CCM amueni kati ya hawa wawili

CCM amueni kati ya hawa wawili

Mkuu umetoa analysis nzuri sana.Binafsi namsupport EL kwa kuwa hapendi longolongo.Aidha,Wamasai na Wameru(mtazamo wangu) wako straight.May be Prof Muhongo apewe U-PM au arudishwe tena kwny eneo lake.
Kuhusu January,wkt safari inaanza tyr ameonekana kutumia mamlaka yake vibaya hasa kupitia Wizara anayoisimamia akiwa Naibu Waziri,hali ya jana kwny baadhi ya mitandao na media imedhihirisha hilo.
 
Kuna ukweli mchungu katika hii mada. Watu wa team za wagombea wengine mnapaswa kukubali.
 
kwa hali halisi, ukinyambulisha point zao na hasa utekelezaji wao na usafi wao, mapendekezo yangu
1. Mwigulu
2. Mhongo
3. Magufuli
4. January

Membe na Pinda poleni kwani mvuto wenu kisiasa, na upole wenu kiutendaji Mpumzike.

Akina Wasira, Bilal, Sitta, Mwandosya, Sumaye tuwape tu asante ya kutumika taifa wakapumzike na Muda umeenda 70+- na wakipewa watafanya kwa mazoea.

Lowasa na Ngereja!!! Hawa sio. sababu zi wazi

Wengine ndo Naniiii?
 
Hawa usiwapime kwa ahadi zao wapime kwa nafasi zao za uwaziri wamefanya nini? Kama kwenye uwaziri hamna kitu ujue na Urais itakuwa hamna kitu
 
kuongea tu kushakuwa rais nzuri! rais ni zaidi ya mipango ya kwenye makaratasi!
 
Ameshindwa kuzuia kivipi????
Labda nikueleze tu,waziri na msimamizi wa sera kwenye wizara. Kwenye escrow lile suala lilikuwa nje ya mikono ya waziri ndo mana hujaona hata sehemu moja ikiwemo kwenye ripoti ya CAG wala kwenye list ya watu walioingiziwa fedha na hata kwenye list ya wati walioonekana kukiuka maadili na kuitwa tume ya maadili jina la PROF MUHONGO.
kwenye escrow baada ya hukumu kutoka correspondence zilikuwa baina ya Katibu Mkuu wa wizara KAMA MTENDAJI MKUU wa WIZARA, Mwanasheria Mkuu na BOT.
Sasa katibu mkuu alimuandikia Mwanasheria Mkuu kumuuliza hela zilipwe au vipi mwanasheria Mkuu kama mshauri no 1 wa serikali kwenye mambo ya sheria akasema zilipwe na kama ulifuatilia ilionekana katibu mkuu aliuliza mara nyingi as je hela zilipwe au vipi na mwanasheria mkuu akainsist hela zilipwe, sasa hata kama wewe ungekuwa Prof Muhongo ungefanya nini? Una mamlaka hayo?
Katibu mkuu wa wizara atafanya jambo bila Waziri kujua? Waliochukua pesa STANBIC unawajua? Nitajie hata mmoja ndipo ntakubaliana na wewe kuwa Muhongo hakuhusika.Acheni ushabiki wa kutofikiri,tunahitaji maisha nafuu kwa wote na siyo ninyi wapiga debe.
 
Hee unabadiri upepo! lakini nimependa uandishiwako
 
Katibu mkuu wa wizara atafanya jambo bila Waziri kujua? Waliochukua pesa STANBIC unawajua? Nitajie hata mmoja ndipo ntakubaliana na wewe kuwa Muhongo hakuhusika.Acheni ushabiki wa kutofikiri,tunahitaji maisha nafuu kwa wote na siyo ninyi wapiga debe.
Ndugu yangu nilishatoa tahadhari kuwa hii thread haijajikita kwenye ushabiki. Tuache hayo haya tuseme Katibu Mkuu alikupa taarifa au hata brief wewe kama waziri wa nishati na madini ungefanyaje kama mshauri mkuu wa masuala ya kisheria wa serikali yaani mwanasheria mkuu amesema pesa zilipwe na BOT????? unajua mfumo wa utendaji kazi kiserikali ukoje?????
Alafu tuweni straight na clear kila siku mnasema STANBIC tu ili kuwafanya watu wawaamin,i kwa nini msiseme account fulani ya Muhongo iliyokuwa stanbic bank iliingiziwa kiasi fulani????
Hivi hiyo ripoti ya CAG ni wapuuzi kuacha kumtaja Muhongo?? Tume ya maadili ni wehu kuacha kumtaja au kumuita Muhongo???? Tuweni realistic watanzania kwenye nyeupe tuseme nyeupe sio hivi. Mungu atusaidie kwa kweli.
 
Huyu kweli ni wa kupewa hongera tu kwa kuandika, hivi ana underestimate nguvu ya ukawa eeh, yaani kusimamisha Muhongo au Makamba ni bora hata uchaguzi tusifanyike tu kuokoa hizo fedha, tunamwachia tu Dr.Slaa aende zake Magogoni

Hao Jamaa Alowataja Ni Wazuri Kwa Malengo Walotutajia, Tatizo Lao Ni Kule Walipo Hakuendeshwi Na Maono Ya Mtu Zaidi Ya Sera Za Chama.
 
Kiualisia kuna kitu umekitambua na uko,sahihi....obama alichukua nchi kwa sera ya bima ya afya kwa wote na moja ya tatizo kubwa la wamarekani lilikuwa ni gharama za huduma za afya...lakini siasa za kiafrika zimejaa mbwembwe na nguvu ya pesa pamoja na makundi...nyere alijitahidi kuvunja makundi mwaka 1995 kwa kuhakikisha mkapa anakuwa mgombea uraisi na kuacha makundi hasimu yakiduwaa...ukisikiliza hotuba ya muhongo na jm zimejaa mpango mkakati pamoja january amejitahidi sana kukopi mawazo ya upinzani ili kumpa nguvu na kama akiteuliwa kampeni zinaweza kufanana especially kwenyemserikali ndogo (wazo).

Pamoja ya kwamba upinzani upo imara kuliko wakati wowote ule bado ccm ina nguvu yako ambayo haiwezi kumalizwa kwa,porojo za mitandaoni..upinzani kufanya vzr kwenyemserikali za mitaa hakujazuia ccm kushinda kwa asilimia kubwa...prof muhongo kaondoka vbya na wengi wamemfahamu baada tu ya kuteuliwa kuwa waziri ambako alijitahidi kufanya kazi yake..January kizazi cha sasa ambaye bado ana nafasi sikumza usoni pamoja kwa sasa nchi kuongozwa na lowassa au membe ni msala,kwa ccm maana yake balaa kwa watanzania.

Ni wakati wa ccm kufanya maamuzi kama ya mwakam95 na sio upuuzi wa 2005 ambao umewaletea shida mpaka leo...kwa watanzaniamuhamuzi mgumu ni kuwaamini ukawa na Wspecially Dr slaa ambaye na yeye simuoni kuongoza kwa ukakamavu kwa miaka kumi au ndio yatakuwa ya lowassa pia mbatia ambaye amejitahidi kusimamia hoja na kutetea hoja zake kwa mapana...nategemea uchaguzi mpana na wenye tija kwa watanzania na kwa yeyote atakayeshinda ana mzigo mkubwa.
 
Tunatakiwa kuwa makini zaidi, tunapotoa maoni yetu kuhusu Raisi ajaye kwa weledi, umakini, uwezo wake wa kifikra na maono yake ya baadae. Bila jaziba na siasa chafu za kuchafuana bila ushahidi wala fact zozote! Prof. Muhongo anafaa zaidi kwa uwezo wake alioonyesha kwa muda wa miaka miwili na nusu tu, maono yake yatatufikisha Tanzania tunayoitaka.

Yani kwa kutajwa kwake tu kwenye ufisadi wa escrow alitakiwa hata nia asitangaze.
Kuwa na weledi na elimu tu hakutoshi.
Uadilifu ni sifa kubwa sana ya Kuwa kiongozi.
 
Am with prof muhongo vision yake iko crystal clear... Na anaweza kuielezea katika lugha nyepesi ambayo hata asie na elimu ya kiviile atamuelewa.

Vision yake kutuunganishia mabomba ya gesi kila nyumba??? Hayo maji tu ambayo gharama ya kuunganisha ni ndogo imeshindikana. Acheni ushabiki usio na macho
 
Kwaninin watanzania tunasahau sana mapema. Hao wote wemepewa nafasi serikalini lakini hukuna walichofanya zaidi ya kutuibia fedha, Mhongo juzijuzi amekataa katakata escro sio za uma, halafu jamaa sio mtu wa mlengo wa kutuwezesha wazawa tumiliki uchumi.
Makamba ndio kabisa kama abisha kamulize Mkewa.

Suruhisho sio kumtafuta mtu ccm bali ni kuipaga chini ili wazaliwa upya kinyume na hapo tutabaki ni hadithi tu.

"Ee Mungu ulie hai mwenye Enzi yote, tufungue akili watanzania tumjue adui yetu CCM na utupe nguvu zakumwadhibu October na jinsi uwezavyo wewe kumwadhibu huyu CCM, Amen".
 
Kwaninin watanzania tunasahau sana mapema. Hao wote wemepewa nafasi serikalini lakini hukuna walichofanya zaidi ya kutuibia fedha, Mhongo juzijuzi amekataa katakata escro sio za uma, halafu jamaa sio mtu wa mlengo wa kutuwezesha wazawa tumiliki uchumi.
Makamba ndio kabisa kama abisha kamulize Mkewa.

Suruhisho sio kumtafuta mtu ccm bali ni kuipaga chini ili wazaliwa upya kinyume na hapo tutabaki ni hadithi tu.

"Ee Mungu ulie hai mwenye Enzi yote, tufungue akili watanzania tumjue adui yetu CCM na utupe nguvu zakumwadhibu October na jinsi uwezavyo wewe kumwadhibu huyu CCM, Amen".

Nimesema tukiacha siasa cha chuki,wivu,ushabiki usio na maono na rushwa lazima tutamchagua kiongozi mzuri ngudu yangu. Niambie Muhongo kaiba wapi na shilingi ngapi?
Nazidi kumuomba Mungu huyu huyu akufumbue macho ili uweze kuona Muhongo ni nani na ana maono gani na hii nchi.
Ni wazawa gani ambao unasema wawezeshwe kumiliki uchumi???? Sikiliza speech ya Prof vizuri mkuu,alishasema hana ugomvi na wazawa kumiliki uchumi wa nchi ila ana ugomvi na wababaishaji na wakwepa kodi??? Nani asiyewajua hawa???????

Kama Muhongo hataki wazawa kumiliki uchumi wa nchi yao angesimamia kutafuta scholarships kwa ajili ya watanzania wa kawaida kwenda kusomea uchumi wa gesi nje ya nchi ili waje kusimamia uchumi wa gesi vizuri????
Kuna swali ukijiuliza tu ndugu yangu hapohapo Mungu anakufungua akili na unapata uelewa.
 
Vision yake kutuunganishia mabomba ya gesi kila nyumba??? Hayo maji tu ambayo gharama ya kuunganisha ni ndogo imeshindikana. Acheni ushabiki usio na macho
Sikiliza speech yake yote na vizuri kabisa ndugu yangu ukiwa na neutral mind utamuelewa vizuri sana.
 
Yani kwa kutajwa kwake tu kwenye ufisadi wa escrow alitakiwa hata nia asitangaze.
Kuwa na weledi na elimu tu hakutoshi.
Uadilifu ni sifa kubwa sana ya Kuwa kiongozi.
Kutajwa kufanya nini???? Je alikuwa ni muhusika au mmojawapo???? kwa ushahidi gani wa kitaarifa ambao hata kesho ukiwapa watu kama FBI wanaochunguza rushwa ya FIFA watakushauri kuwa ana kesi ya kujibu na uende kumshtaki????
 
makamba msanii tu kaandika speech nzuri lkn hana lolote.... kashindwa hata kudhibiti MB za mitandao leo uraisi ataweza?
 
Ndugu yangu nilishatoa tahadhari kuwa hii thread haijajikita kwenye ushabiki. Tuache hayo haya tuseme Katibu Mkuu alikupa taarifa au hata brief wewe kama waziri wa nishati na madini ungefanyaje kama mshauri mkuu wa masuala ya kisheria wa serikali yaani mwanasheria mkuu amesema pesa zilipwe na BOT????? unajua mfumo wa utendaji kazi kiserikali ukoje?????
Alafu tuweni straight na clear kila siku mnasema STANBIC tu ili kuwafanya watu wawaamin,i kwa nini msiseme account fulani ya Muhongo iliyokuwa stanbic bank iliingiziwa kiasi fulani????
Hivi hiyo ripoti ya CAG ni wapuuzi kuacha kumtaja Muhongo?? Tume ya maadili ni wehu kuacha kumtaja au kumuita Muhongo???? Tuweni realistic watanzania kwenye nyeupe tuseme nyeupe sio hivi. Mungu atusaidie kwa kweli.
Umepewa ngapi kumsafisha? Kama hujui kitu kaa kimya, acha kutetea waliooza.
 
Back
Top Bottom