Tanira napata tabu kujibizana na watu walioficha jina unaweza jibizana na jini. Pili napata tabu kuongelea majina maana sio hoja yenye kuongeza tija. Ninachoona umekaririshwa vitu usivyojua. Kinyumbani kuna majina ya ukoo ambayo hata usipotumia yapo tu mfano mwanangu yeyote wa kiume ni kitundu hata wawe kumi na wa kike msua kwa ukoo ila wanakuwa na majina yao hivi yuko Joshua na Gracoius. Mimi na kaka zangu wote ni shumbi, dada zetu ntulu halafu tunakuwa na majina yetu, halafu baba mkubwa, mdogo na baba wote ni mkumbo dada zao kilie halafu wanakuwa na majina yao. Sasa jina la machungani niliitwa mwigullu, au mgulo au mbaga nilipopelekwa cliniki nikapewa majina ya mganga wa zahanati ya mkulu aliyekuwa akiitwa Lameck. Kuna upuuzi umekuwa ukiaminishwa kuwa mimi sikufaulu badala yake nilinunua jina la mtu aliyefaulu. Si kweli. Nilifanya mtihani tena na picha nilipiga. Hii mkumbo unayotafuta haiwezionekana kama ilivyo kitundu ilivyo kwa mwanangu utasikia akiitwa tu Joshua. Ukirudi Meatu hawa wanangu wakike wataitwa Ng'washi kisukuma. Uliza kwa wanyiramba kabla ya kuona hii ni hoja.