kwanza.

Alipowahutubia kikosi kazi alidai anawapa ajira ya miaka 9 ili waje na katiba mpya kama walivyopendekeza kuwa mchakato uanze baada ya 2025.

Sasa kilichobadirisha mawazo yake ni kipi. Nita amini tu siku nikiona mchakato umeanza.
 
Hilo ni balaa sawa na balaa lingine tu, katiba ya nchi haiwezi kutegemea CCM ikubali au ikatae. Good is good by itself. kama kuwa na katiba mpya ni muhimu itakuwa muhimu hata kama CCM haipendi
Ni mtazamo wako na ninauheshimu
 
Mimi naomba tu kuchukua nafasi hii kujipongeza baadhi yetu humu jukwaani kwa kupaza sauti zetu, ingawa kuna wakati tulikejeliwa na PRO CCM.

Lakini pia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Kiukweli na wenyewe wamejitahidi sana kusimama kwa niaba ya Watanzania wanaotaka uwepo wa Katiba Mpya.

Mwisho kabisa nimshukuru Rais wa sasa kwa usikivu wake, kiasi cha kukubali hoja za baadhi ya Watanzania wanaotaka Katiba Mpya. Kiukweli na yeye pia anastahili pongezi. Na iwapo atatanguliza maslahi ya Taifa mbele, basi ajiandae tu kuingia kwenye historia ya kuwa Rais msikivu kuwahi kutokea nchini.

Rai yangu: Rais Samia atengeneze mazingira yatakayo zuia makundi ya kisiasa kuuteka huu mchakato wa kupatikana kwa Katiba Bora kama ilivyokuwa kipindi kile kati ccm vs ukawa. Yaani Katiba iwe na manufaa kwa Watanzania wote! Na siyo kikundi cha watu wachache! Isiwe katiba ya ccm, Chadema, au watu fulani! Iwe ni Katiba ya Watanzania wote.


Tunataka Katiba itakayolinda raslimali zetu, kwa manufaa ya kizazi cha sasa na pia kizazi kijacho!, nk.
Umenena vyema
 
Nina wasiwasi na hiyo Katiba Mpya itakayokuja kama kweli itaweka uwanja sawa wa kisiasa kwa vyama, ili hili lifanyike naamini Samia kwanza anatakiwa kupunguza ile mihemko yake ya ni zamu ya mwanamke 2025, iliyowaondoa kina Lukuvi wizarani.

Lakini kama bado anayo hiyo mihemko, hakuna chochote cha maana kitakachofanyika, ni maigizo matupu na kupoteza pesa za walipa kodi kama ilivyotokea kwa "mentor" wake JK.
Nadhani hapa kwanza wewe punguza mihemko ili ufikiri kuandika vyema na sio kwa mihemko
 
Nina wasiwasi na hiyo Katiba Mpya itakayokuja kama kweli itaweka uwanja sawa wa kisiasa kwa vyama, ili hili lifanyike naamini Samia kwanza anatakiwa kupunguza ile mihemko yake ya ni zamu ya mwanamke 2025, iliyowaondoa kina Lukuvi wizarani.

Lakini kama bado anayo hiyo mihemko, hakuna chochote cha maana kitakachofanyika, ni maigizo matupu na kupoteza pesa za walipa kodi kama ilivyotokea kwa "mentor" wake JK.
Katiba ni mali ya wananchi na italetwa na wananchi pamoja na wewe, sio Rais samia, usipange kulaumu wengine kama katiba safi isipopatikana. Kila mtu (sio chadema wala ACT wala CCM) lazima awe na kitu anachopenda katiba iwe nacho au isiwe nacho na ahakikishe kuwa anachokitaka kimo au asichokitaka hakimo, sio kulalamika tu.
 
Hii katuni inaweza kuwa na ukweli.

Mwaka jana Maza alidai kuwa katiba Tusubiri kwanza kwa kuwa ana rekebisha uchumi kwanza.

Alipowahutubia kikosi kazi alidai anawapa ajira ya miaka 9 ili waje na katiba mpya kama walivyopendekeza kuwa mchakato uanze baada ya 2025.

Sasa kilichobadirisha mawazo yake ni kipi. Nita amini tu siku nikiona mchakato umeanza.
"ALIDAI ANAWAPA AJIRA YA MIAKA 9"............... Hili umelitoa wapi
 
Katiba ni mali ya wananchi na italetwa na wananchi pamoja na wewe, sio Rais samia, usipange kulaumu wengine kama katiba safi isipopatikana. Kila mtu (sio chadema wala ACT wala CCM) lazima awe na kitu anachopenda katiba iwe nacho au isiwe nacho na ahakikishe kuwa anachokitaka kimo au asichokitaka hakimo, sio kulalamika tu.
Wengi wanaodai katiba mpya hawajui wanataka iwe na nini
 
Back
Top Bottom