CCM amueni kati ya hawa wawili

CCM amueni kati ya hawa wawili

Mdahalo ulikuwa ni watia Nia wa CCM,Prof Muhongo ni mtia nia Wa CCM,na katika wote tuliambiwa kuwa ni Lowasa tu ndiye alitbibitisha kuwa hatahudhuria,Unaposema nijiulize kuwa kwanini hawakumwalika unataka kuniambia kuwa hakualikwa,we umejuaje kuwa hakualikwa? Angekuwa hajaalikwa bila shaka yangeorodheshwa majina ya watia nia walioalikwa.Otherwise uje na orodha ya walioalikwa na ambao hawakualikwa
Nilisoma humu humu majina wa watu waliokuwa wanatakiwa kushiriki na la Prof sikuliona, na waandaaji wakasema lowassa ndo amesema hatoshiriki. unapata picha gani hapo??
 
Duuh kweli siasa siasani kwa iyo hadi hapo umeshindwa kunithibitishia na utapiga kelele kumtuhumu mtu kwa nguvu zote????Okey ripoti ya pccb haiwezi kuwa public,ila baada ya kuchunguza wanaruhusiwa kupeleka kwa dpp ili kesi ipelekwe mahakamani, umesikia icho kitu labda hata pccb wakisema?????? kwa sababu wanasema tumechunguza kitu fulani na file lipo kwa dpp.
Take in mind MKE WA KAISARI HAPASWI KUTUHUMIWA
 
Nilisoma humu humu majina wa watu waliokuwa wanatakiwa kushiriki na la Prof sikuliona, na waandaaji wakasema lowassa ndo amesema hatoshiriki. unapata picha gani hapo??
Kama ni kweli unachoongea kipo sahihi nafuta kauli yangu ya kukimbia mdahalo.kuhusu kuwa kwanini hakualikwa may be wamemmarginalize,wanaassume hana effect kwenye huu mchakato.Hizo ni assumptions zangu lkn.
 
Lord denning

Nakupongeza kwa kubaini kuwa prof Muhongo ni kifaa ambacho kitaipeleka tz mbele. Kama tunataka maendeleo, Muhongo ndiyo mtu atakayetufaa, lakini kama tunataka siasa na visasi chagueni ed au bm. God bless our country to enable us to get a right person for our development.
 
Last edited by a moderator:
Nakupongeza kwa kubaini kuwa prof Muhongo ni kifaa ambacho kitaipeleka tz mbele. Kama tunataka maendeleo, Muhongo ndiyo mtu atakayetufaa, lakini kama tunataka siasa na visasi chagueni ed au bm. God bless our country to enable us to get a right person for our development.

Kama sijakosea, hivi si huyu Muongo, sorry Muhongo, wakati watanzania wenye uwezo walipimuomba washirikishwe katika biashara ya gesi akakataa na kuwakejeli kuwa watanzania wanauwezo tu wa kushiriki katika biashara za kuuza juice na njugu. Baadae akakimbilia Canada kusaini mikataba na wazungu. Sasa mtu kama huyu ambae hana sera za maksudi za kuwainua wazawa atawezaje kuwa Rais wao!!

Achana nae huyo. Kazoea kuwa boi wa wazungu. Hivi ile kazi yake ya kuangalia miamba duniani aliyopewa na wazungu baada ya kutimuliwa uwaziri imeishia wapi???
 
Unaweza kutransform kitu bila kuwa na idea ya kutransform? Tupe hiyo idea ya kutransform maana huwezi kutransform kitu ambacho hakipo

Hizo idea wamekuwa nazo kwa miaka mingi vichwani mwao, na wanapopata nafasi waoneshe sasa uwezo wao wa kuchambua mambo na kuyaweka kwa vitendo. hapo ndiyo unashangaa, tunabakia kuimba vibwagizo vya nguvu mpya ari mpya na kasi mpya basi - may be- kilimo kwanza -as if- hawakujua nini kipaumbele katika utumishi wao.

leo tunashuhudia hotuba nzuri zinazolenga moja kwa moja matatizo tulionayo katika jamii zetu, na mtu anakuambia hapa tulipo tufanye nini ili kutoka hapa, sasa hebu jiulize nani katufikisha hapa, maana wengin wapo serekalini tangu awamu ya kwanza hadi leo wamo. anawezaje leo kuwa na mawazo mapya yenye ufanisi??
na kama kweli yana ufanisi inakuwaje hakuyatumia tangu awali mpaka tukafika hapa, alisubiri tuharibikiwe ndiyo waje watoe hotuba za kututoa shimoni??

sitaki kuamini.

mungu ibariki Tanzania.
 
Huu upuuzi woooote ulioandika...ni kwa sababu umeona Urais ni kama ajira ya mtu mmoja, na sio taasisi. Hao uliowasema hata wakiwa na maonao kiasi gani....tambua ndio walewale waliokuwa wameuzunguka utawala uliopo....hawana jipya nao ni vibaka na wataendelea kuzungukwa na vibaka
 
Huu upuuzi woooote ulioandika...ni kwa sababu umeona Urais ni kama ajira ya mtu mmoja, na sio taasisi. Hao uliowasema hata wakiwa na maonao kiasi gani....tambua ndio walewale waliokuwa wameuzunguka utawala uliopo....hawana jipya nao ni vibaka na wataendelea kuzungukwa na vibaka

Ndugu nimetoa angalizo hapo juu kuwa tukiacha siasa za wivu,chuki, ushabiki usio na maono na fedha lazima tutapata kiongozi safi na bora atakayelifikisha hili taifa pale tunapotaka kuwa.
Hivi ndugu unajua maana ya kiongozi ni nini? Kama hujui naomba tu kwa faida vyako tafuta hata mtu aliyesoma biblia akuhadithie vitabu viwili vya samuel na wafalme. Au kama na wewe ni msomaji jaribu kuvisoma hivo vitabu utajua maana ya kuwa kiongozi mkuu wa taifa na aina ya kiongozi na maono yake yana impact gani kwa taifa kwa ujumla.
Kwa kukusaidia tu maono ya kiongozi kiujumla yanafanya huyo mtu aliongoze taifa katika njia anazoamini zitafikia maono yake. kama hana maono mazuri ataongoza taifa kwa njia mbaya ila kama anayo maono mazuri lazima atateua wasaidizi ambao atawasimamia ipasavyo ili tu maono yake yaweze kutimia na ataenenda na kuongoza katika njia zile zile zitakazomfikisha kwenye hayo maono. Ndo mana leo dunia inamsifia kagame kwa sababu ni kiongozi mwenye maono fulani na anaiongoza Rwanda kwenda kwenye njia ambazo anaamini zitafikia maono yake.
Unadai tena ndo walewale waliokuwa wameuzunguka utawala uliopo, ndugu yangu labda hujasoma hapo juu unajua mchango alioutoa Prof Muhongo kwa taifa hili kwenye sekta ya madini na nishati kwa kipindi cha miaka miwili tu aliyokaa kwenye system kabla ya kuondoka????? au ndo chuki tu??? Jisemee wewe mwenyewe bila chuki na upenzi angekaa kwa japo miaka 10 tu tungekuwa wapi?????
Tafakari ndugu.
 
Mb zikiwasha tutaona mengi mwaka huu
 
Lord denning

Nakupongeza kwa kubaini kuwa prof Muhongo ni kifaa ambacho kitaipeleka tz mbele. Kama tunataka maendeleo, Muhongo ndiyo mtu atakayetufaa, lakini kama tunataka siasa na visasi chagueni ed au bm. God bless our country to enable us to get a right person for our development.
Asante ndugu,
Huitaji kuwa mchambuzi wa siasa wa kimataifa kugundua kuwa nchi yetu imekuwa ikiyumba kwa upande wa serikali hasa kuanzia mwaka 2008 kutokana na ugomvi wa hizi timu mbili za EL na BM. kuna miradi imekwama,kuna mipango imeshindwa kutekelezwa kuna watu wameamishwa vituo vya kazi na hata wengine kuondolewa kwenye u dc, rc na hata nafasi mbalimbali kutokana tu na siasa za visasi za kukomoana baina ya hizi timu mbili. Sasa pata picha timu moja ikishika nchi kutakuwa na hali gani kwenye taifa???? na ukizingatia zote ni timu kubwa zenye ushawishi kwenye system na hata kifenda pia.
Kwa prof Muhongo kila mwenye macho ameona ndugu na hata mwenye masikio amesikia.
 
Mi sioni ulazima wa hadi uwe rais ndiyo uibadiri Tz yako kama kweli unania hiyo,Urais si kitu ambacho mtu yeyote anaweza akawa , kwa sababu tu ana sera nzuri au anapigia kelele ufisadi.
 
Ndugu nimetoa angalizo hapo juu kuwa tukiacha siasa za wivu,chuki, ushabiki usio na maono na fedha lazima tutapata kiongozi safi na bora atakayelifikisha hili taifa pale tunapotaka kuwa.
Hivi ndugu unajua maana ya kiongozi ni nini? Kama hujui naomba tu kwa faida vyako tafuta hata mtu aliyesoma biblia akuhadithie vitabu viwili vya samuel na wafalme. Au kama na wewe ni msomaji jaribu kuvisoma hivo vitabu utajua maana ya kuwa kiongozi mkuu wa taifa na aina ya kiongozi na maono yake yana impact gani kwa taifa kwa ujumla.
Kwa kukusaidia tu maono ya kiongozi kiujumla yanafanya huyo mtu aliongoze taifa katika njia anazoamini zitafikia maono yake. kama hana maono mazuri ataongoza taifa kwa njia mbaya ila kama anayo maono mazuri lazima atateua wasaidizi ambao atawasimamia ipasavyo ili tu maono yake yaweze kutimia na ataenenda na kuongoza katika njia zile zile zitakazomfikisha kwenye hayo maono. Ndo mana leo dunia inamsifia kagame kwa sababu ni kiongozi mwenye maono fulani na anaiongoza Rwanda kwenda kwenye njia ambazo anaamini zitafikia maono yake.
Unadai tena ndo walewale waliokuwa wameuzunguka utawala uliopo, ndugu yangu labda hujasoma hapo juu unajua mchango alioutoa Prof Muhongo kwa taifa hili kwenye sekta ya madini na nishati kwa kipindi cha miaka miwili tu aliyokaa kwenye system kabla ya kuondoka????? au ndo chuki tu??? Jisemee wewe mwenyewe bila chuki na upenzi angekaa kwa japo miaka 10 tu tungekuwa wapi?????
Tafakari ndugu.

Kwanza nakusikitikia....kama nilivyokueleza hapo mwanzo,Urais ni Taasisi, na sio mtu mmoja mmoja.

Naona unapenda sana kupata raisi kwa presentations....hilo sio sifa ya kujua ubora wa kiongozo.....tambua ukitaka rais wa namna hiyo....yupo mchagiaji humu alikupa mfano wa kuwa marais wa hivyo unaweza kuwapata 300 UDSM.
Unapokuja kwenye suala la Muhongo...unachozungumza wewe ni simulizi ulizozipata....kipi alichokifanya Muhongo
kinachokugusa moja kwamoja?? Hizi ni siasa.

Muhongo keshaonyesha udhaifu, kwenye sakata la escrow, na ndio maana kajiuzuru.

Makamba na familia yake hawawezi kusema loloye kwa kina Lowasa na Rostam na timu yao ya wapigaji....maana wamefadhiliwa familia nzima.

Tafuita kiongozi mwenye kuweza kutatua matatizo yaliyopo kwa sasa....kati ya hao uliowataja HAMNA.

Tunahitaji kiongozi atakaeweza kutatua tatizo kubwa tulilonalo watanzania nalo ni UFISADI...kati ya uliowataja HAMNA

Maana walikumbatiwa na mfumo uliopo, nao wataukumbatia hata wakitoka.

fikiri, acha ushabiki
 
Kwanza nakusikitikia....kama nilivyokueleza hapo mwanzo,Urais ni Taasisi, na sio mtu mmoja mmoja.

Naona unapenda sana kupata raisi kwa presentations....hilo sio sifa ya kujua ubora wa kiongozo.....tambua ukitaka rais wa namna hiyo....yupo mchagiaji humu alikupa mfano wa kuwa marais wa hivyo unaweza kuwapata 300 UDSM.
Unapokuja kwenye suala la Muhongo...unachozungumza wewe ni simulizi ulizozipata....kipi alichokifanya Muhongo
kinachokugusa moja kwamoja?? Hizi ni siasa.

Muhongo keshaonyesha udhaifu, kwenye sakata la escrow, na ndio maana kajiuzuru.

Makamba na familia yake hawawezi kusema loloye kwa kina Lowasa na Rostam na timu yao ya wapigaji....maana wamefadhiliwa familia nzima.

Tafuita kiongozi mwenye kuweza kutatua matatizo yaliyopo kwa sasa....kati ya hao uliowataja HAMNA.

Tunahitaji kiongozi atakaeweza kutatua tatizo kubwa tulilonalo watanzania nalo ni UFISADI...kati ya uliowataja HAMNA

Maana walikumbatiwa na mfumo uliopo, nao wataukumbatia hata wakitoka.

fikiri, acha ushabiki

Nimegundua tatizo lililopo hapa ni kuwa umeshindwa kunielewa ninachomaanisha ninaposema aina ya kiongozi wa juu ina determine ubora na uchapakazi wa timu inayomzunguka kama unavosema taasisi.
Ngoja nikupe mfano Kagame anapoteuaga mawaziri huwa wanaaandikiana mikataba kuwa wewe waziri utafanya haya na haya ndani ya mda fulani na huo mda unsapofika waziri anakaa nae na wanaangalia kila kitu kudetermine kama waziri amefanikisha yale aliyoahidi ndani ya mda husika. Hiyo inamaanisha nini?? Labda nikusaidie, inamaanisha kagame ana vision yake, na anapomteua waziri wanakubaliana kabisa kuwa ili tufike hapa ndani ya mda fulani fanya haya na haya na ni lazima u deliver usipodeliver basi anakuondoa. So hapa kiongozi kama kagame ameleta impact kwenye system yake nzima.
Soma vizuri mada kuu kwa nini nimewasifia January na Muhongo??? Sio kwa presentations zao tu ila ni kwa kuweza kuonyesha ni wapi kama nchi tumekuwa na tatizo na kwa kuonyesha vizuri kabisa wana mikakati gani na watafanyae ili kufika hapo.
Sikuishia hapo tu nimeenda mbali zaidi kwa kuonyesha wapi naona prof amemzidi January na nimesema January afanye nini ili kuweza kuuthibitishia umma wa watanzania.
Labda nikusaidie ndugu yangu tuseme hujui Muhongo kafanya nini????? Au ndo lile tatizo alilosema la uvivu kwenye jamii yetu linakusumbua??? sasa basi nenda kaulize takwimu za usambazaji umeme vijijini na maeneo mengine zilikuwaje tangu tupate uhuru na kabla muhongo hajaingia wizara ya nishati na madini,alafu uliza zimepanda kiasi gani kwa kipindi cha miaka miwili tu aliyokaaa pale???
Kingine ndugu unajua kuwa ameweka mikakati na kuitekeleza ya kuwapeleka vijana wa taifa lako nje ya nchi kusomea mambo ya gesi na mafuta na kwa sasa inasemekana wapo zaidi ya 100 ili kulifanya tu taifa lako lije kuwa na wataalamu wa hii sekta kwa ajili ya kuusimamia huu uchumi wa hii sekta huko mbeleni??? sasa hayo kayafanya ndani ya miaka miwili tu aliyokaa kwenye system unataka afanyaje tena?????
Umeongelea kuhusu tatizo la ufisadi nakuomba tu ndugu yangu uliza tanesco alifanyaje au kama ukishindwa kamuulize wakili fulani anaitwa mguu aliyegeuza tanesco kitega uchumi chake. Au ukishindwa hapo kamuulize jamaa fulani ivi alitaka vitalu vya bure akafanya udalali.
Unasema kuwa alionyesha udhaifu kwenye sakata la escrow labda useme ni upi huo kwa ushahidi upi na ripoti ipi ambao hata leo tunaweza kumshtaki kwa uzembe na kuliingizia hasara taifa????
Ndugu yangu nikuambie kitu dunia ya sasa sio ya bla bla ni ya facts, watu wanaenda na facts siku izi ndo mana hata juzi umeona fbi waliamua kuingia field kuanza kuthibitisha kuwa fifa kuna rushwa kwa sbabu wenzetu wazungu wanatuzidi hapo,wao wanaenda na facts na sio bla bla, sasa wewe unasema rostamu anafadhili familia ya January bila kuweka ushahidi. unatakiwa uweke ushahidi hapa na sio wa kutunga ili watu wakuelewe na sio kuongea tu.
 
Tatizo la hao uliowataja watakapoingia tuu ikulu wanageuka na kuwa tofauti kabisa na maekezo yao ya awali.

Hizi sera za kiccm kwa kweli zimechosha na hazina mvuto hata awe nani ni yaleyale
 
January na muhungo ni kati ya walioenda nnje ya utaratibu na dawa yao ni kukatwa tu
 
Kuhusu January anapaswa kuludi kitaa ili akajiufunze Taifa likoje kama anataka serious JOB hii Urais ni michezo ya kuwafanya watu wazima na akili zao kama wajinga [Yani anachokifanya January Anaabuse Akili za Watu wenye Ufahamu kwa sana..tena haipendezi binafsi najisikia sio poa, futa kwenye siasa aina ya vizazi vya hivi]...Muhongo nae Shule ya Management kidogo inaitajika kwenye maswala ya admin. Ana kitu kinaitwa Academic bull head yani usomi wa dalasani unamfanya kuona watu wengine wote ni zero kwenye ufahamu hivyo yeye kuwa nambari moko.Ukileta na mapungufu ya watu wanaosomo taaluma ya jiolojia ya kuzarau taaluma zingine na wao kujiona ndio taaluma bora na ngumu Duniani...huyu jamaa anaitajika kupewa shule kama miaka miwili kuandaliwa kuingalia Tanzania na Watanzania ...akipewa shule na kujifunzaa kuona uzalendo ni Watanzania na si Wazungu wanaomshangilia kwenye mikutano na kumuona ni BRIGHT nooo!!Ukiona Wazungu pia wanakusifikia Jiulize kuna nini?

Sasa kupitia wenye ufahamu mtu Kama Muhongo anaitajika kupewa shule na kuandaliwa ili aje kushika wizara ya nishati na madini aweze kujiandaa na plans za kusimamia miradi ya kuwawezesha Watanzania kwa ujumla wao Wamilki sekta za madini na Nishati kama gas.Muhongo bado anaamini uchumi mkubwa utajengwa na wageni wenye mitaji mikubwa....bado ajajijenga kiakili kuwa kwa akili yake na ubunifu wake ni VIPI watanzania wataweza kukopa na Serikali kuanzisha MIKAPANGO MIKUBWA ya KUSIMAMIA makampuni makubwa ya Kizalendo kwenye sekta ya Madini na Nishati.

Pia Muhongo huyu aandaliwe kuja kusimamia State Mining Company kwenye Madini ya VITO ambayo ni Tanzanite, Diamonds, na Ruby....Tulipofika sekta ya maliasili hiyo inaitajika kusimamiwa na serikali makini na kuifanya hiwe ya manufaa kwa Taifa..kama ambavyo Mwalimu Nyerere alikusudia kuimilki Mwadui Mine Kwa Asilimia 100% na akaishia asilimia 50% ambayo tuliludi na kufikia chini ya hapo yani 25%.Sasa Muhongo si kiongozi ambaye ni presidential Material..Muhongo ni executive material alipwe vizuri na previlege nzuri na kupewa heshima ya kuthaminiwa mchango wake ...a man will do his thing!!!Hii habari ya Urais Muhongo Hapana Goo......Mwachie wa Mwitongo wewe bhana kamata executive post piga mzigo bhana.
 
Back
Top Bottom