cc MwanaDiwani njoo umsikilize vuta nikuvute
Atupe na picha za AbdulKatembo Kindovu akiwa anapongezwa
Last edited by a moderator:
cc MwanaDiwani njoo umsikilize vuta nikuvute
Asante mzee Throw-throw wa Lumumba, tulijua huko mambo mdebwedo tu.Kamati Kuu ya CCM iliyoketi leo Kisiwandui,Zanzibar ilitawaliwa na pongezi pamoja na maagizo ya hapa na pale ya kichama. Taarifa za kuaminika toka ndani ya kikao husika zinaonesha kuwa CC imepitisha karibu maazimio yote ya Kamati ya Komredi Mangula.
CC imepongeza ushindi kwenye Serikali za Mitaa. Pia CC imeipongeza Kamati Maalum ya Maadili chini ya Komredi Mangula kwa kuwabana na kuwarekebisha wagombea watarajiwa wa Urais.
"Hapo CC imesifu na kupongeza mwenendo wa wahusika kwasasa na kuwaona wanaofuata taratibu za chama. Hakukuwa na mjadala mkali kama ilivyotarajiwa" kilisema chanzo hicho toka Kisiwandui.
CC pia imempongeza na kumpa baraka Rais na Mwenyekiti wa CCM Taifa kwa jinsi anavyoendelea kulishughulikia kwa weledi sakata la Escrow. Mwenyekiti ameahidi kuwa makini na mtenda haki katika hilo.
CC imeiagiza Sekretarieti ya CCM kufanya maandalizi kabambe ya Kura ya Maoni na uchaguzi mkuu kwa kutoa Ripoti mara kwa mara juu ya mikakati inayoendelea. Sekretarieti imeruhusiwa kuunda kamati mbalimbali za wataalamu ili kufanikisha maandalizi hayo.
CC imetambua na kupongeza ziara za kuimarisha chama na kukagua utekelezaji wa Ilani zilizofanywa na Sekretarieti chini ya Katibu Mkuu Kinana.
"Hayo ndiyo makubwa humo. Kikao hakikuwa na mjadala mkalí. Kilitawaliwa na busara" kimesema chanzo cha taarifa hii.
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
Imezoeleka kwamba ukizuga zuga baada ya muda fulani, wabongo wanasahau, mpaka liibuke issue jingine ndiyo watu kuhamaki kuhusu issue iliyosahaulika.Kikao hicho kinathibitisha ule msemo unaosema ukishangaa ya Mussa utayaona ya Firauni!
Hivi watanzania wataielewaje CC ya CCM, wanapoisikia inaibuka na tamko la kumpongeza JK, wakati kiporo chake cha Muhongo, kuhusiana na Escrow account, ambacho aliahidi 'kukitafuna' baada ya siku 2. baada ya kile kikao chake na wazee wa Dar, hivi sasa inakatika wiki ya tatu, kiporo hicho JK ameshindwa 'kukitafuna' kwa kuwa 'kimechacha' ile mbaya?!
Aaaaah......kakufunga?Mzee tupatupa kwa Kamba namuaminia.
Imezoeleka kwamba ukizuga zuga baada ya muda fulani, wabongo wanasahau, mpaka liibuke issue jingine ndiyo watu kuhamaki kuhusu issue iliyosahaulika.
na kura za maoni wataweka mapingamizi