Genekai
R I P
- Feb 9, 2010
- 12,514
- 5,003
Uko wapi sasa Juliana Shonza? Rudi ujitetee kwenye uzi wako manake "MMETAGA" Arusha tena 4:0, unadhani wanadanganyika kule?
hawa magamba lazima wakimbie nami niliwaambia tangu asubuhi, yuko wapi Ritz, HAMY-D, ifweero, masopakyindi na Simiyu yetu!
Leo Chadema wataiona Arusha kama motoni watu wamechoka kuwa mateka wa Lema.
Wanaojilipua Arusha ni wale waliokataliwa na wananchi.Kuna uzi unaletwa humu muda si mrefu kwa ajili ya malalamiko,si unajua tena hawa jamaa ni watu wa kutafuta kinga mapema,na leo wamedhibitiwa hawataweza kulipua mabomu yao ili uchaguzi uhairishwe tena.
Ndugu wana jamvi,hatimaye siku na saa watanzania tulikuwa tunasubili kwa hamu ili kuweza kujua nani ataibuka kidedea katika kata nne zinazofanya uchaguzi leo jijini Arusha kwa maana ya kata ya Erelai, Kimandolu, Themi na Kaloleni.
Wana jamvi waswahili wanasema dalili ya mvua ni mawingu ,na hofu ni ishara ya woga wa kushindwa,ni wazi chadema wameingiwa na hofu kubwa baada yakuona kuna uwezekano mkubwa wakupoteza kata nne za jiji la Arusha mkoa ambao wamekuwa wakijinasibu kuwa ndiko kiliko kitovu cha chadema.
Hofu hiyo inatokana na kugundua kwamba wananchi wa Arusha wamechoka kuona mkoa wao ukigeuzwa kuwa uwanja wa mapambano na umwagaji damu kwa ajili ya maslahi ya watu wachache.
Hivyo basi ni wazi sasa chadema wamejichimbia kabuli wenyewe kwakutokujali misingi ya utawala bora inayosema kiongozi ni mali ya wananchi ila mwanachama ni mali ya chama wao wakakiuka misingi hiyo na kuamua kufukuza madiwani wao kwa maslahi ya watu wachache.
Ni wazi sasa CCM inaenda kuibuka kidedea na kushinda kwa kishindo katika kata zote nne kwa namna ilivyojipambanua kwa sera zake kipindi cha kampeni na wananchi hasa vijana kuanza kuelewa tofauti iliyopo kati ya chama maslahi jamii(CCM)na chama maslahi binafsi(chadema)
Viva ccm,umoja ni ushindi.
Juliana Shonza huko ulipotea njia,rudi CHADEMA
Chama cha demokrasia na maendeleo,huyu Juliana Shonza hajitambui leo kaja thread eti CCM itashinda,sijui ana Akili kweli huyu binti?wamekutana na MwiguluArudi chadema ipi Mkuu?
Hivi chadema mlikosa watu wa kuwapa uongozi hadi mkampaga huyu mtu nafasi ya uongozi kwenye chama chenu kabla hamja mtimua? jamani jamani jamani,hata kuandika imekua tabu? hata jipendekeze vipi kwenye chama chetu haupati nafasi yoyote ya uongozi,kwanza wewe ni mamluki wa chadema
Asubuhi kwenye majira ya asubuhi ulitangaza hapa Jamii forum kwamba CDM wameshindwa vibaya na CCM imepata ushindi wa kishindo.
1.Je ulimaanisha uchaguzi huu wa madiwani Arusha au mwingine?
Kama ni uchaguzi huu uombe radhi wanajamii forum kwa kupotosha.
2.Kama ulivyofukuzwa chadema kwa matokeo haya CCM hawatawabakiza wewe na Nchemba.Utahamia chama gani sasa?