CCJ Kulikoni!?

CCJ Kulikoni!?

Nasikia leo Mkoa wa Pwani! Duh wasipokuwa makini kwa kweli watapata tabu sana kusajiliwa
 
Nilipoiona CCJ mwanzo, niliudharau na kuiona its a hoax, comming to put just another junk on the game ambalo tayari limeshajaa junks!. Alipoingia Mpendazoe, nikajua amekurupuka na kuhama CCM kwa jazba, nilipomsoma Mzee Mwanakijiji, ndipo nikapata shauku ya kweli kuanza kuiamini CCJ might be something realy, something serious and for realy war, japo mpaka sasa sijabahatika kujua ukweli wa who is who is a really CCJ, wanaambiana, wanaitana, na wanajiunga, huku wengine tukishawishiwa kwa ushawishi kuwa CCJ sasa ndio chama mbadala.

Tusiilaumu bure CCJ, kuna uwezekano Tendwa amewashtukiza (surprise check) hivyo walikuwa hawajajiandaa kama walivyo puliza baragumu, ila kama wakipata muda wa kujiandaa vizuri, they'll put their house in order kabla mgeni hajafika.

Lakini pia tusirule out uwezekano wa hii CCJ inayokaguliwa ndio CCJ halisi, achilia mbali CCJ ya kwenye ma Press Conference na wasemaji wake kibao. Kama hii inayoibuka ndio CCJ kweli na halisi, then I was not wrong. CCJ is a hoax!.

Pasco CCJ hawajastukizwa walikuwa wanafahamu na walikutana na Tendwa ana kwa ana lakini pia chama makini chochote lazima kiwe kimejipanga wakati wote kwani si ni wao walioomba usajili wakijua kuwa lazima wahakikiwe?na si ni wao waliomshurutisha Tendwa na kusema kuwa kama hana pesa wao wako tayari kumkompesha kwa riba ili zoezi lifanyike?sasa kama hawakujipanga nani alaumiwe hapa?na kujipnga huko ni kupi hasa?
 
Kuna tatizo ndani ya CCJ. Wasitafute mchawi. Kuna shida!!
 
Mkuu Ndibalema,
ushahidi unao utaka hapa hutaukuta, wala usitegemee kuuona openly kama unvyotaka kuuona.

Kitu ninachoweza kukupa, labda ni kukumbusha kuwa sisiemu ndiyo iloshika serikali hivyo imemeza taasisi nyingi sana, ikiwa jeshi lapolisi, mahakama n.k vimeshikwa na serikali ya sisiemu; vipi kwa Tendwa?

Kwa macho ya nyama na masikio huwezi kuuona uchafu wa hiki chama, ni mpaka uruhusu fikra zako kuchungulia ndani zaidi, Bunge tu halina ubavu kwa sisiemu, tume za uchaguzi tu hazina ubavu kwa sisiemu awe Tendwa?

Usishangae akawa ana represent kile kilichoaandaliwa na sisiemu kwa manufaa yake, ila ushahidi unaotakuona hapa, mimi nina hakika huwezi kuupata kwa mtazamo wako.


Nakubaliana na wewe Kwamba SISIEMU ni mafia, lakini hili la majina jamani umafia wa sisiemu umetoka wapi? ina maana CCJ ilifanya uandikishaji wa wanachama wake hewa? (Vipandikizi) ? kama ni kweli CCJ hawana Intelligent unit ya kungudua vitu vidogo vidogo kama hivi? kwa nini basi tusipate wasiwasi na utendaji mzima wa CCJ?

Tusifike mbali kote huko, just a simple statement "UHAKIKI WA MAJINA" guys.... mi bado haliningiii akilini SISIEMU na Tendwa wamecheza umafia gani hapa? I'm not convinced...
 
WanaJF hapa msipate tabu CCM ni MAFIA wamewapa hela member wa CCJ ili wasitikee kwenye uhakiki, sasa mtu akipewa kama 200,000 unafikiri atakuja???
 
WanaJF hapa msipate tabu CCM ni MAFIA wamewapa hela member wa CCJ ili wasitikee kwenye uhakiki, sasa mtu akipewa kama 200,000 unafikiri atakuja???

Ni Kweli kaka nasikia hata Mwenyekiti wao naye alipewa 20,000,000 asijipe kadi na Katibu Mkuu akapewa donge nono na ahadi kemkem asijiorodheshe kwenye fomu za Wanachama
 
Bila shaka uko mkono wa CCM. Pengine tatizo ni kwamba CCJ ilivyokuwa launched ilitangazwa sana na kuonekana tishio (iwapo hili ni sahihi au la) kwa CCM. Nandiyo maana Msajili aliagizwa kukihakiki kwa kutumia darubini kali.

Mimi sidhani iwapo chama hicho kingeomba usajili kikawaioda tu kama vile vyama vingine uchwara -- ingepata bila kusita. Tusisahau mwaka 1994 wakati CUF ilipogomea kushiriki uchaguzi mdogo katika jimbo la Kwahani kulikuwa hakuna chama kingine kilichokubali kushiriki dhidi ya CCM, ambayo ilihofu mbele ya jamii la kimataifa kwamba nadharia nzima ya serikali yake kuanzisha kwa demokrasia ya vyama vingi ilikuwa mashakani katika zoezi la kwanza tu la demokrasia hiyo.

Kuna point lakini suala la kufanya underground upande wangu naliona kama lisingewasaidia sana hasa kipindi hiki chenye vyama vya bendera na usajili tu. Nadhani walikuwa sahihi kuingia kwa nguvu ili kuvuta hisia na support za jamii.

Suala la vitambulisho ni tatizo katika nchi yetu. Ukiuliza watanzania wangapi wana vitambulisho ukiacha cha mpiga kura inasikitisha. Mathalani mimi wakati nakwenda kujiandikisha kwenye daftari la kudumu niliulizwa mtaa tu na personal particulars hakuna aliyeniuliza kitambulisho chochote katika suala muhimu na nyeti kama lile hata swali ndogo tu la kiongozi wa mtaa sikuulizwa. Je kitambulisho hakikuwa muhimu zaidi katika suala hili? hivyo vitambulisho vya uraia viko wapi maana ndivyo vingekuwa solution katika hili.

Sijui wanatumia vigezo gani kama mtu amekuja na kadi ya uanachama that is him and for the sake of verification hiyo ndiyo. Hauwezi kwenda bank una kadi yako unataka kuchukua fedha kwenye account yako wakuulize kitambulisho wakati kadi yako ndiyo kitambulisho chako mahali pale.

Issues hizi zinahitaji ufafanuzi zaidi sipati picha kama CCJ baada ya kujiuza kwa watu wangewaomba walete vitambulisho ili kupewa uanachama wangepata response gani. Hapa freedom of association inakuwaje iwapo sina kitambulisho?
 
Inasikitisha kuona hawa CCJ wameshindwa kuorodhesha na kuhakiki wanachama wao 200 kwa Dar tu, ilhali ni wao ndio wamemladhimisha Tendwa aje kuwahakiki wako tayari na wanachama 2,000 Dar, acoording to their chairman. Sasa hapa mwenyekiti wao analalamika Tendwa hawezi kazi ilhali wanachama wao feki na real hawafiki hata 150 hapo mkutanoni. Na hata yeye na katibu wake hawana kadi!
Huu ni uzembe wa hali ya juu, period.
Kuna mtu awali alilinganisha na chama cha chemponda in 1994, sasa kweli wakati ule ccm ilikuwa inajaribu kulazimisha vyama vingi na kufungia macho those things, we are in 2010 tunataka responsible upinzani ambao wataweza kuorganise na kutetea jamii yenye watu takriban 40 million, sasa kama hata kuorganise watu 200 inakuwa taabu, jee siasa za kitaifa wataweza kweli?
Na sioni namna ccm inahusika na uanachama batili, ccj iombe ushauri cuf jinsi ya kuorodhesha wanachama na kuhakiki, wana uzoefu mkubwa hasa visiwani.

Ofisi ya msajili wa vyama vya siasa, inaogopa mno kuisajili CCJ kwa sababu haiujulikani ni akina nani wataenda huko (wakitokea CCM) baada ya CCJ kuwa imesajiliwa.

Kuna watu very potential wanasubiri chama kisajiliwe tu basi halafu wanaanza kai nzito mno hujawahi kuiona hapa Tanzanaia. Mpendzoe yeye katangulia kuja kukilindia imani yake kwa wananchi (ili wananchi wawe na uhakika kuwa chama si cha mamluki)! mpaka pale kitaposajiliwa


Kwa picha ambayo nimeshaipata mimi mpaka sasa hivi, uwezekano mkubwa ni kwamba CCJ haitasajiliwa mpaka uchaguzi mkuu upite. Watu kughushi kadi za uanachama ni kosa la jinai, lakini eti bado watu kama wale wana-appear wenyewe kwenye zoezi zima la uhakiki wa wanachama wa CCJ!

Kuna urasimu gani wa mtu kusajiliwa na CCJ na kupewa kadi halali ya uanachama, eti mpaka mtu afikie hatua ya kulazimika kughushi kadi ya uanachama? CCJ ni chama kichanga mithili ya mtoto ambaye bado ananyonya ziwa la mama hajaanza hata kutambaa.

Je, CCJ kuna nini cha maslahi zaidi ya haki, hadi watu wabovu waanze kukimbilia huko kwa kughushi kadi za uanachama? Maana mtu anapoingia sehemu kwa forgery, huyo siyo mpiganaji, ni opportunist tu. Kamwe CCJ watu kama hao hawatakuja waingie!

 
CCJ watoe kwanza kibanzi katika jicho lao kabla ya kuonesha boriti iliyokatika jicho la CCM!

Mimi hapa sioni mantiki ya CCJ kulalamikia Mkono wa CCM kwenye zoezi hili, ni wazi hakuna ushahidi na wala maelezo yao hayawezi kukidhi haja ya mtu mwenye kufikiri sawasawa, kuvurugika kwa lile zoezi CCJ have themselves to blame, there is no need of CCJ to start witch hunting in CCm or somewhereelse, the witch they are looking for is inside their part! Ni uzembe wao wenyewe, kama walishajua kuwa kuna mbinu chafu toka mwanzo si wangejiridhisha wenyewe kwanza kuwa kilakitu kiko sawa kabla ya kumuita Tendwa!

Ni upuuzi kwa CCJ kuendelea kuinyooshea kidole CCM kwa makosa yao wenyewe, mimi nahis CCJ wants to seek for public sympath by pointing a finger to CCM! Jamani not all evil doings are devils acts, some of them are from our own feelings and desire! Siipendi CCM, sio shabiki wa CCM, lakini kwa hili hapana!

ipo siku utaipenda kaka,kwa mawazo yako haya wewe si wakuamiwa sana!
 
Nasikia leo Mkoa wa Pwani! Duh wasipokuwa makini kwa kweli watapata tabu sana kusajiliwa

Kama mnakumbuka sisiemu wote walisema tangu Mwanzo kuwa hawa jamaa hata kama watatimiza masharti basi hawata pata usajili mpaka uchaguzi upite. Tendwa akarudia hayo lakini alipoona amechemka,a akasema hamna tabu ngoja tuanze, kwa haraka haraka kama ukifikiriautajua kuwa hawa jamaa piaga ua , hawata pata usajili wa kudumu, mpaka uchaguzi upite...
 
Walikuwa wanahangaika na kujibu matamko ya kwenye vyombo vya habari kwanza. Wekeni CVs za hawa viongozi wa muda wa CCJ. Mimi naona tatizo linaanzia kwa hawa.Wanababaika, wanahamanika, hawajiamini, hawazijui siasa za bongo, wanajifunzia UONGOZI hapa, sasa hivi.

Kweli kabisa WildCard
Inaonekana viongozi wa CCJ wanaupungufu ktk idara ya oganaizesheni, hii inawezekan kutokana na viongozi wa muda mpaka wakati huu hawajaweza ku-'achieve' lolote ktk maisha yao, iwe ufugaji wa ngombe wengi au kuendesha kampeni ya kilimo cha mpunga au biashara kubwa au kufanikiwa kupata elimu ya juu n.k vyote hivyo vinahitaji dedication, discipline na visheni.

Mimi mpaka leo swali alilotaka Wildcard kuwa profile/cv/resume ya viongozi wa muda wa CCJ iletwe hapa JF, tuone kabla ya kutaka kusajili chama cha CCJ viongozi wake wamefanikiwa kujifanyia nini wao binafsi na jamii inayowazunguka mpaka wakaamua wamekomaa kujiingiza ktk siasa?!
 
Nadhani tatizo ni CCJ kwa kiasi kikubwa......
Majina ya kuhakikishwa huletwa na Chama chenyewe. Sasa hata huyo mwenyekiti wa CCJ hakuwa na kadi ili ahakikiwe anasema eti alipoteza wakati amenigwa pale Kariakoo (angeweza kuchukua kadi nyingine kwa mujibu wa taratibu za chama chao kwa kadi zinazopotea madhali alitoa taarifa polisi). Huyo Katibu Mkuu wao pia hakuweza kuhakikiwa. Hata wangehakiki watu wote pale Mwembe Yanga bado wasingefika 200! Huoni kuwa tatizo ni CCJ?

Kitu kimoja katika siasa za Tanzania, unapokuwa mpinzani unapaswa kuwa makini sana sana. CCJ wlaikwenda kuzindua chama MwembeYanga. Mpendazoe alikwenda kuchukulia kadi mwembe yanga. MwembeYanga ni TEMEKE na Temeke eneo la CUF. Kwa vyovyote vile kama CCJ hawakushirikiana na CUF (na ninaamini hivyo maana walijiona wao ndio wakombozi na kazi nyingine iliyofanywa na vyama vya upinzani toka mwaka 1992 ni bure) basi CUF ilipandikiza watu katika uanachama na ndio hayo yamewakuta. Hiyo ni Dar mtaona kwingine.

I have an experience with this. Mwaka 2007 CHADEMA tuliweka Mgombea Ubunge katika Jimbo la Tunduru baada ya Akukweti kufariki. Tunduru ni CUF strong hold lakini CHADEMA 'tuliamini' kuwa tunaweza kufanya mabadiliko. CUF walilalamika sana na hatukuwasikiliza. Wakaweka mtego. Kila kata tuliyokwenda wanachama wa CUF ndio walitupokea, wakachukua kadi za CHADEMA na kuunda uongozi na timu za kampeni. Tukafanya kampeni kabambe kabisa with a modern information system (ambayo pia tulitumia Tarime na chaguzi nyingine zote na hivyo kuwa chama cha kwanza kupata matokeo mapema kama tunashinda tunazuia wizi wa CCM).

Uchaguzi ukafika. Watu wakapiga kura. Tukapata kura 2000 tu. Kumbe watu wote tuliokuwa tunafanya nao kazi ni CUF na hawa 2000 kwa kweli ndio haswa walikuwa wafuasi wa CHADEMA kule Tunduru.

This is how CUF safeguard ngome zao. CCJ inaweza kuwa Hoax kama alivyosema Tendwa.
 
Mie kwenye Jambo au swala CCJ nalikalia mbali maana mh naiogopa siamini kama chama kilicho serious anyway ni mtazamo wangu tu
 
...
Tungepata mtu wa CCJ atuthibitishie kuwa hili la majina feki ni kweli hujuma za CCM na Tendwa mwenyewe kutotaka wasishiriki uchaguzi mkuu ingekaa vizuri zaidi.
...

Ngoja kwanza Mwanakijiji amalizie usingizi, akiamka anaweza kusema kama ni hujuma au hawakujipanga!
 
Mie kwenye Jambo au swala CCJ nalikalia mbali maana mh naiogopa siamini kama chama kilicho serious anyway ni mtazamo wangu tu

Kimeahidi kwa kipindi hiki kifupi kitafanya yale ambayo vyama vya Upinzani vimeshindwa kufanya katika miaka zaidi ya 15 iliyopita, so lets wait and see
 
Ngoja kwanza Mwanakijiji amalizie usingizi, akiamka anaweza kusema kama ni hujuma au hawakujipanga!

Kwani bado hajaamka jamani au alichelewa kulala asipokuwa makini hii CCJ itamuongezea Uzee, just Kidding
 
CCJ imekuja kuwachanganyia wananchi habari hili wwatu waache ku-focus kwenye vyama vya maana kama CHADEMA wa focus Kwao, ndio maana kelele nyingi vitendo hamna.Huyo mwenyekiti wao tu alikuwa hana kadi uanachama siku ya kuhakiki na amedai kwamba kadi yake iliibiwa wakati ule alipovamiwa na majambazi.sasa toka siku hile mwenyekiti ameshindwa kupata kadi nyingine?

Tusisahau wakuu "DEBE TUPU HALIACHI KUVUMA".
 
Nadhani tatizo ni CCJ kwa kiasi kikubwa......
Majina ya kuhakikishwa huletwa na Chama chenyewe. Sasa hata huyo mwenyekiti wa CCJ hakuwa na kadi ili ahakikiwe anasema eti alipoteza wakati amenigwa pale Kariakoo (angeweza kuchukua kadi nyingine kwa mujibu wa taratibu za chama chao kwa kadi zinazopotea madhali alitoa taarifa polisi). Huyo Katibu Mkuu wao pia hakuweza kuhakikiwa. Hata wangehakiki watu wote pale Mwembe Yanga bado wasingefika 200! Huoni kuwa tatizo ni CCJ?

Kitu kimoja katika siasa za Tanzania, unapokuwa mpinzani unapaswa kuwa makini sana sana. CCJ wlaikwenda kuzindua chama MwembeYanga. Mpendazoe alikwenda kuchukulia kadi mwembe yanga. MwembeYanga ni TEMEKE na Temeke eneo la CUF. Kwa vyovyote vile kama CCJ hawakushirikiana na CUF (na ninaamini hivyo maana walijiona wao ndio wakombozi na kazi nyingine iliyofanywa na vyama vya upinzani toka mwaka 1992 ni bure) basi CUF ilipandikiza watu katika uanachama na ndio hayo yamewakuta. Hiyo ni Dar mtaona kwingine.

I have an experience with this. Mwaka 2007 CHADEMA tuliweka Mgombea Ubunge katika Jimbo la Tunduru baada ya Akukweti kufariki. Tunduru ni CUF strong hold lakini CHADEMA 'tuliamini' kuwa tunaweza kufanya mabadiliko. CUF walilalamika sana na hatukuwasikiliza. Wakaweka mtego. Kila kata tuliyokwenda wanachama wa CUF ndio walitupokea, wakachukua kadi za CHADEMA na kuunda uongozi na timu za kampeni. Tukafanya kampeni kabambe kabisa with a modern information system (ambayo pia tulitumia Tarime na chaguzi nyingine zote na hivyo kuwa chama cha kwanza kupata matokeo mapema kama tunashinda tunazuia wizi wa CCM).

Uchaguzi ukafika. Watu wakapiga kura. Tukapata kura 2000 tu. Kumbe watu wote tuliokuwa tunafanya nao kazi ni CUF na hawa 2000 kwa kweli ndio haswa walikuwa wafuasi wa CHADEMA kule Tunduru.

This is how CUF safeguard ngome zao. CCJ inaweza kuwa Hoax kama alivyosema Tendwa.

ZITTO.

I agree with u for about 101%

Kwenye gazeti la DailyNews la leo, ukurasa wa pili, kuna picha ya wanaojiita wanachama wa CCJ wakishangilia jana pale Mwembe Yanga ATI BAADA YA KUONA MAJINA YAO HAYAPO ndani ya daftari la uhakiki!

....FOR SURE POLITICAL IS A DIRTY GAME....
icon9.png
 
tatizo liko kwa Msajili.. na watu hawataki kuona tatizo hilo kwa sababu wanapenda kweli tatizo lingekuwa kwa CCJ.

Nilikesha jana kufuatilia suala hili kutoka pande zote na jaribio la msajili ni "kufanya uhakiki hewa" wakati tayari ameshafikia uamuzi. Hili ndilo lilikuwa lengo la kutoa kauli tofauti kati yake na Marmo (ambaye msajili yuko chini yake) ndani ya masaa 24. Lengo lilikuwa ni kuwachanganya wananchi na hivyo kutokutoa muda kwa CCJ kuwaandaa wananchi na kuelewana mfumo.

a. Msajili alisema hana fedha za kufanya uhakiki.. hakuna mtu anauliza hizi za sasa zimetoka wapi?
b. Walisema uhakiki hautafanyika na kuwa CCJ haitashiriki uchaguzi .. sasa wanafanya uhakiki ili kiwe nini?

Wengi humu mnaposikia "uhakiki" hata hamuulizi umefanywaje hadi kuzua malalamishi. Mnachukulia tu kuwa watu wamelalamika bure.

Nimefafanua sehemu nyingine labda nirudie hapa:

Msajili alitakiwa kufanya uhakiki wa wanachama 200 wa mkoa wa Dar.. kaenda Mwembeyanga na kukuta kuna wanachama wa kutoka matawi mbalimbali ya mkoa wa Dar. Yeye kachukua orodha ya watu wa maeneo ya Mwembeyanga na ni HAO TU ndio alioataka kuwahakiki. Wanachama wa CCJ kutoka sehemu nyingine wamekataliwa kwa sababu majina yao hayakuwepo kwenye "orodha ya mwembeyanga".. Hakutaka kuchukua orodha ya sehemu nyingine za Dar kulinganisha! Sasa anapotangaza kuwa watu hawapo kwenye orodha au majina yao hayaonekani ni kweli - in the wrong orodha.

Hii ndio sababu ya uongozi wa CCJ kutaka zoezi lisitishwe kwani "uhakiki wa mkoa" unapofanyika kama uhakiki wa kitu kimoja kunapoteza kabisa dhana nzima ya uhakiki. Cha kuudhi kama kawaida vyombo vya habari vimerudia tu kile kilichoripotiwa na Msajili baada ya kwenda kuuliza maswali ya muhimu kujua nini hasa kimetokea.
 
tatizo liko kwa Msajili.. na watu hawataki kuona tatizo hilo kwa sababu wanapenda kweli tatizo lingekuwa kwa CCJ.

.....

I wish ungeona jinsi Kyabo anavyochemka. Hana busara na hafai kuwa kiongozi. He can't control his emotions and doesnt think before speaking.

Ilikuwa ni kazi ya CCJ kuhakiki wanachama wao kabla ya kumwita msajili wa vyama kufanya uhakiki. Kwa kutokufanya uhakiki wa ndani, inaonyesha ni jinsi gani chama hiki kisivyo makini.

Kingine, Kyabo hana mamlaka ya kuahirisha zoezi, kama ana mamlaka hayo nirekebishwe.

Halafu kuanza kuingiza na kushutumu hila zinazofanywa na CCM ni kukosa kujiamini, inferiority complex. Pia kuanza kutaja kwa kujiamini na jazba kwamba watashiriki kwenye uchaguzi kuanzia madiwani na hadi urais, na kwamba rais wao ni strong kuishinda CCM, alikwenda nje ya mada na anaonyesha jinsi anavyotapatapa.

Pili kusema kuwa yaliyokuwa yakitendeka wakati wa zoezi ni 'upumbavu/ujinga', ana maana msajili wa vyama ni mjinga? With all due respect, Mr Kyabo have to take back some of his words. Msajili wa vyama vya siasa ni taasisi inayohitaji kuheshimiwa (simaanishi kupigiwa magoti wala kunyenyekewa). Msajli wa vyama lazima afuate sheria na taratibu zilizowekwa, asiwe mtu mwenye kuyumbishwa wala kufanya shughuli zake kwa kufuata hisia za clientelle.

Mr Kyabo una/meiangusha CCJ.
 
Back
Top Bottom