CC ya CCM haikuwa na jipya

CC ya CCM haikuwa na jipya

CCM sasa hivi ni kama yai kila mmoja anaogopa kulishika lisije likamvunjikia. Siamini macho yangu kwamba CC wameishia kupongezana kana kwamba hakuna ovu hata moja lililojitokeza katika siku za hivi karibuni na kwamba mambo yote shwali. Tunapashwa kujiuliza kama CC wamepongezana je ile kashfa ya escrow haiwahusu, je wanachama wao waandamizi wanaotajwa kuchota mabilioni kutoka escrow kwao siyo tatizo. Hiki ndo chama tawala (twawala) tunapashwa kuwaangalia kwa jicho la tatu kwa hiyo staili yao ya kupongezana hata pale kunapoonekana kuna matatizo ya dhahiri.
 
Mmeona,kusikia na kuamini maazimio ya CC?

Mzee Tupatupa

Nimecheka kama mazuri,haki ya nani tunahitaji maombi hasa ili tuondokane na hili dubwasha CCM! Kali kuliko yote ni kujadili swala la soko la mahindi!
 
Utamsemaje mkubwa wako ana kwa ana na ukajihakikishia usalama wako? Kilichobaki pongezi tui kupongezana. Wakitoka madarakani ndo utasikia mabaya yake maana wakati huo atakuwa kibogoyo wala hang'ati. Kama pamoja na kuwa na meno naye analalamika kama kina yakhe, basi ujuwe wakati huo akishatoka atakuwa analia na kulalamika aonewe huruma. Sikutarajia mambo makubwa kwenye kikao hicho. Hukumbuki msema kweli binamu yake Mtikila alichofanywa kwa kuwa muwazi mbele za wakubwa zake? Kila mtu (hasa mdogo) anapenda aishi hata kama kwa shingo upande.
 
wana Jf, habarini za asubuhi!!!..
bila kuwachosha ningependa kujuwa idadi ya wajumbe wa CC ya ccm kwa majina.

Maana tunaambiwa Lowassa ana karibia 75% ya wajumbe wa Nec wanao Muunga mkono. je CC ina wajumbe wangapi na ni kina nani?

mimi nawajuwa wajumbe wawili na wote wana muunga lowassa mkono waziwazi, nao ni Sophia Simba na Sadif mwenyekiti wa Uvccm.
 
Hawamuungi mkono wanataka kumchomoa tu tena forex hawataki za madafu, lakini wakimchomoa nyingi basi wanaweza kumpitisha maana wajumbe wote wahuni hawajali maslahi ya nchi bali wanajali matumbo yao tu. Huu ndio ukoo wa panya ni uharibifu tu mwanzo mwisho.
 
Hawamuungi mkono wanataka kumchomoa tu tena forex hawataki za madafu, lakini wakimchomoa nyingi basi wanaweza kumpitisha maana wajumbe wote wahuni hawajali maslahi ya nchi bali wanajali matumbo yao tu. Huu ndio ukoo wa panya ni uharibifu tu mwanzo mwisho.

After all he is not our headache. ..!!!
 
  • Thanks
Reactions: BAK
ni tabia za magamba kutokuwa na msimamo!!! ni kawaida kupata uongozi kwa rushwa ndani ya CC
 
Jipya utalipata mwezi wa tano.

Yaani maamuzi yashindwe kutoka leo yasubiri mwezi wa tano? Au ndo mtaanza utekelezaji wakati huo ndio siku Tisini za kuvua gamba zitakuwa zimefika? Chama cha kikomedi hiki!!!
Vipi Mtemi Chenge anavyowaburuza huko chama kizima? Mmemzungumzia?
 
Back
Top Bottom