CCM Imechokwa, CHADEMA Haijajipanga!

Hivi wewe ni Dr W Slaa wa ukweli au jamaa kaamua ku2mia jina la m2?Kama wewe n slaa nahc kuzimia kila kila nikilimnna jna lako najua pamoja 2naweza kukijenga chama che2 chadema mungu akupe afya tere 2015 ni ye2
 
Pasco

Ulichoandika ndio mtazamo wa majority wa laymen huku mtaani; ila majibu ya slaa yameonyesha facts na logic ya yanayotokea, ili kujenga pale ulipoanzia nadhani ni vizuri kwa Dr. kupata forum ya kueleza haya ili jamii iyajue, kwa mfumo wetu tanzania, waishio by the book ni less than 20% (sina confirmed data lakini CI siyo mbaya). Hii inatokana na historia yetu na culture yetu

Cha pili kwako Pasco: Hawa jamaa wanakuja na part II ya albam iliyohit ya uchaguzi, subiri utagundua wanataka kufanya nini

Kwako dr. Slaa, awamu ya pili ianze sasa msicheleweshe sana
 
wakuu mimi sina technical language kama za Dr Slaa na Pasco ila sina imani na Zitto kama ana upinzani halisi, hasa baada ya kuteuliwa kuwepo kwenye tume ya madini na kauli zake juu ya mitambo ya dowans na pia kuifagilia ccm pasipostahili, he's a ccm member in disguise-Lyatonga type! Hivyo, aspewe uongozi wa juu wa upinzani ndani ya bunge!
 
Hebu tuangalie ulivyoanza........................


Ok thats your opinion

Mbowe sio born leader, ni made leader, tena ameletewa uongozi kwenye kisaani cha chai. Zitto ni born leader na amepambana kufika hapo alipofika......

mmmh ...........halafu ukatoa conclusion kama hii


yaani kwa kuwa Mbowe ni "made leader"..........na Zitto ni "born leader"..........kwa hiyo ndio kigezo cha kuona Zitto ni zaidi ya Mbowe?


Mwishoni ukatoa ANGALIZO kuwa wewe ni Political analyst ambaye ni Objective...............Dr. W. Slaa akasema hivi


wewe ukaja kusema hivi.............


Only your observation!!......................ni kweli ulichoandika ni ulicho-observe ukiwa Dodoma........na mambo mengine................HOWEVER ukatuwekea ANGALIZO kuwa wewe ni Political analyst..........hiyo statememnt nzito na hata mtu anaposoma post zako anakuangalia kwa uzito huo................kw ahiyo majibu na maswali ya Dr. Slaa ni sahihi kabisa na hukutakiwa kujibu kirahisi namna hiyo........"observation"...with angalizo kuwa wewe ni Political analyst ambaye yuko objective....................

ulipomjibi Dr. Slaa kwamba jicho lako ni similar to lile la mwananchi wa kijijini na sio .........."researcher as member of academia"........una imply nini?........je una-imply alivyokujibu Dr. Slaa ni kwa mlengo wa research inayofanywa na Academician........jibu ambalo wengi wetu tunatambua unakotaka kuelekea.............you simply want to tell us kuwa jibu la Dr Slaa liko academic zaidi kuliko reality................then Mkuu Pasco kwa ufupi ukiondoa hilo angalizo lako..............then observation yako ni sahihi...........
 

Hivyo ndiyo nilivyosema.
 

Ogah, asante, nimekusikia na maoni yako, nayafanyia kazi.
Pasco.
 

naomba kama political analyst utuambie nini kilipelekea chadema kuunda kambi ya upinzani based on facts na sio kwa hisia za personalities kama ulivyo fanya kwemnye mada nzuri sana na kuipunguzi credibility kwa kiwango kikubwa.

Taarifa katika vyombo vya habari zinaonyesha kuwa mbowe aliawaalika cuf katika majadiliano ya kumpata spika na uundwaji wa kambi ya upinzani. Taarifa za awali katika vyombo vya habari hamad rashid alikubali. Lakini baadaye msimamo wa cuf ulipotolewa ikaonekjana cuf haiko tayari kushirikina na chadema hata kidogo katika mambo hayo mawili.

Cha kushangaza baada ya chadema kupoteza nafasi ya uspika kauli za hamda rashidi zinzonyesha kuwa cuf ipo tayari kushuirikiana na chadema, je hauoni kuwa nguvu ya fedha za mafisadi katika kinyang'anyiro cha uspika ndio kilisababisha vyama hivi visishirikiane badala ya ubinafsi wa viongozi wa chadema kaka unavyodai?
 
So far nadhani kamanda Mbowe amefanya kazi nzuri sana, na Zitto nae tunamhitaji achape mzigo lakini Ishu kama ile ya Dowans kusema kweli ilinisikitisha jinsi alivyokuwa akiipigia debe.

Nakubaliana na analysis kwamba Zitto bado anahitaji kuonesha kwamba amekomaa na ni kweli ni mwanamageuzi, na hana tamaa na umimi. mbali ya suala la Dowans, nilishtushwa wakati wa kampeni pale alipotangaza nia yake ya kugombea urais mwaka 2015! sijaelewa bado nia yake ilikuwa ni nini. badala ya kutumia ile platform kumjenga mgombea urais wa chama chake mwaka huu 2010, alitumia muda mwingi kujijenga mwenyewe sio kwenye ubunge, bali kwenye urais! hii inanisadikisha kwamba Zitto ana upungufu fulani mkubwa ambao sina hakika kama dawa yake ni time.
 

Mkuu wewe badala ya kujibu hoja zilizoongelewa na Dr wa ukweli unaanzisha hoja nyingine ndani ya hoja. Suala la Dr Slaa kutokuhudhuria kuapiswa kwa "rais" ameshalitolea ufafanuzi na kama hujaridhika ungeweza kuanzisha thread nyingine. Huu utaratibu wako wa kuibua hoja ndani ya hoja kwa sababu umeshindwa kujibu hoja unanipa mashaka sana kama kweli wewe ni independent analyst
 


Asante sana Dr. Slaa kwa maelezo mazuri na uchambuzi mwanana. Kwa hata mimi sijaona analysis yoyote aliyofanya huyo jamaa aliyetoa hoja. Badala yake, maelezo yake yamejaa feelings and emotions!!!!! Sioni hata uhalali wa yeye kujitangaza kama political analyst.

Kwa faida ya wengine wenye mtazamo kama wa kwake, ningependa tukumbushane kuwa dhana ya ubinafsi CHADEMA mimi huwa naitazama kama inapandikizwa na watu kwa sababu wanazozijua wenyewe. Mlolongo wa uongozi ndani ya CHADEMA kwa maoni yangu umekuwa ni mzuri na usio na ubinafsi. Mathalani, Wenyeviti wamepokezana pasipo hata mgogoro kama ilivyo kwa vyama vingine: Kutoka kwa Mtei, kuja kwa Bob Makani, then Freeman Mbowe. Vilevile Makatibu waku, Bob Makani, Dr. Slaa. Isitoshe, watu kutoka maeneo mbalimbali wameshika nafasi za juu CHADEMA pasipo ubaguzi wowote, miongoni mwao ni Walid Kaborou (Kigoma), Barongo (Ruvuma), Zitto (Kigoma), Tundu Lissu (Singida), Said Arfi (Rukwa), Anna Komu (Zbar -kama sikosei) etc.

Si vyema kupokea jambo na kuliamini kama lilivyo bila kuchanganua!!!!!
 
PASCO, naomba usiendelee kujiaibisha kwa kujiita Political Analyst or whatever kind of Analyst. You don't deserve at all. Usipende kujibebesha sifa ambazo huna!!!!!! Maelezo na michango yako haina tofauti sana na ya layman.
 
Napenda kutoa angalizo moja kuhusu watu ambao wanataka uongozi kwanza (Mr. Ema). Tumeshuhudia kwamba umaarufu wa vyama alivyoongoza Mr. Ema ulikua ukishuka siku kwa siku pale suala la uongozi lilipowadia na yeye daima kwa maoni yake mwenyewe alitaka daima awe mwenyekiti. Sasa basi kama Mh Zitto ni maarufu aendelee kuutumia umaarufu huu kwa manufaa ya wananchi na chama pia, Chadema nimekkuwa nikiiheshimu sana pia kwa system yao ya uongozi, toka enzi za kina Bob Makani na mzee Mtei na ninaamini wataendeleza hili. Pia nina imani kubwa kijana mwenzangu zitto utafika muda wake katika hili.
-Pia kama kuna mamluki yeyote amejificha chadema tunamuomba aondoke kwani ni kipindi ambacho Watanzania tunalilia mabadiliko ya kweli yenye dhamira ya kweli.
 
Hawa ndiyo mapolitical analyst wetu hapa bongo. Sidhani kama political analyst anaweza kutumwa na chama fulani kusafiri kutoka Dar kwenda Mwanza kwenda kum record Askofu mmoja aliyeamua kuingia kwenye siasa huku akiwatuhumu wenzie kuwa wameingia kwenye siasa na wanapendelea chama na mgombea fulani. Political nalyst lazima angejua mazara ya hii kitu kwa jamii na asinge kubali. Pili huyu political analyst hawezi kuaminiwa tena na vyama vingine kwa sababu yupo kwenye payroll ya chama kimojawapo na bila ya kukosea pengine haya maoni yake ni kumalizia change zilizobaki kwenye kazi ya kwanza ambayo vyombo vya TV viliiona kuwa ni hatari kwa taifa na kuishia kuchukua sehemu tu ya mahojiano hayo
 
hii topic/thread imesimama sana wajameni, am learning alot from u guys

thanx to u all and keep it cool
 

Post yako inareflect moja ya characteristics ya chadema ni kuficha mabaya na kuanika mazuri. Pasco katoa mawazo yake, maoni yake. Toa ya kwako bila kushambulia Pasco na kumpa mpa viushauri eti vya kuvuta subira badala ya kumshukuru kwa kutoa aliyoweza kuyatoa.
 
mkubwa umeonge..mi nilidhani naona pekeyangu..mbowe might be a mwenyekiti lakini zitto ni more powerful..kwakwel hapa hawakujipanga..na kingine suala la kushirikisha wapinzani wengine mi nadhani ni zuri, sometime waache misimamo isiyo na tija
 
Angalizo: Pasco wa Jamii Forums ni political commentator ambaye yuko objective, bila kuegemea chama chochote, upande wowote na hufanya kazi kwa wote, ila ni muumini wa demokrasia ya kweli ndani ya bunge for the balance of power, hivyo nashangilia sana kambi ya upinzani kuingiza vichwa 100 bungeni, ni matumaini yangu, 2015 kazi itakamilishwa!

Wanabodi, nimeshabadili angalizo kama linavyosomeka hapo, sio political analyst ni just political commentator!.
 
Shalom, Pasco wa Jamii forum amesharekebisha sio Political analyst any more, he is just a political commentator.
Ila pia anaweza akawa ameajiriwa mahali fulani, katika kutekeleza maagizo ya mwajiri wake, anaweza kumtumia yoyote as long as hiyo ndio mode ya maisha yake. To put records clear, hakuna senti tano ya chama chochote iliyotumika kumlipa Pasco huyu ili kusaidia chama chochote, bali Pasco huyu hufanya kazi kwa maslahi ya taifa, ndio maana amekiri wazi ni mshabiki wa demokrasia ndani ya bunge, na kupongeza wingi wa wabunge wa upinzani bungeni for the balance of power.
 
PASCO, naomba usiendelee kujiaibisha kwa kujiita Political Analyst or whatever kind of Analyst. You don't deserve at all. Usipende kujibebesha sifa ambazo huna!!!!!! Maelezo na michango yako haina tofauti sana na ya layman.
Matonange, kwanza karibu JF, pili nimeshabadili title yangu kama inavyosomeka hapa, ila pia ukweli mimi ni layman, I belong to the class of ma lumpen ploretariat.

Pasco wa Jamii Forums ni political commentator ambaye yuko objective, bila kuegemea chama chochote, upande wowote na hufanya kazi kwa wote, ila ni muumini wa demokrasia ya kweli ndani ya bunge for the balance of power, hivyo nashangilia sana kambi ya upinzani kuingiza vichwa 100 bungeni, ni matumaini yangu, 2015 kazi itakamilishwa!

Wanabodi, nimeshabadili angalizo kama linavyosomeka hapo, sio political analyst ni just political commentator!.
 
Rais wetu mtarajiwa Dr.Slaa umenikuna na ninakuahidi na watanzania ni mashihidi kuwa wanajua wewe ndio Rais wao mioyoni mwao,uendelee kutujuza mambo na kutupigania kwani tunaamini Marehemu Baba wa Taifa hili J.K.Nyerere amerudi kupitia kwako.Kwani Rais Mkapa aliliambia taifa kuwa alipozidiwa huko Saint bernad Hosp. alisema "huu ugonjwa hautaniachia lakini nitawaombea kwa mungu" sitasahau maneno haya na kwa wote wanaojisafisha leo bila kutubu kwa Mungu wakati wamechafuka sana wangesoma alama za nyakati kwa kurejea hosia wake.Slaa uko juu na Tanzania inakutegemea.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…