Juliana Shonza
JF-Expert Member
- Dec 19, 2012
- 2,009
- 1,607
Ndugu wana jamvi,hatimaye siku na saa watanzania tulikuwa tunasubili kwa hamu ili kuweza kujua nani ataibuka kidedea katika kata nne zinazofanya uchaguzi leo jijini Arusha kwa maana ya kata ya Erelai, Kimandolu, Themi na Kaloleni.
Wana jamvi waswahili wanasema dalili ya mvua ni mawingu ,na hofu ni ishara ya woga wa kushindwa,ni wazi chadema wameingiwa na hofu kubwa baada yakuona kuna uwezekano mkubwa wakupoteza kata nne za jiji la Arusha mkoa ambao wamekuwa wakijinasibu kuwa ndiko kiliko kitovu cha chadema.
Hofu hiyo inatokana na kugundua kwamba wananchi wa Arusha wamechoka kuona mkoa wao ukigeuzwa kuwa uwanja wa mapambano na umwagaji damu kwa ajili ya maslahi ya watu wachache.
Hivyo basi ni wazi sasa chadema wamejichimbia kabuli wenyewe kwakutokujali misingi ya utawala bora inayosema kiongozi ni mali ya wananchi ila mwanachama ni mali ya chama wao wakakiuka misingi hiyo na kuamua kufukuza madiwani wao kwa maslahi ya watu wachache.
Ni wazi sasa CCM inaenda kuibuka kidedea na kushinda kwa kishindo katika kata zote nne kwa namna ilivyojipambanua kwa sera zake kipindi cha kampeni na wananchi hasa vijana kuanza kuelewa tofauti iliyopo kati ya chama maslahi jamii(CCM)na chama maslahi binafsi(chadema)
Viva ccm,umoja ni ushindi.
Wana jamvi waswahili wanasema dalili ya mvua ni mawingu ,na hofu ni ishara ya woga wa kushindwa,ni wazi chadema wameingiwa na hofu kubwa baada yakuona kuna uwezekano mkubwa wakupoteza kata nne za jiji la Arusha mkoa ambao wamekuwa wakijinasibu kuwa ndiko kiliko kitovu cha chadema.
Hofu hiyo inatokana na kugundua kwamba wananchi wa Arusha wamechoka kuona mkoa wao ukigeuzwa kuwa uwanja wa mapambano na umwagaji damu kwa ajili ya maslahi ya watu wachache.
Hivyo basi ni wazi sasa chadema wamejichimbia kabuli wenyewe kwakutokujali misingi ya utawala bora inayosema kiongozi ni mali ya wananchi ila mwanachama ni mali ya chama wao wakakiuka misingi hiyo na kuamua kufukuza madiwani wao kwa maslahi ya watu wachache.
Ni wazi sasa CCM inaenda kuibuka kidedea na kushinda kwa kishindo katika kata zote nne kwa namna ilivyojipambanua kwa sera zake kipindi cha kampeni na wananchi hasa vijana kuanza kuelewa tofauti iliyopo kati ya chama maslahi jamii(CCM)na chama maslahi binafsi(chadema)
Viva ccm,umoja ni ushindi.